GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Sunday, October 28, 2012

UJUMBE: MKARIBISHE YESU KWENYE CHOMBO CHAKO (MESSAGE: INVITE JESUS INTO YOUR VESSEL)

Sunday Sermon with English Translation


Na Mch.: Mwangasa (Resident Pastor)
Maelfu wakisifu na kuabudu katika ibada ya leo (28 0ct.)

Multitudes during today’s services’ praise and worship(28th Oct.)
Mathayo 14:22-33, Yesu alikuwa akiendelea kutenda kazi alizokuja kuzifanya duniani na ukisoma kuanzia Mathayo 14:1-… Utaona aliwalisha watu elfu tano (waume). Na wakati watu wakitaamaki akawalazimisha wanafunzi wake kupanda chomboni ili wavuke bahari. Wanafunzi wake walipokuwa katikati ya bahari ndipo ilipotokea upepo mkali na kuanza kusukasuka chombo. Tuna mmbo mengi ya kujifunza kupitia maandiko haya:-


In the passage of Matthew 14:22-33, we see that Jesus was one who busied Himself with the mission that was bestowed upon Him to accomplish here on earth. In reading from Matthew 14:1, you will see that He fed five thousand people (this figure accounting only for the men that were present). Thereafter, Jesus constrained His disciples to enter into a ship that they should cross over the sea. While His disciples were along this journey though, their ship was tossed about with the waves as a strong wind was upon the sea. There are many things that we can learn from this passage:

HALI YA WANAFUNZI KATIKA CHOMBO: 
(THE DISCIPLES STATE OF AFFAIRS IN THE SHIP):
Ukitafakari kwa makini utaweza kuona hali ya wanafunzi chomboni; inawezekana walishaanza kumlaumu Yesu, au kumlaumu kwa kuwalazimisha kupanda chomboni na yeye asiwemo.

If you were to contemplate, you would begin to come to terms with the disciple’s state of affairs in the ship; it is quite possible in fact that they had began to grumble against Jesus, or grumble against His order for them to enter into the ship without Him accompanying them.
Pia, wanafunzi wa Yesu walikuwa wamekata tama, kwasababu tukio hili lilipotokea mwanzo walikuwa na Yesu chomboni akaukemea upepo lakini mara hii Yesu hakuwepo chomboni. kwa maana hiyo wanafunzi walikuwa katika hofu kuu.


Furthermore, the disciples of Jesus had given up as in a previous sea storm, Jesus was onboard the ship with them. This time round, they were not with Him and as such they were even more petrified and in great distress.

Biblia inasema hata wanafunzi walipomuona Yesu akitembea juu ya maji, wakahisi ni kivuli chake. hapa tunajifunza kuwa kuna wakati kwenye maisha unaweza kuwa unapita kwenye hatua ngumu kimaisha, na kwasababu ya hofu ukajikuta unaiogopa njia ambayo ndio ufumbuzi wa tatizo lako.


The Bible says that when the disciples saw Jesus walking on the water they perceived that it was a spirit. Hear we learn that there are times in life that one may find him or herself enduring a tough season and on account of fear, one will be afraid of a particular appearance or occurrence that will in fact be for their breakthrough.

KWANINI YESU ALITEMBEA JUU YA MAJI:

(WHY DID JESUS WALK ON THE WATER?):

Yawezekana umejiuliza kwanini Yesu alikuja huku akiwa juu ya maji; Kimsingi bahari ndio ambayo ilikuwa tatizo kwa wanafunzi wake, kwahivyo Yesu alikanyaga bahari kuonyesha kuwa  lile tatizo lilikuwa chini ya miguu ya Yesu. Kumbe Yesu yupo juu ya tatizo linalokuzunguka maana lipo chini ya miguu yake.


It could be that you have asked yourself, why did Jesus walk on the water? Principally, the tumultuous sea was the disciple’s key problem, as such Jesus walked on the water to demonstrate that that problem was under His feet. Of a truth, Jesus is above the problem that surrounds you, in other words, your problems are under His feet.

Na ndio maana Petro naye alijaribu kupita juu ya tatizo yaani bahari lakini alipoiangalia bahari alipata hofu. HAPA tunajifunza jambo kwamba hatakiwi kuliangalia tatizo bali mwangalie Yesu ambaye yupo juu ya tatizo.


