GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Sunday, November 25, 2012

UWEZA MUNGU WETU

Na Mchungaji: MWANGASA (RP)





Danieli 3:1-30; 6:10-;  tumesoma habari mbili ambazo zinawahusu kwa ukaribu watu wane yaani, Danieli, Meshaki, Shedraka na Abednego.  Kipindi kile Babeli walivamia Yerusalemu na kuwachukua waisraeli utumwani, na kati yao wakachukuliwa watu kadhaa kwenda kufanya kazi za mfalme, baadhi ya waliokuwepo ni hawa wane. Kupitia hao tunapata kujifunza:-





Habari ya Kwanza kuhusu Sanamu iliyowekwa na Mfalme Nebkadneza: (Danieli 3:1-30):

Mtoto akitoa ushuhuda baada ya Maombezi
Mfalme Nebkadneza baada ya kuvamia wayaudi na kuwachukua utumwani, akatenga siku na kuwalazimisha watu wote waiabudu sanamu aliyoitengeneza. Lakini Shedraka, Mashaki na Abednego hawakukubali kuinama kuiabudu sanamu. Ndipo baadhi ya Wakaldayo wakapeleka mashtaka, tunaona hili katika mstari wa 8* “Basi baadhi ya Wakaldayo wakakaribia, wakaleta mashitaka juu ya Wayahudi.” Hawa ndio waliopeleka mashtaka kwa Mfalme. Mfalme akakasirika akasema, moto na uongezwe mara saba. Kibiblia mara saba ni namba ya ukamilifu wa Mungu, ukianzia kwa habari ya ukuta wa Yeriko ulianguka siku ya saba hivyo, hawa wakina shedraki hawakushtuka kwasababu walijua ukamilifu wa utukufu wa Mungu umekaribia.

Jambo la ajabu likatokea pale mfalme alipowatupa kwenye moto, maana moto uliwalamba na kuwateketeza wale walioenda kuwatupa. Lakini wao hawakuungua, moto haukuwaweza kabisa.  Lakini jambo la muhimu kujifunza kupitia habari hii. Pata picha ya hali iliyokuwepo kwa hawa watu watatu, maana lilikuwa ni jambo gumu kwao. Wangetarajia Mungu awaokoe mapema yaani Mungu asingeruhusu watupwe kwenye moto.  

Kwanza; Mungu alitaka atimize neon lake alilonena kupitia nabii Isaya KWAMBA “Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.” Isaya 43:2, Mungu wetu ni moto ulao, na kwakulithibitisha hilo akaruhusu hadi wafikie dakika ya mwisho, ili ajichukulie utukufu wake.


Pili; Mungu huwa anaokoa dakika ya mwisho, pale unapohisi kuwa huna msaada mwingine ndipo Mungu anajichukulia utukufu; watu wengi wanakata tama mapema bila kujua kuwa Mungu huokoa katika saa ambayo hukuitarajia, Wakina Shedraka wangetarajia Mungu awaokoe katika hatua ya kwanza, lakini Mungu alikuja kwao dakika ya mwisho.

Tatu; tunaona watu walioenda kuwashtaki kwa Mfalme; hapa tunajifunza kuwa unapoishi kuna watu watasema, kuna watu watakupinga, kuna watu watakushtaki kwa waganga wa kienyeji wakitaka kukuangamiza. Lakini ni muhimu kujua kuwa Mungu wetu ni Mungu wa kuokoa. Unapookoka Mungu anakuwa pamoja na wewe.

Nne; ndani ya moto kulikuwa na mtu wane; Yesu Kristo yupo pamoja nasi, imeandikwa, “wa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu;” 1 Yohana 5:4, hakuna moto ambao umeanzishwa na wanadamu, utakaoweza kukushinda. Sisi tumezaliwa na Mungu, na lazima tuushinde ulimwengu. Ni kweli unaweza kuwa unapitia kunye tatizo ambalo limekuwa moto kwenye maisha yako, lakini jambo la muhimu kujua kwamba, Hakuna moto uliofanywa na wanadamu utakaoweza kukushinda, kwasababu maana baada ya kuokoka unakuwa umezaliwa na Mungu.


