GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Monday, September 24, 2012

UJUMBE: VIUMBE NA MAUMBILE HEWA.

Na Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima. Tarehe 17.6.2012

UTANGULIZI:-

Viumbe ni vilivyo umbwa , vyaweza kuwa wanadamu, vitu maji, anga na vitu vingine vyote, na Mumbile ni mtazamo au jinsi viumbe hivyo vinavyoonekana. Ni Muhimu kujua viumbe vya kiroho vinaweza kuvaa maumbile tofauti. Ndio maana Yesu alipofufuka, Mariam mama yake alimuona na kuhisi ni mtunza bustani utajuuliza kwanini mama yake hakumtambua kirahisi na wakati alikuwa naye muda wa kutosha, hii ni kwasababu Yesu alijibadili na kuwa kama mtunza bustani, na mariam akahisi ni mtunza bustani.

ROHO ZINAWEZA KUVAA MAUMBE : Kibiblia:-

Unaposoma kitabu cha mwanzo ni muhimu kujua kuwa kimeelezea kuhusu asili ya ulimwengu, mwanzo wa vitu vyote. Emu tuangalie kwa undani MWANZO 3:1-24.. HII NI HABARI YA Adamu na Hawa walipokula tunda, katika mstari wa 13 Hawa akasema "nyoka alinidanganya" lakini nyoka huyuhuyu ndio anaitwa shetani. Kumbe tangu kitabu cha mwanzo (asili) kinadhihirisha kuwa kuna uwezekano wa shetani (wa rohoni) kuvaa umbo la nyoka. Kama shetani angemtokea hawa kwa umbo lake la asili, asingefanikiwa kumdanganya hivyo ilimlazimu avae mwili. Sasa kumbe uwezekano wa kuvaa umbo upo.

Maandiko yanayoonyesha uwezekano huo:-
 • ZABURI 91:13 utajiuliza kwanini biblia inasema "utakanyaga nyoka au simba".. ukichambua kwa akili ya rohoni jambo hili; Utagundua kuwa Biblia inaonyesha uwezekano wa viumbe wa rohoni kuvaa miili.
 • LUKA 10:19 Biblia inaonyesha maumbo; kumbe unaweza kuona mtu anasema. "ugonjwa huu ulinianza nilipoumwa na mdudu" na ndio maana Mungu ametupa mamlaka ya kukanyaga nyoka na ng'e kwasababu  shetani aweza kuvaa maumbile ya hivyo vitu.
 • MARKO 16:18; Biblia inasema hata ukinywa kitu cha kufisha; yaani sumu kumbe shetani aweza kujibadili na kuwa sumu.
• ISAYA 27:1 Kumbe Biblia inaonyesha kuwa kunanyoka aliye baharini na ndio maana utaona kuna ajali zinatokea baharini, kumbe kuna shetani limejigeuza na kuwa joka baharini.

mara nyingi shetani hutenda kazi kwa kujibadilisha na kuwa kiumbe chochote ili kukuangusha, au kukufuatilia au kukutoa kwenye kusudi la Mungu. Ni muhimi kama mtu uliyeokoka kuwa makini na kujua kuwa shetani aweza kujibadili na kuwa umbo lolote ili akuteke.

SHETANI AWEZA KUJIBADILI MAUMBILE MBALIMBALI

Shetani anaweza kujibadili maumbile kwa ajili ya kutimiza azma yake aliyoikusudia, shetani akiamua kumteka mtu anaweza kutumia mtu, kitu, mti, gari au kitu chochote kutimiza azma yake. Na ndio maana Joshua alipokutana na mtu asiyemjua akamuuliza “je wewe ni wa upande wetu” Na mtu huyu alikuwa rohoni si mwilini tunaweza kuona katika kitabu cha JOSHUA 5:13-15, Joshua alijua kuwa kuna uwezekano wa shetani kujibdili katika maumbile mbalimbali. Ndio maana kwa watu walioko mikoa ya shinyanga wanajua kunavijiji wanavyoita Gamboshi, ni miji yenye watu lakini ya kichawi, yaani mapepo na mashetani wamejibadili na kuwa mji. Kumbe shetani aweza kujibadili.

KUTOKA 8:6-7 tunaona hapa kuwa Haruni alinyoosha fimbo na kutokea vyura, juu ya nchi ya Misri, na waganga wa misri wakafanya vilevile kuleta vyura juu ya nchi, utajiuliza kwanini hawa waganga waliweza kuleta vyura.. ni kwasababu shetani anaweza kujibadili kwenda kwenye maumbo mbalimbali.

UFUNUO 13:10. Yohana aliona katika ulimwengu wa roho, maumbo ya wanyama mbalimbali yote hii ni kudhihirisha kuwa shetani anaweza kujibadili, UFUNUO 13:6. shetani hapa ameonekana kama mnyama aliyetoka baharini, kimsingi yeye shetani ni roho lakini anaweza kuvaa maumbo mbalimbali ili kutenda kazi katika kutimiza azma yake. Ni muhimu kukataa na kuangamiza maumbo yote ambayo shetani anatumia ili kukushambulia. “deactivate them in The Name Of Jesus”

Na ndio maana ni rahisi mtu kukwambia, ugonjwa ulimwanza baada ya kupaliwa. kumbe shetani amegeuka na kuwa kitu cha kumpalia mtu ili kupitisha ugonjwa huo na kumfanya mtu ahisi kuwa kile kitu ndio kimesababisha. Hata kipindi cha Yesu walipokuwa wanavuka baharini na mashua ukaja upepo mkali na ukataka kuangusha kile chombo, lakini Yesu akaukemea na upepo ukatulia. Kimsingi Yule ni shetani alijibadili na kuwa upepo ili kuwazuia wasihubiri injili.

MIJI YA ROHONI.

UFUNUO 21:2 hapa tunaona kuwa Yohana aliona mji wa rohoni. Ufunuo 21:10 huu mji ambao Yohana aliona na haupo kwenye ulimwengu wa mwili na huwezi kuuona kimwili. Huu mji sio wa mwilini kwasababu Yohana akasema “ akanichukua katika roho” maana yake hakuwa katika ulimwengu wa mwili bali wa Rohoni. Na ndio maana hata shetani huiga “imitator” na kufanya miji duniani ili kuendesha shughuli zake. Ndio maana watu wengi wanaokufa katika mazingira ya kutatanisha “misukule” nao hupelekwa kwenye hiyo miji ya rohoni.

Hata kuzimu ni mji wa rohoni, ambao Yesu alipokufa alishuka kuzimu nakumlaani shetani, kuzimu ni mji wa rohoni.

USHINDI DHIDI YA VIUMBE HEWA.

1. Tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na ng’e na nguvu zote za Yule muovu, wala hakuna kitu kitakacho kudhuru kwa namna yoyote ile.

2. Pia twaweza kuwashinda viumbe wa rohoni kwa kunena kwa lugha mara kwa mara, ambapo unamruhusu Roho mtakatifu akupiganie, hivyo viumbe vya ajabu vitajikuta vinajitenga na wewe.

3. Maombi pia ni silaha Kubwa dhidi ya viumbe vya hewa. Maombi yanalazimisha viumbe hivi kuondoka mahali ambapo walianza kujijenga kwa muda mrefu. Maombi yanauwezo wa kuangamiza ngome.