That is why; Peter attempted to walk on his problem (i.e. the sea) but unfortunately became fearful when he displaced his focus to looking upon the boisterous elements. Here we learn that our focus should not be on our problems but rather on Christ alone who is on top of the problem.

Ukimwamini Yesu unavuka kutoka mautini unaingia uzimani, na Yesu ana mamlaka na funguo za mauti na kuzimu. Hivyo ukiwa kwenye tatizo, usiangalie tatizo bali mwangalie Yesu. unapoelekea kwa Yesu usipepese macho, mtazame Yesu aliyekufa msalabani kwaajili yako.   


If you believe in Jesus you will cross over from death to life; moreover, Jesus has the authority and keys of hell and of death. Therefore when you are in a predicament, do not look upon it but rather fix your focus upon the LORD. In moving toward Him do not shift your gaze, only behold Jesus Christ who died on the cross for you.

 
JAMBO LA KUFANYA UKIWA NDANI YA TATIZO:

(WHAT TO DO WHEN YOU ARE IN A PREDICAMENT):

Katikati ya bahari wanafunzi wakamuona Yesu kama tumaini lao, na ndipo Petro alipoamua kumfuata. kimsingi uamuzi wa Petro kumfuata Yesu kwa kutembea juu ya maji ni sahihi kabisa, ila tatizo ni kwamba petro alitumia uzoefu wake wa bahari ambao ukamfanya asiwaze sauti ya Yesu aliyemuita. watu wengi wameshindwa kutoka ndani ya tatizo kwasababu ya taarifa walizozisikia kutoka kwa watu.


In the midst of the raging seas the disciples saw Jesus as their defense and put their trust in Him, as such Peter was determined to go after Him. Peter’s decision to get to Jesus by walking on the water was a sound one indeed; but the problem was that he relied upon his familiarity of the seas which caused him to disregard the voice of the LORD who had called him. Many people have been unable to break out from their predicament because of what they have been told by others.

Mfano; Mtu ana tatizo la ndoa na ndio limeanza, lakini baada ya kuongea na mtu mwengine mwenye tatizo kama hilo, anamwambia kuwa amedumu kwenye tatizo hilo kwa miaka mingi. Taarifa hiyo moja tu inamfanya huyu ambaye tatizo la ndoa ndio limeanza, akate tamaa na kuingiwa na hofu  kabisa kwa kuhisi naye atadumu kwa miaka hiyo yote.


For example:  a certain newlywed has a marital problem, but after sharing this issue with another person who has a similar problem, the newlywed is told that he or she is rooted therein for the next good couple of years. This single opinion alone is highly likely to cause the newlywed to lose heart and be filled with fear, believing that he or she is stuck for good.

Ni muhimu kujua hakuna haja ya kuangalia tatizo wala watu wengine waliopo kwenye tatizo. tunatakiwa tumuangalie Yesu Kristo ambaye aweza kukutoa kwenye tatizo ulilonalo. unapomwita Yesu kwenye mwili wako uliojaa magonjwa atakapofika yeye yote yatakoma, ukimwita Yesu kwenye ndoa yako yenye matatizo atakapofika tatizo litakama.


It is important to know that there is no need to behold the predicament at hand, neither to look upon others who are also in the same boat. What is needful is for us to look upon Jesus Christ who is able to save from the predicament that one may be facing. When you call the LORD to your sickly body that is filled with disease, when He arrives all issues will cease. When you call the LORD to attend your marital problems, when He arrives the issue will cease.

Isaya 41:9-10 “wewe niikushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa; usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwamaana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.”  Kama ukijua jambo ambalo Mungu anataka utend kwenye tatizo utalibadili tatizo hilo na kuwa daraja la kukuvusha na kukupeleka kwenye hatma njema ya maisha yako.


Isaiah 41:9-10:
“Thou whom I have taken from the ends of the earth, and called thee from the chief men thereof, and said unto thee, Thou art my servant; I have chosen thee, and not cast thee away. Fear thou not; for I am with thee: be not dismayed; for I am thy God: I will strengthen thee; yea, I will help thee; yea, I will uphold thee with the right hand of my righteousness.”
If you knew what it was that God has intended to perform toward you in the midst of your predicament, you would give it a substitute title of bridge instead of problem; and it will be the kind of bridge that would take you up and over and toward your life’s pleasant destiny.