Habari ya pili kuhusu, Danieli na Mfalme Dario: (Danieli 6:10-28):

Katika kipindi cha Mfalme Dario, watu kadhaa wakaamua kwa hila kumuangamiza Danieli, na hawakuona jambo lolote la kumuangamiza isipokuwa kwa habari ya Mungu wake. Imeandikwa, “Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba.” Hivyo, Mfalme akaweka muhuri kwenye sharia, lakini Danieli bila kujua ile sharia yeye akaendelea na Ibada kama kawaida; wakati huohuo, liliandaliwa ntanuru la samba ambao nao hawakupewa chakula kwa muda wa siku saba. Lakini cha ajabu kuwa walipomtupa ndani ya shimo wale samba hawakuweza kumdhuru. Ndipo mfalme akaamuru wale waliopangia hila watupwe wao. Ambapo samba waliwadaka hewani kabla ya kufika chini. Katika habari hii kuna mambop kadhaa ya kujifunza:-

Kwanza; Simba wakagoma kumla Danieli; biblia inasema, “Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika wake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto.” Waebrania 1:7.  Mungu anasema hutufanya sisi watumishi wake kuwa miale ya moto, n wale samba walimuona danieli kama mwali wa moto hivyo hawakuweza kumrarua. Unapookoka unakuwa mwali wa moto katika ulimwengu wa roho na hakuna silaha inayoweza kukudhuru.

Pili; Danieli alikuwa mtu wa kabila la Yuda na kwaabari ya Yuda kuna Simba wa kabila la Yuda, samba wasingeweza kumdhuru, kwa kuwa Danieli alikuwa pamoja na Mungu aliye simba wa kabila la Yuda. Hakuna haja ya kuogopa yale magumu unayopitia,. Kwa kuwa ndani yako kuna simba wa kabila la Yuda yaani Yesu Kristo. Pamoja na kukosa chakula kwa muda wa siku saba, hawakuweza kumla Danieli mtu wa Mungu.

Tatu; baada ya Mfalme kugundua kuwa samba wameshindwa kumuua Danieli, ndipo akaamuru wale waliotaka kumuua Danieli kwa hila waingize wao shimoni. Likatimia andiko kuwa, “Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake;  Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.” Mhubiri 10:8, wale waliokuandalia kifo au aibu kwa hila, itamrudia mwenyewe. Mungu huwaondoa wenye haki kwenye ajali na kuwaweka waovu badala yake.  Wanakupiga vita kwa hila usiangaike we mwangalie Mungu, yeye atakupigania.

Unapokuwa unaomba, inabidi ujue kuwa upo na Mungu awezaye kutenda kwa namna ya ajabu sana; Yoshua 10:9 “Bwana naye akawatapanya mbele ya Israeli, naye Israeli akawaua uuaji ulio mkuu hapo Gibeoni, akawafukuza waikimbilie hiyo njia ya kukwelea kwenda Bethhoroni, na kuwapiga hata kufikilia Azeka, tena hata kufikilia Makeda. Kisha ikawa, hapo walipokuwa wakimbia mbele ya Israeli, hapo walipokuwa katika kutelemkia Bethhoroni, ndipo Bwana alipowatupia mawe makubwa kutoka mbinguni juu yao hata kufikilia Azeka, nao wakafa; hao waliokufa kwa kuuawa na hayo mawe ya barafu walikuwa ni wengi kuliko hao waliouawa na wana wa Israeli kwa upanga.” Mungu aliwahi kuwaangushia mawe, maadui wa Israeli, Unatakiwa ujue BWANA amewatia adui zako mikononi mwako uwatende unavyotaka. Unatakiwa ujue hauko peke yako Mungu yupo kwaajili yako, kukuokoa. Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa na njia za kutoka mautini zina yeye!!!



Glory Of Christ (T) Church
Ufufuo na Uzima
Dar es Salaam, Tanzania.

Sunday, November 18, 2012

UJUMBE: MIAKA YA MAISHA YETU ( MESSAGE: THE YEARS OF OUR LIVES)


Na. Mch. Mwangasa (Resident Pastor)


Mchungaji Mwangasa (Resident Pastor) akihubiri kanisani
Ufufuo na Uzima, Dar es Salaam
Mwanzo 47:7-12
9* “Yakobo akamjibu Farao, Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni mia na thelathini; siku za miaka ya maisha yangu zimekuwa chache, tena za taabu, wala hazikufikilia siku za miaka ya maisha ya baba zangu katika siku za kusafiri kwao.” Haya yalikuwa ni mazungumzo baina ya Yakobo na Farao baada ya Yusufu kwenda kumtambulisha babaye kwa Farao. Lakini kitu cha kushangaza Farao akamuuliza Yakobo, siku za maisha yako ni ngapi? Na hilo ndilo lilikuw jibu ya Yakobo kwa Farao.