4. Sisi ni rungu la Bwana ambaolo kwa sisi, Mungu hufyeka farasi na mpanda farasi(viumbe hewa) kumbe hakuna wakufyeka ila sisi tuliookoka.


kunauwezekano wa kuwepo mji kabisa katika ulimwengu war oho kwaajili ya uhalibifu. Kuleta uhalibifu.. katika ulimwengu waroho kuna miji lakini ya rohoni.

Mungu wetu ni Mungu Mtakatifu, wa upendo, hakuna kama yeye.. ni Mungu mkuu mno.. atufunuliaye mambo ya rohohoni maagumu tusiyo yajua.. na wala kuyawazia. MUNGU ANATUPENDA SANA.

Ufufuo na Uzima (The Glory Of Christ (T) Church)
Tanganyika Packers,
Kawe, Dar es Salaam.

Sunday, September 23, 2012

UJUMBE: NYOTA KIBIBLIA


Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima 23.9.2012



UTANGULIZI:

Huu ni mwendelezo wa somo la Nyota na Maisha mtu aliyonayo. Mathayo 2:1; Kama tulivyoona tangu mwanzo kuwa nyota ni kipawa, uweza, hatma au hali ya mtu ya baadaye. Tukaona nyota ya Yesu ilionekana kabla Yesu hajazaliwa na mamajusi wa mashariki walimwona kama Mfalme.



MAANANYOTA:

Kama tulivyooa sehemu ya kwanza kuwa nyota ni kiashiria cha rohoni, kinachoonesha mtu atakuwa nani baadaye, mafanikio ya mtu au hatma ya mtu. Viashiria hivi ndivyo vinavyoitwa nyota.



NYOTA KATIKA BIBLIA:

Hesabu 24:14-17 Baraki alikuwa mfalme, na alipoona kuwa wanaisrael wanakuja ili kushambulia ufalme wake, akamtafuta Balaam amtabirie. Hayo ni maneno ya Balaamu aliyoona, Hivyo Balaamu alipoangalia taifa la Israel akaona nyota, kimsingi nyota ya mtu inaonyesha jinsi mtu atakavyokuwa baadaye. Hivyo balaamu aliweza kumuona Yesu tangu mwanzo na ndio maana mamajusi wa mashariki nao pia walimwona Yesu kama nyota.



Nyota yaweza kuonyesha kusudi la maisha ya mtu, na ndio maana ingawa Suleimani alizaliwa na mke wa Huria ambaye Daudi alimuua mumewe ili ampate lakini kwasababu nyota ya kujenga hekalu ilikuwa juu yake (yaani Suleimani), Mungu alimchagua kujenga Hekalu. Daudi alikuwa na watoto wengine wengi, lakini aliyechaguliwa kujenga ni Suleimani kwasababu ndio mwenye nyota ya kujenga yaani tangu anazaliwa



Isaya 47:8-12; Hapa biblia inataja neno “wajuao Falaki”, hii ni elimu inayohusu mambo ya nyota ambayo wachawi husoma. Katika Mathayo 2:1- Biblia inataja mamajusi, wao ni wasomaji wa nyota ambao waliiona nyota ya Yesu kabla ya Yesu hajazaliwa. Nyota ya Yesu iliwafanya mamajusi kumfuata kutoka mbali, na wakati huohuo Herode alifadhaika. Kumbe nyota ya mtu ikionekana watu wanaweza kuifuata na kukuletea unalohitaji. Watu wengi wapo katika vifungo mbalimbali kwasababu nyota zao zimefunikwa.



MAMBO 15 AMBAYO UTAYAONA KAMA NYOTA YA MTU HAIPO:

·        Umahiri na utendaji kazi wa mtu hauonekani; kama mtu hana nyota ule umahiri wa wake na utendaji kazi hauwezi kuonekana. Hata ajitahidi kufanya kazi kwa bidii umahiri hawezi kuonekana.

·        Hawezi kuwa mbunifu katika maisha; nyota huleta ubunifu sasa kama haipo basi ubunifu wa mtu hautaonekana. Mtu huyo atakuwa anashindwa kubuni kitu cha kufanya ili kupata mafanikipo katika maisha.

·        Hawezi kufanya kazi zake kwa ufanisi; nyota huleta ufanisi katika kazi, mtu akikosa nyota basi ule ufanisi wake hauwezi kuonekana, mtu huyo atakosa ufanisi katika kazi zake.

·        Hukosa mvuto; nyota huleta mvuto hivyo mtu nyota yake haipo, anakuwa anakosa mvuto hata wa watu kuomuona tena.

·        Hukosa kibali; nyota humfanya mtu awe na kibali hivyo mtu anapochukua nyota, kimsingi anakuwa amechukua kibali chako.

·        Huwezi kusikilizwa katika jamii; kwasababu nyota huleta kusikilizwa, mtu akichukuliwa nyota hawezi kusikilizwa katika jamii.

·        Hawezi kuthubutu;

·        Anakosa uthubutu wa kutenda;

·        Anakosa ujasiri wa kusema; mtu akikosa nyota anakosa ujasiri wa kusema.

·        Anakosa uthubutu wa kutoa maamuzi magumu; mafanikio ya mtu ni matokeo ya maamuzi magumu aliyowahi kuyafanya.

·        Anakosa ujasiri wa kudai unachojua ni kweli;

·        Huwezi kutumia hata kile ulichonacho; ndio maana ya lile andiko utajenga nyumba na mtu mwingine atalala ndani yake”.

·        Anakuwa na matatizo;

·        Anakuwa na hofu ya kutenda mapenzi ya Mungu; nyota ikichukuliwa mtu aweza kuwa na hofu ya yajayo, yaliyopo au yaliyopita.

·        Kukosa uaminifu kwenye mambo ya Mungu.



Kwahiyo wachawi au waganga wanapochukua nyota yako kimsingi, mambo hayo yanakuwa hayapo kwenye maisha yako.



JINSI WACHAWI WANAVYOCHUKUA NYOTA NA MATUMIZI YAKE:

Utajiuliza ni wakina nani wenye uwezo wa kuiona nyota; biblia inathibitisha kuwa waganga na wachawi wana uwezo wa kuiona nyota na kuifuata. Na kama nyota haina ulinzi wa Mungu waganga wanaweza kuichukua nyota. Kuna watu wanadhania kuwa uchawi haupo na kutokujali uwepo wake, lakini uchawi upo kwasababu biblia imetaja kuwa uchawi upo.



Wanachuaje; kwasababu wachawi wanaweza kuiona nyota ya mtu na kuifuata, hivyo wakigundua kuwa nyota ni nzuri wanaweza kuichukua na kumuuzia mtu mwingine; na ndio maana mtu anaweza kuzaliwa nyota ya uongozi, ujasiri, upendeleo, ubunifu au kupata kibali mbele za watu, alafu ikachukuliwa na kupewa mtu mwingine. Na ndio maana kuna watu ni matajiri kwasababu ya nyota za watu; na wakati huohuo mtu Yule ambaye nyota yake oimechukuliwa anaanza kuwa na matatizo; kile kibali au upendeleo aliokuwa nao awali hawezi kuwa nao tena.