Maombi :

Prayer:

Baba Mungu katika Jina la Yesu Kristo leo nimetambua kuwa ninatakiwa nitakiwa nikutazame wewe ninapokuwa kwenye tatizo. ninaomba msamaha kwasababu ya kutazama mambo mengine badala kukutazama wewe Mungu, Mungu naomba unisamehe katika Jina la Yesu.


Father God in the Name of Jesus Christ, today I have discovered that I am to behold you whenever I find myself in any kind of situation. I ask you to forgive me because I have fixed my focus on many other things instead of you oh God, I ask you to forgive me in the Name of Jesus.


 
Katika Jina la Yesu nimeamua kukuita wewe leo, imeandikwa katika Yeremia 3:33 “niite, nami nitakuitikia, name nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.” Leo ninakuita katika Jina la Yesu. Mungu kutoka katika kiti chako cha enzi ninakuita katika Jina la Yesu. Ninakutumaini wewe Mungu katika Jina la Yesu. Natakanivuke na wewe Mungu hadi ng’ambo ya maisha yangu katika Jina la Yesu.


In the Name of Jesus, I have decided to call upon you today, it is written in Jeremiah 33:3, “call unto me, and I will answer thee, and shew thee great and mighty things, which thou knowest not.” Today I call upon you in the Name of Jesus. Oh God, before your throne I call upon the Name of Jesus. I trust in you oh God in the Name of Jesus. I want to cross over with you unto the other side of my life in the name of Jesus.


*picha zote zimechukuliwa katika ibada ya leo*

*All the pictures were taken during today’s service*



MWITE YESU KWENYE TATIZO ULILONALO!!!

INVITE JESUS INTO YOUR SITUATION!!

UFUFUO NA UZIMA {THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH}
TANGANYIKA PACKERS,
Dar es Salaam, TANZANIA

Sunday, October 21, 2012

UJUMBE: MAJESHI YA BWANA {MESSAGE: SOLDIERS OF THE LORD }

Sunday's Sermon with English Translations:
Na Mch. Mwangasa (RP)

With Ps. Mwangasa (RP)

Mchungaji Mwangasa akihubiri neno la Uzima Jumapili hii.

Pastor Mwangasa preaching the word of life this past Sunday

Mwanzo 14:1-16; Kedorlaoma na wafalme wenzake walifanya vita na kufanikiwa kumteka Lutu ambaye alikuwa nduguye Ibrahimu; Mungu akamwambia Ibrahimu kuwa nduguye (Lutu) alikuwa amekamatwa na kutekwa, Ndipo Ibrahimu akaamua kwenda vitani dhidi ya wafalme wale ili kumwokoa nduguye. Baada ya vita akafanikiwa kumkomboa Lutu na kurudisha mali zote zilizokuwa zimeibiwa. Kumbe pamoja na Ibrahimu kuahidiwa Baraka lakini ilimlazimu kupigana vita.



Wachungaji (RP's) wakisikiliza Ibada.

Pastors (RP’s) listening to the sermon

Genesis 14:1-16; During their warfare, King Chedorlaomer and his allied kings took Lot, relative of Abraham captive. God ensured to inform Abraham that his relative (Lot) was captured and carried away, and thus Abraham duly set out to save his relative by launching an offensive against the kings. After his successful warfare, not only was Lot delivered, but all that was plundered was also restored.  We see here that even though Abraham had a promise of blessing, it was still necessary for him to make war.




Vivyo hivyo katika kitabu cha Waefeso 6:10-12; tunagundua kuwa sisi tuliokoka tunatakiwa kupigana vita, ingawa vita vyetu si vya mwilini bali vya rohoni. Kuna wakati unaweza kuona mambo yanaendelea katika ulimwengu wa mwili, na ukafikiri kuwa yanatokea tu lakini kimsingi katika ulimwengu wa roho kuna vita inayoendelea. Shetani alinyang’anywa mamlaka na funguo ya mauti na Yesu alilikabidhi kanisa zile funguo za mauti.