Jibu la Yakobo linatupa jambo muhimu la kujifunza, ukifuatilia maisha ya Yakobo utagundua kuwa ni kweli yalikuwa ya kusafiri sana, ukianzia tangu alipozaliwa, baadaye alimkimbia Essau na kwenda kwa Labani, haikutosha akarudi kupatana na Essau, bado taarifa za mauaji ya Yusufu nayo yalichangia kufanya maisha yake yawe ya tabu. Na ndio maana alipoulizwa na Yusufu siku za maisha yake ni ngapi, ikabidi atenge muda aliosafiri yeye na maisha yaliokuwa wameishi wazee wake yaani (Ibrahimu na Isaka).

Tukitaka kufuatilia maisha ya Yakobo alipokuwa kwa Labani, tunaweza kufahamu kupitia andiko hili Mwanzo  31:38-41, haya ni maelezo ya Yakobo kwa Labani, baada ya Labani kumpekuwa kutokana na upotevu wa miungu yake. Ndio maana hapo Yakobo anasema alikuwa anafanya kazi mchana na usiku, alibadilishiwa mishahara mara kumi kwasababu kila hasara ililopatikana ilirudishwa kwa Yukobo. (Mwanzo 30:25-44) pamoja na yote hayo, bado Labani alimdhulumu Yakobo, hivyo maisha ya Yakobo yalikuwa yamejaa tabu na dhulumiwa.

Mch. Bihagaze akimkaribisha Mch. Mwangasa
madhabahuni

Wakati Labani akiwa amevuruga makubaliano yale, Yakobo akamtazama Mungu, na hapa ndipo tunaona jambo la ajabu pale Yakobo alipoweka fito kwenye maji, na wale wanyama walipokunywa wakapata mimba. Hapa tunajifunza jambo kuwa hata kama wanadamu wamekudhulumu, Mungu anaweza kukusaidia nawe utaneemeka kuliko waliokudhulumu. Hili jambo lilitokea wakati Labani ametorosha madume yote ili Yakobo asipate uzao kwa wanyama wale. Ukiokoka unakuwa na Mungu, hakuna haja ya kusikitika kuwa umebaki peke yako, kuna Mungu ambaye hawezi kukuacha.

Maelfu ya Watu wakimwabudu Mungu Jumapili hii Ufufuo na Uzima

Imeandikwa Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.” Yohana 5:4. Ukiokoka Mungu anakuwa pamoja na wewe, yaani umezaliwa na Mungu, na kila kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu. Na hapa kwa Habari ya Yakobo, Mungu alikuwa anataka ile ahadi aliyomuahidi Ibrahimu itimie kwa Yakobo.


Inawezekana kwenye maisha yako, unaishi kama Yakobo, maisha yaliyojaa kusafiri ena huku ukipapasa papasa bila kujua unakoelekea. Inabidi ujue jambo hili kuwa ukimpata Mungu unakuwa umepata jibu la maisha yako. Imeandikwa, Utajiri na heshima ziko kwangu,  Naam, utajiri udumuo, na haki pia.” Mithali 8:18. Mtafute Mungu ndipo utakutana na Utajiri na Heshima. Wewe ndio unajua siku za miaka yako ni mingapi, unajua mambo gani magumu unayopitia, lakini Mungu anakuuliza siku za maisha yako ni ngapi.

Hata katika habari ya mwana mpotevu, aliposemezana na baba yake kuhusu maisha aliyopitia, alirudishiwa yote (Luka 15:17-23). Leo mwambie Mungu miaka ya maisha yako. Mungu anasema “Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.” Isaya 43:26. Kuna haja ya kuhojiana na Mungu, usiwambie watu mwambie Mungu. Yesu akamwambia Yule mwanamke kwenye kisima, kuwa yeye ndio maji yaliyo hai, kama unakiu ya jambo lolote mwambie Yesu Kristo (Yohana 4:14). Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa na njia za kutoka mautini zina yeye!!!!!


shukrani za pekee kwa Frank Minja , Mpiga picha.
The Glory Of Christ Tanzania Church
Ufufuo na Uzima
Dar es Salaam
Tanzania

Translation::


MESSAGE: THE YEARS OF OUR LIVES

By Ps Mwangasa (Resident Pastor)


Genesis 47: 7-12
Verse 9 “And Jacob said unto Pharaoh, The days of the years of my pilgrimage are an hundred and thirty years: few and evil have the days of the years of my life been, and have not attained unto the days of the years of the life of my fathers in the days of their pilgrimage.”