Mtu aliyechukuliwa nyota; anakuwa na mafanikio mwanzoni lakini ghafla yanabadilika baada ya kuchukuliwa nyota. Kimsingi; Mungu akikupa kutu huwa kinadumu lakini kama maisha ya mtu yanaashiriwa na nyota pale nyota inapochukuliwa mtu huyo upendeleo wake unaanza kuondoka. Rudisha nyota yako kwa Jina la Yesu.



Maombi ya kuamuru aliyechukua Nyota yako arudishe:

Baba katika Jina la Yesu leo nimetambua kuwa nina nyota, nayo yaweza kuchuliwa na kunitia katika matatizo; hivyo ninaamuru ila aliyechukua nyota yangu arudishe katika Jina la Yesu. NInapokonya nyota yangu iliyochukuliwa katika Jina la Yesu, naamuru mahali popote ilipowekwa na kutumika ninaamuru irudi kuanzia sasa katika Jina la Yesu.



Ninaamuru umahiri wangu, ufanisi, uwezo wangu wa kutenda na uwezo wa kuthubutu ninaurudisha katika Jina la Yesu. Ninaamuru kibali, afya, ujasiri na mvuto wangu urudi katika Jina la Yesu; nataka nyota yangu katika Jina la Yesu.

UFUFUO NA UZIMA {THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH}
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM.

Sunday, September 16, 2012

NYOTA YA MTU NA MAISHA ALIYONAYO

 
Na Mchungaji Josephat Gwajima  16.9.2012

Utangulizi:
Biblia imeeleza kuhusu nyota ya Yesu ilivyoonekana  kutoka mashariki,(Mathayo2:1); Hii inadhihirisha wazi kuwa kila mtu ana nyota yake. Hivyo katika mfulilizo wa somo hili tutaona maana ya nyota, kazi ya nyota, nyota yaweza kufunikwa kichawi, madhara ya kuishi bila nyota, dalili za kuchukuliwa nyota, nyota yaweza kurudishwa na namna ya kutambua nyota yako. Hapa hatuzungumzii kuhusu kusoma nyota au utabiri wa nyota bali tunaangalia nyota kama ilivyo katika Biblia.
MAANA YA NYOTA:
Nyota katika Biblia inawakilisha kipawa, hatma ya mtu, lengo lililomfanya Mungu akulete  hapa duniani na kusudi lako la maisha. Hivyo tunaposema nyota yako ipo au imechukuliwa maana yake hayo mambo yamechukuliwa au yapo. Kimsingi hakuna mtu asiye na maana tangu kuzaliwa kwake, kwasababu kila mtu aliye duniani amekuja kwa kusudi lake.
Kuna tofauti kati ya elimu na nyota; elimu sio nyota lakini elimu yaweza kunoa nyota. Na si kwamba kujifunza kunaleta nyota bali nyota ipo kwa wote lakini elimu inainoa nyota; na ndio maana ni rahisi kumwona mtu hana elimu lakini anamafanikio mahali fulani. Ukisoma Mhubiri 9:11 Biblia inasema wakati na bahati huwapata wote na sio swala la elimu au ujuzi tu.
KAZI YA NYOTA:
1.       Nyota humfanya mtu kuwa mahiri katika utendaji kazi wake. (Effectiveness)
2.       Nyota huleta ubunifu katika maisha ya kila siku (Creativity)
3.       Nyota inamfanya mtu anatenda kwa ufanisi (Efficiency)
4.       Nyota huleta mvuto kwa watu kutoka mbali ili kuleta vitu kwa ajili yako. (Attraction)
5.       Nyota humfanya mtu awe na maisha yenye mwelekeo na kibali mbele za watu. (Acceptance  and Favor)
6.       Nyota humfanya mtu kusikilizwa katika jamii.
Kuna vitu ambavyo mtu anaweza kuvipata kwasababu nyota yake imeonekana. Nyota yaweza kuvuta zawadi yaani vile vitu ambavyo hujavitaabikia, na ndio maana Yesu alipokuwa mdogo aliletewa zawadi na mamajusi wa mashariki. (Mathayo 2:11) kwahiyo nyota ikichukuliwa maana sahihi ni kwamba hayo mambo hapo juu yote hayapo.
Mathayo 2:1-2; Wakati Yesu anazaliwa kulikuwa na watu wanaitwa mamajusi, ambao walikuwa na uwezo wa kusoma nyota. Hivyo katika ulimwengu wa roho waweza kuona watawala wajao, maisha yajayo au yale yatarajiwayo.  Na ndio maana Mamajusi wa mashariki ya mbali waliweza kuifuata nyota ya Yesu.
Nyota inapoonekana inaweza kufuatwa, yaani watu waona zile kazi zake na kumfuata mtu. Kimsingi tunaposema mtu hana nyota maana yake umahiri, ufanisi na kibali vimechukuliwa. Lakini nyota ikionekana  maana yake haya mambo yote yamerudishwa na hapo utamwona mtu anafanikiwa hata kama elimu yake sio kubwa.
NYOTA ILIYOCHUKULIWA/ ILIYOFUNIKWA KICHAWI:
Nyota ikifunikwa au kuchukuliwa kichawi maana yake mvuto, umahiri, ufanisi na uwezo unakuwa umechukuliwa au umefunikwa. Na ndio maana kuna watu wanahangaika kuanzisha kampuni, kujenga nyumba, kulima, au kufanya biashara kama nyota imefunikwa au kuchukuliwa kichawi huwezi kupokea mafanikio ya sahihi kwenye maisha. Watu wengi wanahangaika kuonekana au kukubalika lakini kumbe tatizo lipo kwenye nyota yaani imefunikwa au imechukuliwa kichawi.
Wachawi wanaweza kuona nyota ya mtu na kuifunika ili isionekane; na kwa namna hii watu wengi wanaonekana hawana mafanikio katika maisha kumbe nyota zao zimefunikwa. Hivyo ni muhimu kupambana Kwa Jina la Yesu ili nyota yako ionekane.
MADHARA YA KUISHI BILA NYOTA YAKO:
  •   Kwa kuwa nyota ndiyo inamwezesha mtu kuwa na kila kitu, ndio kusudi la mtu, upendeleo wa mtu; hivyo madhara ya kutokuwa na nyota ni kutokuwa navyo vyote vile.
  •  Siku zote unakuwa unatenda chini ya kiwango (Under performance). Na kwa namna hiyo hakuna mtu anakubali kile unachotenda; yaani elimu na maarifa yote yakuwa chini ya kiwango.
  •  Utapata na kuibiwa; unapata kazi baadaye unaibiwa au unapata mchumba baadaye anaibiwa. Kimsingi huwezi kudumu na haya mambo.
  • Unapata lakini anatumia mtu mwingine.