That is why, in the book of Ephesians chapter six, verses ten to twelve (Ephesians 6:10-12) we discover that for those of us who are saved, there is a necessity for us to engage in combat, and yet this warfare of ours is not carnal, but spiritual. There are times when you may deem of things pertaining to the natural life as just mere events but fundamentally in the spiritual realm there is a battle raging. Jesus stripped Satan of authority and snatched from him the keys of death and He bestowed unto the church those keys of death.
Sehemu ya Maelfu ya watu wakiabudu na kusifu katika ibada ya leo Ufufuo na Uzima

Multitudes banding together in praise and worship during today’s service at Resurrection and the Life

Kwa kujua kuwa hana uwezo na amenyang’anywa mamlaka, shetani anatumia wanadamu ili kutimiza lengo lake la kuwadhuru wanadamu. Kimsingi mtu alipuliziwa pumzi na Mungu kwasababu hiyo roho yake ina nguvu (superior) katika ulimwengu wa roho. Hivyo shetani anawatumia hao kutimiza lengo lake la kuwadhuru wanadamu wengine. Kwa hiyo mtu kuwa mchawi maana yake ni kutumiwa na shetani katika kudhuru wanadamu.


Knowing that he has no power and that he has been stripped of authority, Satan uses people in order to fulfill his mission of destroying people. God breathed into man the breath of life and thus his spirit is the superior in the spiritual realm. That is why Satan uses people to destroy people, executing his mission. In effect, a person who practices witchcraft is one who is being used by Satan in order to destroy others.



Hatutakiwi kuwaogopa wachawi kwasababu kama wao wanavyotumiwa na shetani ndivyo sisi tunavyotumiwa na Mungu; na habari nzuri ni kwamba Mungu wetu ni mkuu kuliko shetani. Kumbe kama vile Ibrahimu alipowafuatia Mfalme Kedorlaoma na wenzake na kurudisha vyote, na ndio maana kwa msaada wa Mungu Joshua alisimamisha Jua wakati wakipigana vita.
Platform Choir wakiongoza sifa na Kuabudu Ufufuo na Uzima.

The platform choir leading praise and worship at
The House of Resurrection and the Life


We are not supposed to fear witches because just as they are used by Satan, so we are used by God; and the good news is that our God is sovereign, even over Satan.
In the same way in which Abraham pursued King Cherdolaomer and his allied kings and restored all, Joshua also by the help of God subdued and stopped the sun whilst his battle was raging.



Huwezi kumiliki na kurudisha afya, biashara, kazi au mafanikio uliyonyang’anywa na shetani bila kupigana vita. Kimsingi huwezi kumiliki bila kupigana, shetani ni kama mfalme Kedorlaoma anaweza kuteka na kujimilikisha vile ambavyo Mungu ametuahidia kwa hivyo ili kumiliki ni lazima kufanya vita naye. Kama Mungu alivyomwagiza Ibrahimu kwenda vitani kupambana na waliomteka nduguye ndivyo Yesu ametupa mamlaka ya kupambana na shetani na kumshinda hatimaye kurudisha mali zote.


You cannot take dominion and restore your health, business, career or prosperity which has been plundered from you by Satan without making war. This is a principle, you cannot dominate without battling it out, Satan is like King Chedorlaomer and he can capture and dominate that which God has promised us. Therefore in order to dominate we must make war against him. Just as God commanded Abraham to go to war and contend against those who had taken his relative captive, Jesus has given us authority to contend against Satan and to eventually defeat him, restoring all that had been plundered.

Watu waliokubali kumpa Yesu maisha yao (kuokoka) katika ibada ya Leo
Ufufuo na Uzima

People who made a decision to give their lives to Jesus (get saved) during today’s service at Resurrection and the Life.

Maombi ya Vita:
Baba Katika Jina la Yesu Kristo, umesema lolote tutakalo muomba Mungu kwa Jina la Yesu tutapokea, leo ninasimama kupigana vita katika ulimwengu wa roho. Imeandikwa na alaaniwe azuiaye upanga wake usimwage damu leo ninatumia upanga ambao ni neon la Mungu kuwasambaratisha mapepo wachafu wote, jeshi la giza la wachawi na waganga wanaharibu maisha yangu nina wasambaratisha katika Jina la Yesu.


Father in the Name of Jesus Christ, you said that whatsoever we ask of you oh God in the Name of Jesus, we will receive, today I stand to make war in the spiritual realm. It is written, cursed be he that refrain’s his sword from shedding blood, today I exert the sword, which is the word of God to scatter every unclean spirit, dark forces of sorcerers and witches that are ruining my life, I scatter them in the Name of Jesus.