The above verse in an excerpt from the conversation that Jacob had with Pharaoh after Joseph had introduced his father to Pharaoh. The amazing thing to note is when Pharaoh inquired of Jacob “how old art thou?”, the verse above was Jacob’s reply to Pharaoh.

Jacob’s reply teaches us an important thing, if you follow up on Jacob’s life you will discover that verily it was one of many-a-pilgrimage from birth, later in life he fled to Laban from Esau, as if that was not enough he then journeyed again to reconcile with Esau, and on top of everything else the news of Joseph’s apparent death weighed heavily also in making his life sorrowful. That is why when Joseph was asked his age, it was necessary for him to differentiate his hard life from that which was better lived out by his ancestors (Abraham and Isaac).


In reading up on Genesis 31:38-41, we can follow up on the life of Jacob whilst he was with Laban; the passage describes the relation between Jacob and Laban after Laban had searched him out for his missing idols. That is why Jacob complained that he worked day and night; had his wage changed ten times and furthermore, had the cost of every ill that occurred passed onto him (Genesis 30:25-44.) Despite all of this, Laban oppressed Jacob and therefore Jacob’s life was filled with hardship and mistreatment.



In spite of Laban’s constant breaching of their agreements, Jacob beheld God and it is here that we see the wonders of God when Jacob put rods in the water that caused the animals to mate and conceive when they went for a drink. Here we learn that even though men have oppressed you, God can help you such that you will even prosper more than those who oppressed you. This feat took place when Laban took back all the male flocks so that Jacob would not get the offspring of those animals. In getting saved you unite with God and there is no need for you to despair over loneliness, for there is God who will never forsake you.



It is written For whatsoever is born of God overcometh the world: and this is the victory that overcometh the world, even our faith” John 5:4. When you get saved God unites with you, meaning that you are born of God and everything that is born of God overcomes the world. God wanted that which was promised to Abraham to be fulfilled in Jacob.


It could be that your life’s story is like that of Jacob’s, a life filled with pilgrimage and wondering without a sense of direction. The imperative thing to know here is that, in having God you have the answers for your life. It is written “Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness.” Proverbs 8:18. Seek after God and from thence shall you meet with riches and honor (righteousness). You know your age and the hardships you have gone through but God still wants to know of the days of your life.


In the passage of the prodigal son, even he after speaking with his father about his past had everything restored unto him (Luke 15:17-23). Today, tell God of the years of your life. God says Put me in remembrance: let us plead together: declare thou, that thou mayest be justified.” Isaiah 43:26. There is need for us to converse with God, do not discuss with man but instead with God. Jesus told the woman at the well that He is the living water and be there anything that you are thirsty for, tell Jesus Christ (John 4:14). Our God is a God who saves and the path of deliverance from death has He!


Glory of Christ Tanzania Church




Sunday, November 11, 2012

UJUMBE: WAKATI WA BWANA


Na Mch. Mwangasa (Resident Pastor) 11/11/2012

Mch. Mwangasa (Resident Pastor)
Akifundisha Neno la Mungu
WAKATI KWA KILA JAMBO:


Mhubiri 3:1-8 “kila jambo kuna majira yake…” Mhubiri 9:11 “Nikarudi na kuona, chini ya jua, si wenye mbio washindao katika michezo… … lakini wakati na bahati huwapata wote”. Biblia inataja kwa kila jambo linalotokea lina majira yake; hakuna jambo linalotokea kama sio wakati wake kutokea. Kwa bahati mbaya sana, wanadamu tunaishi kwa kufuata majira na si majira kuwafuata watu, yaani hatuwezi hatuna jinsi ya kubadili majira, lakini kuna jinsi ya kuishi katika majira tofauti. Watu wengi wamekata tama kwasababu ya kutokujua majira na wakati katika maisha yao.


Platform Team wakimwabudu Mungu
leo wakati wa kusifu na kuabudu


Mhubiri 7:14 “siku ya kufanikiwa hufurahi, na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambasamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asiweze kufahamu jambo lolote litakalofuata baada yake.” Maana ya maneno haya ni kwamba duniani Mungu ameweka mambo mazuri na mabaya pamoja; yaani kuna wakati wa mambo mabaya na saa ya mambo mema. Kwasababu hiyo, watu wameshindwa kujua litakalo fuata mbeleni. Na Mungu amefanya hivi makusudi ili watu wamtafute na kumwomba yeye peke yake.