DALILI ZA NYOTA ILIYOFUNIKWA:.
Ø  Maisha kukosa mwelekeo; mtu akikosa nyota hata kama akiwa na elimu kama nyota haipo lazima mtu huyo atakosa mwelekeo.
Ø  Kukwama kibiashara na kuishi maisha kwenye madeni.
Ø  Unafanya kazi lakini hupati maendeleo. Yaani mtu anapata mshahara mzuri lakini anakosa mafanikio halisi kwasababu ya nyota iliyofunikwa au kuibiwa.
Ø  Wewe ni kiongozi lakini jamii haikutambui.
Ø  Ukichangia hoja za mijadala mbalimbali hakuna anayekusikiliza.
Ø  Umesoma lakini hupati kazi, na ukipata kazi haiendani na elimu yako
Ø  Maisha ya upweke na hakuna anayekujali katika familia.
Ø  Unatenda kazi kwa bidii lakini hupandi cheo.
Ø  Kama ni binti  sifa zote lakini hakuna anayekuchumbia maana huonekani.
Ø  Kuandamwa na mabalaa na mikosi.
Ø  Kupotelewa na watu wa muhimu
NYOTA YAWEZA KURUDISHWA:
Hatua ya kwanza kama hujaokoka unatakiwa kuokoka; kuokoka ni kumpokea Yesu awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako ili upate uwezo wa kushindana, hivyo ukigundua nyota imechukiliwa unatakiwa umpokee Yesu ndani ya moyo wako. Ni kitu cha kushangaza kuhitaji msaada wa Yesu halafu yeye humtaki kimsingi kuokoka ni hatua ya kwanza ya kurudisha nyota.
Hatua ya pili ni kushindana kwa maombi; kama mtu anayetaka kurudisha nyota yake ni lazima achukue hatua  ya kushindana katika maombi. Hivyo baada ya kuokoka hatua inayofuata ni kushindana ili nyota irudi. Nyota yaweza kurudishwa kwa kuomba katika Jina la Yesu Kristo.

UTAJUAJE NYOTA YAKO NI IPI:
Usithubutu kwenda kwa mganga wa kienyeji au kusoma kwenye magazeti ili kujua nyota yako.  Ni muhimu kujua kilichoibiwa ni kipi katika maisha yako. Isaya 47:13Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na wasimame hao wajuao falaki, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata.FALAKI ni elimu juu ya mambo ya nyota; biblia inataja kuwa kuna watu wanaojishughulisha na usomaji wa nyota. Lakini kuna mambo kadhaa yanayoweza kukuonyesha nyota yako ni ipi:-
Moyo wako, akili zako na mawazo yako yanakuwa katika hilo jambo AMBALO NI NYOTA YAKO. Mfano kama nyota yako ni biashara basi utakuta moyo wako upo kwenye biashara, basi lazima nyota yako ni k biashara. Kama nyota ni kuimba au siasa lazima moyo utakupeleka kwenye kuimba na siasa. Hivyo tambua kuwa kwenye nyota yako ndipo kuna Baraka zako.
Jambo ambalo ni nyota yako utalitenda bila kupambana; Yaani hutatumia nguvu kwenye kulitekeleza jambo hilo.

MAOMBI YA KURUDISHA NYOTA:
Kurudisha nyota Iliyoibiwa:
Baba katika Jina la Yesu, nimetambua kuwa nyota yangu yaweza kufunikwa na kuibiwa; na leo ninaamua kuirudisha kwa Jina la Yesu kila nyota yangu iliyoibiwa, nyota ya kukubaliwa, ufanisi, umahiri, biashara, kazi au nyota ya hatma njema naamuru irudi kwa Jina la Yesu Kristo. Ninaamuru nyota yangu ikombolewe kwa damu ya Yesu, ninaamuru iachiliwe katika Jina la Yesu.



Kufunua nyota iliyofunikwa:
Katika Jina kuu la Yesu ninasafisha nyota yangu iliyofunikwa; nyota ya mafanikio ninaisafisha kwa Jina la Yesu. Katika torati kila kitu husafishwa kwa Damu nami natumia Damu ya Yesu kusafisha nyota yangu katika Jina la Yesu. Ninatakasa nyota yangu iliyochafuliwa katika Jina la Yesu.  Ninang’arisha nyota yangu katika Jina la Yesu.

Kuangamiza wasimamizi wa nyota:
Ninasimama kinyume na kila mashetani, wachawi na waganga wa kienyeji wanaoshikilia nyota yangu katika Jina la Yesu. Waliofunika nyota ninawaangamiza katika ulimwengu wa roho, ninateketeza wote walioiba nyota yangu kwa Jina la Yesu. Katika Jina la Yesu niharibu kazi na utawala wa mashetani wanaoiba nyota yangu katika Jina La Yesu.

Kukiri ushindi:                           
Ninatangaza kurudishwa kwa nyota yangu katika Jina la Yesu; ninatangaza maisha yangu kung’arishwa katika Jina la Yesu. Mafanikio yangu yamerudi katika Jina la Yesu. Nimeshinda  kwa damu ya Yesu.

UFUFUO NA UZIMA (THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH)
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DARES SALAAM.

Friday, September 14, 2012

UTOTO (KIFUNGO CHA UTOTO)

Na Pastor Adriano Makazi:

Unapo kuwa mtoto mdogo unakuwa huwezi kujitegemea kwa jambo lolote lile hadi usaidiwe na mzazi au mkubwa wako aliye kuzidi umri.

Utoto si udhaifu au ugonjwa bali ni hatua ambayo kila mtu ameipitia au anaipitia.

Mfano mzuri tunaona hata YESU mwenyewe alipo vaa mwili alivaa umbo la utoto hii ni kuonyesha kuwa ni lazima hatua hii kila mmoja wetu aipitie.


KUNA AINA TATU ZA UTOTO
1: Utoto wa kimwili. (mwilini)
2: Utoto wa kiroho. (rohoni)
3: Utoto wa akili. (nafsini)

Mtoto wa kimwili anakuwa hajui na hafahamu na hawezi mambo mengi yahusuyo mwili

Mtoto wa kiroho anakuwa hajui na hafahamu na hawezi mambo mengi yahusuyo roho

Mtoto wa akili anakuwa hajui na hafahamu na hawezi mambo mengi yahusuyo kutumia akili(mfano kufikiri, kuwaza, kutafakari, kuamua kwa usahihi n.k)

Kwa kuwa kila kitu kinaanzia kwenye hali ya utoto na kinakuwa taratibu hadi kufikia hali ya utu uzima ndio maana Mungu alituonyesha hili kupitia mwanawe Yesu,jinsi alivyo zaliwa na hadi akakuwa na hatimaye akaanza kazi katika utu uzima.

Watoto huwa wanapatikana kwa uchungu mwingi na maumivu makali,

Angalia jinsi mwanamke azaapo mtoto wake jinsi anavyo zaa kwa uchungu na maumivu makali.

Angalia jinsi Mungu alivyo tuzaa sisi kwa uchungu mwingi kwa kumtoa mwanawe wa pekee Yesu akafa kwa ajili yetu sisi.

Angalia jinsi Yesu alivyo tuzaa sisi kwa njia ya mateso mengi (kupigwa mijeredi,kutemewa mate,kipigiliwa misumari,kuvalishwa taji ya miiba,kufa msalabani,kuchomwa mkuki ubavuni.

Mtoto yeyote azaliwapo anazaliwa akiwa amebeba kusudi la Mungu ndani yake tangu tumboni mwa mamaye.

Mfano=Yesu,Yohana mbatizaji,Yeremiha,Samsoni,Gidioni,Yoshua,Musa n.k


KWA NINI MUNGU ANARUHUSU TUPITIE UTOTO?