 

Imaandikwa kwasababu hii mwana wa Adamu alidhihirishwa ili azivunje kazi za ibilisi, leo ninavunja kazi za ibilisi kwenye maisha yangu katika Jina la Yesu. Leo ninawafuata na ninarudisha vyote walivyochukua kwangu Kwa damu ya Yesu Kristo. Afya yangu, mali zangu, nyota yangu na kila jambo walilolichukua kwangu ninarudisha katika Jina la Yesu Kristo.


It is written, for this reason did the son of man appear so that he should destroy the works of the devil, today I destroy the works of the devil over my life in the Name of Jesus. Today I pursue and recover all that was plundered from me by the blood of Jesus Christ. My health, my prosperity, my star and all else that was plunder from me I restore them all in the Name of Jesus.




Ninatangaza ushindi kwenye maisha yangu katika Jina la Yesu, ninatangaza kuwa mali zangu na Baraka zangu zimerudi na ninazifunika katika Jina la Yesu, leo nimeokoka kutoka kwenye mtego wa mwindaji katika Jina la Yesu.


I declare victory over my life in the Name of Jesus, I declare that my prosperity and blessings have been restored and I seal them in the Name of Jesus, today I am delivered from the hunter’s trap in the Name of Jesus.

IBADA KATIKA PICHA (Sunday's Surmon in Pictures):














(we are sorry for the wrong date on pictures;  They were all taken on 21st Oct. 2012)
UFUFUO NA UZIMA (THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH)
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM.

Monday, October 8, 2012

UJUMBE: NGUVU YA MSAMAHA


Na Mchungaji Yekonia Bihagaze (RP) Jumatatu 8.10.2012
UTANGULIZI:

Mwisho wa somo ili utagundua nguvu iliyopo nyuma ya kusamehe. Kuna watu wanapitia kwenye matatizo na magonjwa kwasababu ya kutokusamehe.

Mathayo 6:9-12 “basi ninyi salini hivi…12 msipowasamehe wengine makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu” Zaburi 103:3 Hapa tunaona kuwa kanuni ya Mungu ni kusamehe kwanza kabla ya kuponya. Na ndio maana waweza kumwona mtu anasema ameokoka lakini bado yupo kwenye ugonjwa kwasababu ya kutokusamehe.

KWANINI UMSAMEHE ALIYEKUKOSEA:

Kumsamehe mtu aliyekuumiza sio jambo la mzaha, na ndio maana kuna watu wanasema kuwa wamesamehe lakini ndani ya mioyo yao bado hajasamehe. Tunatakiwa kusamehe kwasababu kuna nguvu iliyopo nyuma ya mtu aliyekukwaza au kukuumiza.

Watu wengi wanashindwa kusamehe kwasababu hawajui nguvu iliyopo nyuma ya yule mtu aliyewakwaza. Emu tuangalie mfano wa gari; Gari linapomgonga mtu serikali haishtaki gari bali anayeshtakiwa ni dereva. Vivyohivyo ukiumizwa unatakiwa uangalie ile nguvu iliyopo nyuma ya aliyekuumiza. Kimsingi kuna nguvu inayotenda kazi nyuma ya aliyekuumiza na usipoijua hiyo nguvu utajikuta unashindwa kusamehe.

VITU VITATU AMBAVYO NI VIPIMO KAMA UMESAMEHE AU BADO HUJASAMEHE:

1. Ukimsamehe mtu utamwongelea vizuri:

Kama kweli umemsamehe mtu utamwongelea vizuri mbele za watu, kama unasema umemsamehe mtu alafu bado unamwongelea vibaya ujue bado hujasamehe kutoka moyoni mwako. Ukimkuta mtu anaongea mabaya kuhusu mtu aliyemkwaza basi ujue ndani ya moyo wake kuna madabahu ya makwazo na machungu. Na kwasababu hiyo kuna watu wamefukuzwa kazi, wamepigwa kwasababu ya kushindwa kuwanenea watu mazuri.