Tokea siku uliyookoka Mungu  ndiye anayeshughulikia maisha yeko. Na ndio maana unahitaji kujua baada ya kuokoka thamani yako ni kubwa sana; unatakiwa ujue kuwa Mungu anayekushughulikia ndiye muumbaji wa mbingu na nchi; naye ameweka majira na wakati kwa kila jambo.


Wakati wa Kusifu na Kuabudu: UFUFUO NA UZIMA
MAMBO YA KUFANYA KIPINDI UNASUBIRI WAKATI BWANA:


Ukisoma kwa habari ya Hana:

(Angalia.. 1Samweli 1:1-…)  Hana alikaa muda mrefu bila kupata mtoto lakini jambo la muhimu ambalo alifanya ni kwamba, akawa anaenda kuomba huko shilo kila mara. Kumbe pamoja kuwa tunapitia katika wakati mgumu ni muhimu kuomba, watu wengi wameshindwa kupokea na hata kutokujua wakati wao kwasababu wamekuwa hawaombi, wakati wapo katika magumu. Haijalishi, tatizo limechukua muda gani, kwasababu hata tatizo la Hana lilichukua muda mrefu lakini aliendelea kuomba. Ndipo biblia inasema katika mstari wa  20” “ikawa wakati ulipowadia,Hana akachukua mimba akamzaa mtoto mwanaume” kumbe mtoto wa Hana *Samweli, alikuwa anasubiri wakati wake ufike. Tatizo halikuwa kwa Hana, bali wakati ulikuwa bado haujafika. Jambo la kujifunza hapa ni kuwa, wakati Hana anasumbuka kwa kukosa mtoto, alitumia muda ule kuomba. Hili ni jambo la muhimu sana kipindi unasubiri ahadi yako.


Mungu alikuwa ameruhusu Hana apite katika shida ile ili aandike Historia. Wakati mwingine Mungu anaweza kuruhusu upitie wakati mgumu ili utengeneze historia nyingine kwenye maisha yako. Hivyo ni muhimu kujua muda ule unaosubiri muujiza wako unatakiwa ufanye nini. Kama Hana angekatatamaa, Samweli asingekuja leo na hata kama angekuja ingekuwa si kwa kusudi la mwanzo. Subiri wakati wa BWANA, hakuna haja ya kukata tamaa wala kuvunjika moyo.




Kwenye Biblia tunaweza kuona maisha ya Yusufu:

Tunajifunza maisha ya Yusufu ambaye aliota ndoto (angalia Mwanzo 37:5), kuwa mkuu kuliko ndugu zake; ingawa alipitia kipindi kigumu sana, ambacho kama asingesimama na BWANA angekuwa ameshakata tamaa. Yusufu alijua kuwa Mungu ni Mungu wa wakati na majira katika kila jambo. Jambo la kujifunza kwa Yusufu ni kuwa hakutenda dhambi, hata ilipobidi kwenda gerezani kwaajili ya kukwepa dhambi. Kumbe ni muhimu kujilinda na dhambi wakati unamngojea BWANA. (angalia Mwanzo 37-48). Siku zote mawazo ya Mungu sio ya wanadamu, na ndio maana Yusufu aliwaambia ndugu zake kuwa ninyi mliniwazia mabaya lakini Mungu aliniwazia mema.kumbe jambo linguine la kufanya wakati unasubiri ahadi yako kwa Mungu ni kutokutenda dhambi.



Pia tunaweza kujifunza kuhusu jambo hili kupitia Nabii Danieli:

Danieli 9:1-3; Danieli baada ya kusoma kitabu cha tarehe, akafahamu kuwa ulikuwa wakati wa wana wa Israeli kutoka utumwani. Kumbe kuna umuhimu wa kusoma wakati na majira, hata mkulima mzuri ni yule anayejua kusoma majira na wakati. Ndipo Danieli akachukua hatua ya kufunga na kuomba ili kumwomba Mungu watoke utumwani. Jambo la ajabu analokutana nalo ambalo ni kikwazo kingine ni Mkuu wa anga la Uajemi, (angalia Danieli 10:1- … ). Kumbe inawezekana wakati wako ukafika lakini kuna mkuu wa anga (shetani) ambaye amekaa kuzuia. Kuna watu wanapitia wakati mgumu na wa kukatisha tamaa na kumbe kuna mkuu wa anga anayezuiua. Jambo la kufanya ni kupambana na mkuu wa anga hapo lazima wakati wako udhihirike.