  • Kwa sababu ni hatua ambayo kila mtu lazima aipitie ndipo awe mtu mzima baadaye.
  • Kwenye utoto ndio sehemu ya kujifunza mambo mengi na vitu vingi vya aina mbalimbali.
  • Kwenye utoto ndipo tuna jifunza unyenyekevu.
  • Kwenye utoto ndipo tunajifunza utii
Mungu anapo kuweka kwenye utoto anatazamia ujifunze mambo mengi ili uwe mtu ajuae vitu vingi baadaye na uweze kutumika vizuri na yeye.

MIKATABA YA ITOKANAYO NA MANENO ANAYOKUTAMKIA MTU


Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima.     14. 9. 2012


Utangulizi:
Kuanzia mwanzo wa wiki hii tumekuwa tukijifunza kuhusu mikataba inayotokana na maneno; na tuliona kuwa maneno yaweza kuleta mikataba, na hasa tulijifunza zaidi juu ya maneno anayotamka mtu binafsi; Pia tuliona maandiko kadhaa Mithali 6:2; na pia tukaona kuwa uweza wa laana au baraka upo katika maneno ambayo mtu anatamka Kumbukumbu la torati 30:15, 19; hivyo tulijikita zaidi katika mikataba ya maneno mtu anayojitamkia. Leo tutaona maneno ambayo mtu anatamkiwa na mtu mwingine.

MANENO YA KUTAMKIWA NA LAANA:
Mwanzo 9:18-29; kuna mambo ya kuangalia; Hamu baba wa Kanaani akauona uchi wa baba yake, akaenda kuwaambia nduguze ( ukiangalia hapa nani mwenye kosa waweza sema ni aliyelewa na kukaa uchi) Lakini wanawe wengine wawili walipomuona wakamfunika baba yao. Lakini katika Mstari wa 25’ Nuhu katoka kwenye ulevi, akamlaani mototo wa aliyemuona akiwa uchi.

Tunaona hapa, tatizo kubwa lilikuwa Hamu kuwaelezea wenzake kuwa baba yake yuko uchi. Lakini Nuhu alimlaani Kanaani ambaye ni mototo wa Hamu; na wana wakanaani ndio wanaotajwa katika kitabu cha  Mwanzo 10:15-20; Kutoka 3:8; Kutoka 23:23; Joshua 24:11. Hii laana ya Kanaani ndiyo iliyokuja kuwadhuru watoto wake yaani Wahivi, Wakanaani, Wayebusi na hii ndiyo laana inayowatafuna. Lakini ukiangalia mwanzo ilianzia kwenye maneno ambayo Nuhu alitamka kwa wajukuu wake.

LAANA INATENDAJE KAZI:
Waefeso 6:1 “ Enyi watoto watiini wazazi wenu katika BWANA, maana hii ndiyo haki”; kimsingi watu anawazi wa rohoni na wa mwilini; wazazi wa rohoni wanaitwa Wazazi katika BWANA.  Na katika Waefeso 6:2 “waheshimu baba na mama yako, uwe na heri…”  Neno hili uwe na heri… linatajwa kwenye biblia ya kingereza  kuwa “It may be well with you” YAANI ili mambo yakuendee vizuri; hivyo kumbe kuna uwezekano wa mtu kuwa anaenenda vibaya kwasababu ya kutokuwaheshimu wazazi. Na hapa ndipo Nuhu alitamka maneno ya Laana kwa watoto wake na yakatimia.

Sasa kitu kinachotokea ni kwamba; Yesu alisema “maneno niwaambiayo ni roho tena ni uzima” na pia biblia inasema “Kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafundisho” kumbe kuna maneno yenye pumzi au roho ya shetani. Na ndio maana waweza kumuombea mtu kwa maneno na akafufuka kwasababu maneno yale ni roho. Hivyo kama ukimkosea mzazi akatamka maneno juu yako, yale maneno kwakuwa ni mabaya, mashetani yanakuwa nyuma ya yake ili wasimamie yatimie. Hivyo nyuma ya maneno kuna roho, aidha ya roho takatifu au roho chafu.
“KAMA UNATAKA KUWA MTU WA MUNGU MZURI; TUMIA MANENO YAKO VIZURI”

ROHO ILIYO NYUMA YA MANENO:
Mpaka hapa tumeona kuna roho nyuma ya maneno; na ndio maana Hesabu 14:28-29 Mungu anasema nitawatendea yale ninayo yasikia mnasema, kumbe maneno ambayo mtu anayatamka yana nguvu nyuma yake ya kuweza kutokea.  Sasa maneno mabaya yanapotamkwa juu ya mtu; mashetani wanachofanya ni kuyachukua maneno hayo na kuyatimiza kwa mtu aliyetamkiwa.  Mfano mzazi akikutamkia maneno labda hutazaa, utakuwa kichaa, hutafilisika au tutaona utakapooa. Hayo maneno yanaweza kuwa kifungo kwenye maisha ya mtu.

Na ndio maana katika kitabu cha Mithali 26:2; Biblia inasema, “…laana isyo na sababu haimpigi mtu…” kwaiyo kumbe kama laana inasababu itatenda kazi bila shaka. Kwasabu kuna mashetani wanasimamia laana. Na ukiangalia kwa habari ya Elisha na Naamani, Baada ya Naamani kutakaswa alitaka kumpa hela Elisha,  Elisha akakataa lakini baada ya muda mtumishi wa Elisha Gehazi akaenda kwa Naamani na kutaka mali kwako, matokeo yake Elisha alipojua kwa roho wa Mungu,; akamtamkia kuwa uwe na ukoma. Na kuanzia saa ile Gehazi akawa na Ukoma. Kumbe mtu awezakuwa kwenye kifungo kwasababu ya maneno aliyowahi kutamkiwa.

Kumbe; kuna watu wapo kwenye vifungo vya magonjwa, kutokuzaa, kutokuolewa au matatizo mbalimbali kwasababu ya maneno ya kutamkiwa. Kumbukumbu 28:15-. Hapo zinatajwa laana nyingi hapo, kumbe laana hata za maneno zaweza kuja kwa namna ya matatizo, kupungukiwa, kushindwa, kukata tama n.k. Inawezekana wewe hukutamkiwa maneno, lakini baba au mama yako alitamkiwa ulipokuwa tumboni ni muhimu kuvunja maneno hayo.

MAOMBI BAADA YA SOMO:
Baba Katika Jina la Yesu Kristo; leo ninasimama kinyume na maneno yote niliyotamkiwa, katika Jina la Yesu. Maneno ya kushindwa, ya kukata tama au ya kutokufanikiwa, ninafuta maneno yote kwa Jina la Yesu. Ninafuta maneno niliyotamkiwa nikiwa mdogo ninayafuta kwa Jina la Yesu. Ninaamuru maneno hayo yote hayatatimia katika Jina la Yesu. Yeyote aliyatamka awe baba, au mama au mtu yeyote; ninayafuta maneno niliyotamkiwa kwenye ndoa, kwenye mahusiano ninayafuta Katika Jina la Yesu.