2. Ukimsamehe mtu utamwombea:

Ishara nyingine kuwa ya kuonyesha kuwa umesamehe ni kumwombea mwingine mazuri; na ndio maana Eliya alipotaka kujenga madhabahu ya Mungu alibomoa kwanza madhabahu ya baali, hata leo huwezi kujenga madhabahu ya Mungu ya amani kama bado moyoni unamadhabahu ya kutokusamehe. Watu wengi wamejikuta wakiomba mabaya kwa watu waliowakosea na kwa namna hiyo wanashindwa kupokea majibu ya matatizo yao.

3. Ukimsamehe mtu utawasiliana kwa uzuri:

Ukimsamehe mtu utawasiliana naye kwa uzuri, nah ii ni kwenye madhabahu ya moyo wako. Hata kama amekujibu vibaya wewe mjibu kwa uzuri. Ni kweli kuwa ukisamehe Yule mtu atakudharau lakini ni muhimu kujua kuwa tunasamehe si kwa ajili ya waliotukosea bali kwa ajili yetu.

Watu wengi wanashindwa kusamehe kwasababu ya kukosa nguvu ya uwezesho ya kuweza kusamehe. Kila mtu aliyeokoka anayo nguvu ya uwezesho ya kusamehe, nayo ni Roho Mtakatifu. Kila mtu aliyeokoka ana Roho Mtakatifu naye hutuwezesha kusamehe, kuokoka kunakupa nguvu ya uwezesho kusamehe. Bila kusamehe huwezi kupokea kutoka kwa BWANA.


MAOMBI YA KUSAMEHE:

Baba katika Jina la Yesu Kristo ninaomba nguvu ya msamaha wako; leo nimetambua kuna nguvu inayotenda kazi nyuma ya mtu aliyenikwanza, leo ninawasamehe wote walionikwaza katika Jina la Yesu. Ninatangaza msamaha, ninavunja madhabahu ya makwazo na kutokusamahe ndani yangu katika jina la Yesu Kristo.

Baba ninaomba uniponye na matatizo yaliyoingia ndani yangu kwasababu ya kutokusamehe katika Jina la Yesu. Leo ninabadilika katika Jina la Yesu. Mimi ni mzima na nimeponywa katika Jina la Yesu.

UFUFUO NA UZIMA (THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH)
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM.

Monday, September 24, 2012

UJUMBE: VIUMBE NA MAUMBILE HEWA.

Na Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima. Tarehe 17.6.2012

UTANGULIZI:-

Viumbe ni vilivyo umbwa , vyaweza kuwa wanadamu, vitu maji, anga na vitu vingine vyote, na Mumbile ni mtazamo au jinsi viumbe hivyo vinavyoonekana. Ni Muhimu kujua viumbe vya kiroho vinaweza kuvaa maumbile tofauti. Ndio maana Yesu alipofufuka, Mariam mama yake alimuona na kuhisi ni mtunza bustani utajuuliza kwanini mama yake hakumtambua kirahisi na wakati alikuwa naye muda wa kutosha, hii ni kwasababu Yesu alijibadili na kuwa kama mtunza bustani, na mariam akahisi ni mtunza bustani.

ROHO ZINAWEZA KUVAA MAUMBE : Kibiblia:-

Unaposoma kitabu cha mwanzo ni muhimu kujua kuwa kimeelezea kuhusu asili ya ulimwengu, mwanzo wa vitu vyote. Emu tuangalie kwa undani MWANZO 3:1-24.. HII NI HABARI YA Adamu na Hawa walipokula tunda, katika mstari wa 13 Hawa akasema "nyoka alinidanganya" lakini nyoka huyuhuyu ndio anaitwa shetani. Kumbe tangu kitabu cha mwanzo (asili) kinadhihirisha kuwa kuna uwezekano wa shetani (wa rohoni) kuvaa umbo la nyoka. Kama shetani angemtokea hawa kwa umbo lake la asili, asingefanikiwa kumdanganya hivyo ilimlazimu avae mwili. Sasa kumbe uwezekano wa kuvaa umbo upo.