Inawezekana umedumu kwenye tatizo kwa muda mrefu sana, umefika hata hali ya kukata tamaa lakini ni muhimu kujua kuwa kila jambo lina wakati wake. BWANA akiamua kutenda kwako, hakuna wa kuzuia kusudi la BWANA.  Unapookoka unatangaza wakati wa BWANA kwenye maisha yako, huu ndio wakati wa BWANA. Hata Yusufu alipita kwenye nyakati tofauti na ngumu lakini wakati wa BWANA ulipotimu aliyaona aliyoahidiwa. Huu ndio wakati wa BWANA kwako na unatakiwa uutangaze katika ulimwengu wa roho. Huwezi kumiliki bila kupigana na mkuu wa anga azuiaye, na kutangaza wakati wa BWANA. Hata Yesu wakati ulipofika alitangaza wakati wa BWANA duniani, tangaza wakati wako katika Jina la YESU. Huu ni wakati wako katika Jina la Yesu.



Translation:


MESSAGE: THE TIMING OF THE LORD

With Ps. Mwangasa (Resident Pastor) 11/11/2012

THERE IS A TIME FOR EVERYTHING:

Ecclesiastes 3:1 To everything there is a season…” [Read Ecclesiastes 3:1-8].
Ecclesiastes 9:11I returned, and saw under the sun, that the race is not to the swift…but time and chance happeneth to them all.”
The Bible tells us that to everything there is a season and that nothing comes to pass outside of its appointed time. Unfortunately though for mankind, we live in step with the seasons, and not the seasons occurring in step with us. There is no means available to mankind to alter the seasons but what there is, is a way in which man can live to cope through the different seasons. Many people have given up because they are unaware of the times and seasons of their lives.

Ecclesiastes 7:14In the day of prosperity be joyful, but in the day of adversity consider: God also hath set the one over against the other, to the end that man should find nothing after him.”
These words demonstrate that in the world God has put both prosperity and adversity, indicating that there is a time for adversity and a time for prosperity. God has allowed this on purpose so that man, in not knowing which lies ahead will entreat Him only.


From the day of your salvation God began to concern Himself with your life. Therefore it is imperative for you to know that from salvation you are of great value and that the God who concerns Himself over you is the creator of the heavens and the earth and He has appointed times and seasons for everything.

WHAT TO DO WHILE WAITING FOR THE TIME OF THE LORD:

In reading up on Hannah:

 (Refer to 1 Samuel 1, from verse one onwards)
Hannah was barren and without child for many years but the notable thing she did was that she ensured to go for prayer at Shiloh at its every appointed time. Despite the hardship that we go through we see here the importance of consistent prayer, many people have not been able to receive and be made aware of what kind of season they are in because they do not pray, her time came about in the midst of her hardship. The duration of the problem does not matter because even Hannah was barren for a long time but she continued in prayer. That is why the Bible says in verse twenty “Wherefore it came to pass, when the time was come about after Hannah had conceived, that she bare a son…” Hannah’s son, Samuel was awaiting his right time to come.
As such the problem was not with Hannah, but rather that her time had not yet come. What we can learn from Hannah is that despite her grief over her barrenness she utilised her time well in prayer. This is a very important thing to do while awaiting your promise.

God allowed Hanna to pass through that problem so that she would make history. Sometimes God can allow for you to endure hardship so that you can attribute a different history to your life. Therefore it is important to know what to do while you are waiting for your miracle from the LORD. If Hannah had given up, Samuel would not have been born and even if he was later born it would have been out of line with God’s original purpose. Wait for the time appointed by the LORD, there is no need to give up or have a broken heart.

From the Bible we can also get an analysis of Joseph’s life:

We can learn from the life of Joseph who dreamt that he was head over his brothers (refer to Genesis 37:5) that despite the hard times that he endured; if he had not held fast unto the LORD he would have given up. Joseph knew that God is a God of times and seasons and that there is a time for everything. What we can learn from Joseph is that he did not sin, and for his refusal to sin he even ended up being imprisoned.  Hear we learn the importance of keeping yourself from sin while awaiting the LORD (refer to Genesis 37 – 48). The thoughts of God are never as those of man, and that is why Joseph told his brothers that even though they had purposed evil toward him God purposed good. So in effect you must ensure not to commit sin while awaiting your promise from the LORD.