Kazi iliyopotea kwasababu ya maneno ya kutamkiwa, niaamuru uarudishwe katika Jina la Yesu. Ninakataa kupoteza katika Jina la Yesum nikipata nimepata katika Jina La Yesu.  Ninatangaza ushindi na mafanikio kwenye maisha yangu katika Jina la Yesu, natangaza Baraka Juu yangu kwa Jina la Yesu.

UFUFUO NA UZIMA {THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH}
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM 


MAKE GOD YOUR NO 1.

While I was preaching, I identified several young ladies who did not have husbands.
I suggested to them to get married to a nice young man in church. They all refused.

“Why don’t you want to marry him, is he not a handsome man?”
“Yes he is,” they answered.
“Is he a spiritual person?”
“Yes he is. He is even a pastor.”
“Does he not have a car and a house?”
“Yes he does. Actually his car is very nice.”
“Then why don’t any of you want to marry him?”
“Because he has a wife already,” they answered.
I continued, “But you can be his second wife?”
In chorus they all cried out, “No way, no sir, we will not be second wives, we want to be number one.”

They felt insulted that I would offer them the second position. They wanted to be wives but not second wives. These young ladies wanted to be wives but only if they would be the FIRST AND ONLY wives.

THIS IS HOW GOD FEELS.

 He knows we will serve Him but He wants us to serve Him FIRST. It is actually an insult to put God after anything! Unfortunately, God is constantly relegated to the second, third and sometimes tenth place of importance. It is time for God to take His PROTON (foremost) position in your life.

Thursday, September 13, 2012

DOUBT YOUR DOUBTS (T B Joshua)


The promise of God can only be appropriated by faith which comes through hearing and obeying the Word of God. In Romans 8:35-39, Paul advised Christians to keep their solid front in the face of hard times. Don’t doubt the genuineness of your spiritual experience or question your sonship in Christ because of your situation. God has promised to respond only to the faith that is produced by and rests in His Word or promise. From now on, don’t doubt your faith; doubt your doubts for they are unreliable.

Sunday, September 9, 2012

UJUMBE: MIKATABA YA DAMU


Na Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima. 9.9.2012

UTANGULIZI:
Katika mfululizo wa masomo haya tayari tumekwisha kujifunza kuhusu kafara ya damu na tukaona pia kuhusu Kafara ya mwanakondoo ambaye ni Yesu kristo. Leo tunaangalia kuhusu mikataba inayoweza kusababishwa na damu iliyomwagika.

TABIA ZA DAMU KATIKA BIBLIA:
Mwanzo 4:10; Adamu alikuwa na watoto wawili mmoja aliitwa Kaini na mwingine Habili; Kaini alipomuua Habili; Mungu akamwambia Kaini, Damu ya ndugu yako inanililia. Kumbe damu yaweza kulia na inaweza kuongea pia.

Kumbukumbu 12:23 Mungu anasema kuwa “…damu ni uhai”. Kumbe damu ina uhai; kwa namna hiyo kuna tabia kadhaa za damu:
i)                   Damu ina sauti
ii)                 Damu yaweza kulia
iii)               Damu inaleta laana
Na ndio maana Mungu amekataza kula au kunywa damu, hii ni kwasababu hizi tatu Kumbukumbu7:27; Walawi 17:10,12

DAMU INA SAUTI (INANENA):
Damu iliyomwagika chini inaweza kunena mema au yaweza kunena mabaya,damu inenayo mema ni ya Yesu peke yake, Waebrania 12:24 inasema, “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.Kumbe kuna damu inayonena mema (damu ya Yesu Kristo) na pia kuna damu inayonena mabaya (damu ya wanyama,ndege hata watu)

Damu yaweza kuongea mabaya juu ya mtu; damu ikimwagwa hunena na ndio maana hata nchi yaweza kuingia kwenye matatizo kwasababu ya damu inenayo iliyomwagika.

Mambo ya Walawi 19:26 Msile kitu cho chote pamoja na damu yake; wala msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi. Mungu amekataza kula nyama pamoja na damu kwasababu damu ni uhai, na ina sauti. Na ukiangalia katika biblia kila mahali ambapo damu imekatazwa na uchawi pia umetajwa. Kwa maana hiyo tunajifunza kuwa uchawi upo na unaushirikiano wa karibu na matumizi ya damu.

MAFUNDO YA KICHAWI:
Ukisoma Ayubu 15:26 Humshambulia na shingo ngumu,  Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;mafundo yapo na wachawi ndio wanayo yafunga. Wachawi wanaweza kuloga katika kufunga mafundo, hivi ni vifungo vya kichawi ambavyo hutumia kudumisha maisha ya watu. Kumbukumbu 18:11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. Kuna mafundo ya aina mbalimbali mojawapo ni mafundo ya maamuzi; yaani mtu anashindwa kuwa na maamuzi, na ndio maana watu wengi wanashindwa kupiga hatua kwenye maisha kwasababu wamefungwa katika maamuzi.

Wachawi pia hutumia mafundo haya kufunga matumbo ya kina mama ili wasipate watoto; na ndio maana ya maandiko yale yanayosema Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.Mathayo 18:18. Kwenye ulimwengu wa mwili mtu anaweza akaonekana anaumwa au ana matatizo lakini katika ulimwengu wa roho anakuwa amefungwa. Luka 13:16 huyu mwanamke alionekana amepooza kumbe shetani alikuwa amemfunga.

DAMU INAVYOTENDA KAZI:
Sasa kwa kujua kuwa kila damu iliyomwagwa inauwezo wa kusema, wachawi hutumia tabia hiyo ya damu kufunga maisha ya watu. kwahiyo wanachofanya wachawi au waganga ni kuchukua mnyama na kumchinja yule mnyama na kuinuizia inene tatizo lako. Kimsingi; hii damu iliyomwagwa ndiyo inayoitwa madhabahu ya tatizo lako. Na ndio maana waganga wa kienyeji huagiza kuku, mbuzi au ng’ombe ile ni kwa ajili ya kumwaga damu ili inene  mabaya juu ya mtu.

Damu inapomwagwa inatoa sauti; yaani katika ulimwengu wa roho ni sauti kubwa ili mtu akae katika tatizo; kinachotokea pale damu inaponena mashetani husikia rohoni na kwa njia hiyo mashetani yanapata mlango wa kuingia kwenye maisha ya mtu. Hivyo mashetani huja ili kutekeleza sauti ya ile damu inayonena. Kwa njia hiyo shetani amefunga maisha ya watu na kifungo kinakuwa kikubwa kulingana na wingi wa damu iliyomwagwa

DAMU INAYOTOKANA NA KUCHANJWA CHALE:
Biblia iko wazi sana kuhusu kuchanja chale kwenye miili ya watu. Mambo ya Walawi 19:28 Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi Bwana. Mambo ya Walawi 21:25; Yeremia 48:37 Yaani; mtu huyu sio kwamba imemwagwa damu ya mnyama kwa ajili yake bali anakuwa amechanjwa mwenyewe kwenye mwili na ameitoa damu yake mwenyewe. Kimsingi; mganga anapokuwa anachanja chale huwa ananena maneno ambayo huwezi kuyaelewa. Yale maneno ndio sauti ya ile damu iliyo mwagwa.