Furthermore, we can instruct ourselves about this matter via the Prophet Daniel:

Daniel 9: 1-3
After reading from prophetic records Daniel became aware that it was time for the restoration of Jerusalem. So here we see the great importance in investigating on times and seasons, a good farmer is he who knows how to understand the seasons. It was then that Daniel went forward with fasting and prayer that God should restore Jerusalem. An amazing thing to note of here is the contending of the Prince of Persia (read Daniel chapter ten from verse one). We see that it could be that your time has come but the Prince of the Air (Satan) has positioned himself in opposition. There are people who go through hard and discouraging times but behind it all is the Prince of the Air who is opposing. What needs to be done is warfare against the Prince of the Air and surely then, your time will manifest.


It could be that you have enduring the same problem for a very long time, and you are even at the point of giving up but assuredly that there is a time for everything. When the LORD has purposed to perform something toward you, no amount of opposition can prevent the fulfilment of the purpose of the LORD. When you got saved it was your declaration that it from then it is the LORD’s time in your life, this is the LORD’s time. Even Joseph went through different seasons and hard times but when the time of the LORD came about he saw all that he had been promised. This is the time that the LORD has purposed for you therefore ensure to declare so in the spiritual realm. You cannot dominate without battling against the Prince of the Air who opposes, and to declaring that it is the time of the LORD. Even Jesus when He arrived He declared that it was the time of the LORD on the earth, declare your time in the Name of Jesus. This is your time in the Name of Jesus!



GLORY OF CHRIST (T) CHURCH

UFUFUO NA UZIMA

DAR ES SALAAM

TANZANIA.

Monday, November 5, 2012

UJUMBE: NEEMA YA MUNGU {MESSAGE: THE GRACE OF GOD}

Sunday Sermon's notes with English Translation!!!

   
Na. Mch. Mwangasa {Resident Pastor}      4.11.2012 


TAFSIRI YA NEEMA YA MUNGU KIBIBLIA:

THE BIBLICAL INTERPRETATION OF THE GRACE OF GOD:



Tito 2:11 “maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa…” Waefeso 2:1-10. Kuna tafsiri nyingi sana ya neema ya Mungu; lakini tafsiri ya karibu zaidi inasema neema ni upendeleo wa Mungu kwa mwanadamu ambao hatukuungaramia, tafsri nyingine inasema neema ni daraja kati ya Mungu na wanadamu. Tafsiri nyingine ya neema ya Mungu kwetu ni njia ya Mungu kumfikia mwanadamu kwa njia ya Kristo Yesu.



Titus 2:11 “For the grace of God that bringeth salvation hath appeared to all men…”

Ephesians 2: 1-10

There are many interpretations of the grace of God; but the most accurate states that grace is God’s unmerited favor toward man. Grace has also been interpreted as the bridge between God and man. Another interpretation of God’s grace for us is that it is the path that God takes to get to man, through Christ.



Hata kwenye agano la Kale kulikuwa na tafsiri ya neema mfano utakaposoma katika kitabu cha Mwanzo 6:8  “lakini Nuhu akapata neema machoni pa BWANA”. Kimsingi, ulimwengu wa kipindi kile uliokolewa kwasababu ya neema ambayo Nuhu aliipata kwa BWANA. Pia ukisoma katika kitabu cha Yona 4:2; Kwa Tafsiri ya Yona neema ilikuwa ni tabia ya Mungu KWAMBA Mungu ni mwenye rehema na huruma yaani ni kawaida ya Mungu.



Even in the Old Testament we can find a mention of grace, for example when you read Genesis chapter six verse eight (Genesis 6:8)But Noah found grace in the eyes of the LORD.” Principally, those who were saved at that time were saved on account of the grace that Noah had received from the LORD. Furthermore, if you read in the book of John chapter four verse two (John 4:2), John’s definition of grace is that it is the character of God; His compassion and mercy are part and parcel of His nature.



Ukiangalia katika agano jipya tunapata tafsiri nyingine ya neema; Yohana 1:7; kabla ya Kristo upendeleo wa mtu kwa Mungu ulikuwa unapatikana baada ya mtu kutenda matendo mema; lakini Yohana anataja neema kama upendeleo unaokuja bila kugharimia. Kimsingi; ingawa wanadamu walikuwa wametenda dhambi lakini pamoja na dhambi za wanadamu Mungu akaja kumwokoa Mungu, ndio maana katika  Warumi 3:24, Paulo anaeleza kuwa tumepokea ukombozi wa Mungu  bila kugharimia.



Further sifting through the New Testament uncovers another definition of grace, John 1:7. Prior to Christ appearing, an individual’s benevolence and outward righteousness was the only way in which one could obtain the favor of God. But John mentions grace as being unmerited favor. So in effect even though man has sinned, despite this sinful state God came to save man and that is why in Romans 3:24 Paul says that we have received salvation freely.



TUMEOKOLEWA NA NEEMA YA MUNGU:

WE ARE SAVED BY THE GRACE OF GOD:



Kama utapata nafasi ya Kufuatilia Maisha yako utagundua kuna wakati ulipita mahali kwasababu ya neema ya Mungu. Tumepata neema bure.  Unapokuwa umeokoka unakuwa umepokea neema ya Kristo iliyo ya bure; ndio maana hata kama unapitia katika hali ngumu lakini ni muhimu kujua kuna neema ya Mungu iliyo kuu ambayo ni zaidi ya matatizo au magonjwa unayopitia. Hii ndio maana ya lile andiko katika Tito 2:11 “maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa…” Neema ya Mungu yatutosha.



In taking time to reminisce upon your life, you will discover that there were times that it was only by the grace of God that you managed to make it through. Grace has freely been bestowed upon us. In that you are saved, it is that you have received this free grace of Christ; that is why even if you are enduring great hardship it is important to know that there exists the grand grace of God which is greater the problems or sickness that you are enduring. This is what is meant in Titus 2:11For the grace of God that bringeth salvation hath appeared to all men…” God’s grace is all sufficient.



Hakuna haja ya kuangalia watu wanakuita nani kwasababu hata kipindi cha Yusufu watu walimwona mfungwa mbakaji lakini Neema ya Mungu ilimwita kuwa ni waziri mkuu wa Misri. Ingawa alipitia kwenye wakati mgumu lakini bado neema ya Mungu ilimwita waziri Mkuu. Unapoona hayo ni muhimu kutenga muda wa kumshukuru Mungu kila siku, unapoliona jua linawaka yupo anayesababisha liwake mshukuru Mungu kwa neema yake.



There is no need for you to be concerned with the name-calling being people hurled at you because even in Joseph’s days, people labeled him prisoner and rapist but it was the grace of God that instead called him Prime Minister of Egypt. Despite the hardships he endured, the grace of God still called him Prime Minister. In beholding this it thus becomes important to put aside time to for thanksgiving every day; for us just to see the sun rise is enough reason to give thanks to God for His grace.



NEEMA YA WOKOVU:

GRACE OF SALVATION:



Hii ni neema iliyondani ya watu waliompokea Yesu Kristo. Wakati wengine wakipitia matatizo wanaenda kwa waganga wa dunia hii sisi tuliompokea Yesu Kristo tuna neno la ushindi (kwa kupigwa kwake sisi tumepona Isaya 53:5). Unapokuwa umeokoka yaani umempokea Yesu Mungu anakufanya uwe mtoto wake hivyo anakuwa anataka kila unachokitenda kiwe nembo ya utukufu wake.



This is the grace which is within those who have received Christ Jesus. While the people of this world consult with sorcerer’s and witches for their hardships, we who have received Jesus Christ have the words of victory: by His stripes, we are healed (Isaiah 53:5). When you are saved (when you have received Jesus) God makes you His child and as such he desires for His glory to be displayed in all that you do.



Kumbe ukiokoka unakuwa umepokea neema ya Mungu lakini hatuwezi kutenda dhambi kwasababu kuna neema. Neema inatuagiza kuishi maisha matakatifu. Mungu hachanganywi na dhambi. Inawezekana unapitia katika hali ngumu kimaisha lakini jambo la kujua ni kuwa neema ya Mungu yakutosha. Tuna neema ya Mungu sisi tuliompokea Yesu Kristo kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yetu.



In effect when you are saved you have received the grace of God, but because there is grace we must not use it as an excuse for committing sin. Grace commands us to live a holy life. God does not mix with sin. It could be that you are going through a hard time in life but it is imperative to know that God’s grace is sufficient. For those of us who have received Jesus as LORD and Savior of our lives, we have the grace of God.
THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH

KAWE, DAR ES SALAAM,
TANZANIA.