Utajiuliza kwanini Mungu anakataza watu kupigwa chale; kimsingi damu inayomwagika ni uhai wako, kwa lugha rahisi ni kwamba unapochanjwa  chale unakuwa umeacha uhai wako kwa mganga wa kienyeji. Hivyo mganga anaweza kukuona na kukufuatilia kirahisi, hivyo akiamua kukufanya urudi kwake anaweza kukurudisha kirahisi kwasababu uhai wako umeuacha kwake.

DAMU YA YESU KRISTO:i                                                                                                           
Unaweza ukajifunza kwanini Yesu alipokuja duniani asingekufa kwa kuumwa au njia nyingine ambayo haimwagi damu, Siri kuu ya kuja Yesu duniani ni kwa ajili yetu sisi tufunguliwe na kutoka kwenye vifungo kwa damu ya Yesu ambayo yenyewe hunena mema daima.

Yaani Mungu alipoaamua kumkomboa mwanadamu ikamlazimu kuvaa mwili ili aje kuukomboa ulimwengu. Na ndio maana aliitwa Immanuel yaani Mungu pamoja nasi, naye alipokuja duniani akaenda msalabani ili atengeneze madhabahu yake kwa njia ya kumwaga damu. Na nguvu ya damu ya Yesu ni kuwa hakutenda dhambi hivyo damu yake ina nguvu dhidi ya madhabahu zote za giza.
Wakati wao wanaitia damu za mafahari na mbuzi sisi tunanena damu ya Yesu, inayonena mema. Kwa kutumia damu ya Yesu twaweza kunyamazisha damu nyingine za giza.

Ibada ilimalizika kwa maombi:
Baada ya kujifunza somo hapo juu omba hivi;
Kamata kuhani wa madhabahu:
Ninakamata kuhani wa madhabahu  kwa jina la Yesu. Kila wachawi na waganga wote wanaosimama kama kuhani wa madhabahu, ninawakamata kwa jina la Yesu. Ninaharibu kazi zao katika jina kuu la Yesu Kristo. Imeandikwa mtakalolifunga duniani na mbinguni litakuwa limefungwa; ninawakamata na kuwafunga wote Katika Jina La Yesu.


Bomoa Madhabahu:
Katika jina lenye Nguvu la Yesu Kristo ninaharibu kila madhabahu za kishetani kwa Jina La Yesu. Ninabomoa madhabahu zinazoleta vifungo kwenye maisha yangu katika Jina La Yesu. Madhabahu za magonjwa, mikosi na laana ninazibomoa na kuzisambaratisha katika Jina la Yesu. Ninateketeza madhabahu zote katika Jina La Yesu.

Nyamazisha damu yoyote iliyomwagwa inayonena mabaya kwa ajiliya maisha yako:
Nanyamazisha damu zote zinazonena mabaya juu yangu katika Jina la Yesu, Nanyamazisha damu ya mbuzi na damu zote za wanyama kwa Damu ya Mwanakondoo. Ninaamuru damu yoyote inayonena mabaya juu yangu inyameze Kwa Damu ya Yesu Kristo. Imeandikwa Damu ya Yesu inanena mema nami kwa Damu hiyo ninanyamazisha kila damu za mashetani na damu ya Yesu inene mema kuanzia sasa.

UFUFUO NA UZIMA {THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH}
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM.




Saturday, September 8, 2012

EVERY SIN, MISTAKE or FAULT YOU SEE IN SOMEONE IS ALREADY IN YOU!


When you see a brother or sister in fornication or adultery, just begin to see yourself. You are seeing another version of yourself. You may ask, “Pastor, how is this possible?” The answer is in the Scripture: “buT ConsIdeResT noT the beam that is in thine own eye?” Matt7:3

Jesus warned us to consider our own faults before commenting on the faults of others. In order to help us further, He gave a blanket suggestion: “Judge not!” In other words, say nothing about anything! This is one of the commonest problems of Christians. How we love to criticize people, how we love to see the mistakes in our friends!

“To consider” means “to think deeply, analyze, to meditate, to ponder and to reflect”. When you reflect deeply on the issue you will realize that you are also guilty.

TESTIMONIES: “The Thief Threw My Handbag Back!!!”

Be encouraged and inspired in your faith as you read this testimony of an Emmanuel TV viewer who was privileged to receive an Anointing Sticker from a friend who had visited The SCOAN.
 “Emmanuel!!! My names are Lydia Cheembe from Zambia and I am writing in to testify about the goodness of God. God is so good and faithful to His children! I received Anointing Water and an Anointing Sticker from a friend of mine who had visited The SCOAN. I was so happy as I used to watch Emmanuel TV all the time and knew how God was using these simple items. I put the Anointing Sticker on my car.

“So, one day last week as I was driving into town from my building site, I left the window of my vehicle open. While the vehicle had stopped due to traffic, a thief suddenly stretched through the open window, snatched away my handbag and ran away with it! I had 25,000,000 Zambian Kwacha, which is equivalent to about $5000 in my handbag.

“Immediately, I took hold of the Anointing Sticker and prayed with it, “God of Prophet TB Joshua, help me!” God is so good!! To my greatest surprise, immediately the thief ran back to my vehicle, threw the handbag back into the vehicle and sprinted away! I got the bag and counted the money. He did not take anything! Praise God! I am very happy and I thank God for this testimony. May God continue to bless Senior Prophet T.B. Joshua. Emmanuel!! What God has done for me through the Anointing Sticker is too much. God is so faithful. May God bless you!”

Lydia Cheembe, Zambia

Source: http://distanceisnotabarrier.wordpress.com/2012/09/08/the-thief-threw-my-handbag-back/

Friday, September 7, 2012

Why Did God Created Devil? Pastor Chris Oyakhilome Answer It:

The quick vote question of the week is: “Why did God create the devil?” Is their a personality known as the devil? If there is, was it God who created it? Why? That’s the question.

Answer: First and foremost, Jesus let us know that there is a personality known as the devil. The whole Bible teaches that there is a personality known as the devil and gives us the history of the devil. The Bible lets us know that the devil was a person that was created; he was created, but he was not always a devil; he became a devil. I want to read something to you from the Bible that will help you understand these facts. I will start with what Jesus said in St. John’s gospel chapter 8; they engaged in an argument, and He said these words “Ye are of your father the devil, and the lusts of your father ye will do. He was a murderer from the beginning, and abode not in the truth, because there is no truth in him. When he speaketh a lie, he speaketh of his own: for he is a liar, and the father of it.” [John 8:44] [Pastor Chris emphasizes] “Ye are of your father the devil, and the lusts of your father ye will do. He was a murderer from the beginning” From the beginning? What beginning is Jesus talking about when He says “from the beginning;” does that mean from the beginning when he was created? No, Jesus used the expression “the beginning” in two different references: the first reference we will find has to do with the creation; the second reference has to do with when He began His ministry. He had told His disciples “Ye have been with me from the beginning,” [John 15:27] the beginning of His ministry. Those are the two references that Jesus used the term ‘beginning,’ and I want to give you one or two scriptures in reference to that St Mark’s gospel chapter 10 from verse 4, “And they said, Moses suffered to write a bill of divorcement, and to put her away. [Talking about divorce with Jesus] And Jesus answered and said unto them, For the hardness of your heart he wrote you this precept. But from the beginning of the creation, God made them male and female.” [Mark 10:4-6] From the beginning of the creation, God made them male and female? That means the beginning of creation He’s talking about there is not the creation of everything but the creation of man. When God created man, He made them male and female; that’s what He is talking about. So you can see the same reference in Matthew 19:4,8 – same expression – and then in 1 John 3:8, “He that committeth sin is of the devil; for the devil sinneth from the beginning. For this purpose the Son of God was manifested, that he might destroy the works of the devil.” The devil sinneth from the beginning; what beginning? John is still referring to this beginning that Jesus was talking about, not Satan’s own beginning. Remember the scriptures never contradict themselves, so Satan from his beginning was not in sin, from his beginning was not a murderer as Jesus said. Jesus said he was a murderer from the beginning; that beginning is the beginning of man’s creation.

Now, we look at Satan and how he begins and what happened to him. We go over to the book of Ezekiel chapter 28 from verse 12, “Son of man, take up a lamentation upon the king of Tyrus, and say unto him, Thus saith the Lord GOD; Thou sealest up the sum, full of wisdom, and perfect in beauty. Thou hast been in Eden the garden of God;…” [Ezekiel 28:12-13]. Now, that already gives us a clue that that King Tyrus that it’s talking about is not just an ordinary man; He’s dealing with a spirit personality that was present in the garden of Eden and the Bible does mention three personalities as far as the garden of Eden is concerned: one is Adam, the other Eve and the other one was the one that came in the body of a serpent, and that’s the devil. He had been in Eden, and then it says here “…Thou sealest up the sum, full of wisdom, and perfect in beauty. [that’s the latter part of verse 12, now verse 13] Thou hast been in Eden the garden of God; every precious stone was thy covering, the sardius, topaz, and the diamond, the beryl, the onyx, and the jasper, the sapphire, the emerald, and the carbuncle, and gold: the workmanship of thy tabrets and of thy pipes was prepared in thee in the day that thou wast created.” [Ezekiel 28:12-13]. “In the day that thou was created,” so he was created,…there was a definite time that this being was created. Verse 14 gives us another light here; it says “Thou art the anointed cherub that covereth; and I have set thee so: thou wast upon the holy mountain of God; thou hast walked up and down in the midst of the stones of fire.” [Ezekiel 28:14]. That’s very significant. To be anointed means that God sets you apart for the power that goes with it; He gives you the ability to make divine decisions. That’s very significant; it means you can make divine choices. You can make choices for God, [and] you can decide you are going to do this in His name and get about doing it; that’s very powerful, [because] it’s not every angel that is anointed, but this angel was anointed.

Mark that because of where we are going after verse 15, “Thou wast perfect in thy ways from the day that thou wast created, till iniquity was found in thee.” [Ezekiel 28:15] That’s very powerful; he was perfect in his ways from the day he was created until the day that iniquity was found in him. Verse 16,“By the multitude of thy merchandise they have filled the midst of thee with violence, and thou hast sinned: therefore I will cast thee as profane out of the mountain of God: and I will destroy thee, O covering cherub, from the midst of the stones of fire. Thine heart was lifted up because of thy beauty, thou hast corrupted thy wisdom by reason of thy brightness: I will cast thee to the ground, I will lay thee before kings, that they may behold thee.” [Ezekiel 28:16-17] Do you see that verse 17, “Thine heart was lifted up because of thy beauty, thou hast corrupted thy wisdom by reason of thy brightness?” He was carried away because of his beauty. Carried away with his beauty, he had so esteemed himself. Yes, the Bible does tell us that he was extremely beautiful, because God had made him so, but he wasn’t supposed to become proud and have his heart lifted. Praise God! Here is where his problem began, but let’s see Isaiah chapter 14 from verse 12 “How art thou fallen from heaven, O Lucifer, son of the morning! how art thou cut down to the ground, which didst weaken the nations! For thou hast said in thine heart, I will ascend into heaven, I will exalt my throne above the stars of God: I will sit also upon the mount of the congregation, in the sides of the north: I will ascend above the heights of the clouds; I will be like the most High. Yet thou shalt be brought down to hell, to the sides of the pit.” [Isaiah 14:12-15] I will be like the most High; I will ascend into heaven; this was where the iniquity was found in him.

Sin was found in him – pride – and the pride resulted in this self exaltation. He decided he would ascend to heaven and take the place of God. He chose to do this; why? Wasn’t he supposed to only do what he was supposed to do? Oh, yes, but you see, because he was anointed, he could make decisions unlike other angels. Now, you say, “How do you know that no other angel could make the same decision today?” Well, no other angel is going to do that, because we are not told about others that are anointed. He was anointed, he was God’s highest angel, and he corrupted his wisdom, corrupted it with pride, so there is where the devil came from. He was not always a devil; did you notice what his name was – Lucifer, son of the morning? A beautiful being; that’s how God made him, and he was cast down when he tried to ascend up. He was cast down when he wanted to go up and war against God and that’s the way where he became an adversary to God and all of God’s works. But, God also has determined when his punishment will be. Remember, there were others who fell with him; there were angels that he deceived that went along with him and one time Jesus was casting out devils and the devils cried out to Jesus, “Have you come to destroy us before the time? We know who you are; you are the Holy One of God.”[Matthew 8:29] They knew Jesus, and they said “Have you come to destroy us before the time?” They know that there is a set time for their destruction, and the Bible talks about it; if you study the book of Revelations, it talks about it.

Satan’s going to end up in the Lake of Fire [Revelation 20]. First, he will be imprisoned at the bottomless pit, and he will be there for 1,000 years and after the 1,000 years have ended, the bibles says an angel will go and bring him out of there and then he will be cast into the Lake of Fire; that will be his end. Praise God!

So, you said “why did God create the devil?” The devil was not created by God as a devil, but he became a devil. God created Lucifer, son of the morning, and he became a devil. Just like you, you were born as a nice innocent kid and then when you were growing up you decided to tell lies; where did that come from? You started stealing; where did that come from? You became insultive to other people; where did that come from? That little thing that everybody was happy about when you were born, looking so innocent; you hadn’t done anything wrong; where did all the wrongs that you did come from? Somehow, they came from the heart. Why? Because Satan had sown that in man and man had fallen; that’s why every man needs redemption; every man needs salvation; every man has to come out of sin. Everyone has to accept that which Christ has consummated for us – salvation. Praise God!

Source: http://www.pastorchrisonline.org/topicalblog/qatranscripts/2012/06/22/episode-11-quick-vote-question-on-gods-purpose-for-creating-satan/

TRUE CHRISTIANITY LIES IN THE PURITY OF THE HEART


Christianity, although practiced by man on earth, is not a physical exercise. It is a spiritual affair in which the Christian communes in faith with the Lord and Saviour, Jesus Christ. This means that true Christianity lies in the heart, in the purity of heart. It is not a matter of prayer, fasting and waving hands in worship without a thorough reformation of heart and life. The Holy Spirit wants to take up residence within you to aid you in developing a holy character – one in whom God can dwell. Allow God, through His Word, by His Spirit, to replace all darkness within with a gentle light, to replace the night with the day, to replace all bitterness within with the sweetness of His grace. For the happiness of seeing God is promised to those and those only who are pure in heart (Psalm 24:3-5).