Maandiko yanayoonyesha uwezekano huo:-
 • ZABURI 91:13 utajiuliza kwanini biblia inasema "utakanyaga nyoka au simba".. ukichambua kwa akili ya rohoni jambo hili; Utagundua kuwa Biblia inaonyesha uwezekano wa viumbe wa rohoni kuvaa miili.
 • LUKA 10:19 Biblia inaonyesha maumbo; kumbe unaweza kuona mtu anasema. "ugonjwa huu ulinianza nilipoumwa na mdudu" na ndio maana Mungu ametupa mamlaka ya kukanyaga nyoka na ng'e kwasababu  shetani aweza kuvaa maumbile ya hivyo vitu.
 • MARKO 16:18; Biblia inasema hata ukinywa kitu cha kufisha; yaani sumu kumbe shetani aweza kujibadili na kuwa sumu.
• ISAYA 27:1 Kumbe Biblia inaonyesha kuwa kunanyoka aliye baharini na ndio maana utaona kuna ajali zinatokea baharini, kumbe kuna shetani limejigeuza na kuwa joka baharini.

mara nyingi shetani hutenda kazi kwa kujibadilisha na kuwa kiumbe chochote ili kukuangusha, au kukufuatilia au kukutoa kwenye kusudi la Mungu. Ni muhimi kama mtu uliyeokoka kuwa makini na kujua kuwa shetani aweza kujibadili na kuwa umbo lolote ili akuteke.

SHETANI AWEZA KUJIBADILI MAUMBILE MBALIMBALI

Shetani anaweza kujibadili maumbile kwa ajili ya kutimiza azma yake aliyoikusudia, shetani akiamua kumteka mtu anaweza kutumia mtu, kitu, mti, gari au kitu chochote kutimiza azma yake. Na ndio maana Joshua alipokutana na mtu asiyemjua akamuuliza “je wewe ni wa upande wetu” Na mtu huyu alikuwa rohoni si mwilini tunaweza kuona katika kitabu cha JOSHUA 5:13-15, Joshua alijua kuwa kuna uwezekano wa shetani kujibdili katika maumbile mbalimbali. Ndio maana kwa watu walioko mikoa ya shinyanga wanajua kunavijiji wanavyoita Gamboshi, ni miji yenye watu lakini ya kichawi, yaani mapepo na mashetani wamejibadili na kuwa mji. Kumbe shetani aweza kujibadili.

KUTOKA 8:6-7 tunaona hapa kuwa Haruni alinyoosha fimbo na kutokea vyura, juu ya nchi ya Misri, na waganga wa misri wakafanya vilevile kuleta vyura juu ya nchi, utajiuliza kwanini hawa waganga waliweza kuleta vyura.. ni kwasababu shetani anaweza kujibadili kwenda kwenye maumbo mbalimbali.

UFUNUO 13:10. Yohana aliona katika ulimwengu wa roho, maumbo ya wanyama mbalimbali yote hii ni kudhihirisha kuwa shetani anaweza kujibadili, UFUNUO 13:6. shetani hapa ameonekana kama mnyama aliyetoka baharini, kimsingi yeye shetani ni roho lakini anaweza kuvaa maumbo mbalimbali ili kutenda kazi katika kutimiza azma yake. Ni muhimu kukataa na kuangamiza maumbo yote ambayo shetani anatumia ili kukushambulia. “deactivate them in The Name Of Jesus”

Na ndio maana ni rahisi mtu kukwambia, ugonjwa ulimwanza baada ya kupaliwa. kumbe shetani amegeuka na kuwa kitu cha kumpalia mtu ili kupitisha ugonjwa huo na kumfanya mtu ahisi kuwa kile kitu ndio kimesababisha. Hata kipindi cha Yesu walipokuwa wanavuka baharini na mashua ukaja upepo mkali na ukataka kuangusha kile chombo, lakini Yesu akaukemea na upepo ukatulia. Kimsingi Yule ni shetani alijibadili na kuwa upepo ili kuwazuia wasihubiri injili.

MIJI YA ROHONI.

UFUNUO 21:2 hapa tunaona kuwa Yohana aliona mji wa rohoni. Ufunuo 21:10 huu mji ambao Yohana aliona na haupo kwenye ulimwengu wa mwili na huwezi kuuona kimwili. Huu mji sio wa mwilini kwasababu Yohana akasema “ akanichukua katika roho” maana yake hakuwa katika ulimwengu wa mwili bali wa Rohoni. Na ndio maana hata shetani huiga “imitator” na kufanya miji duniani ili kuendesha shughuli zake. Ndio maana watu wengi wanaokufa katika mazingira ya kutatanisha “misukule” nao hupelekwa kwenye hiyo miji ya rohoni.

Hata kuzimu ni mji wa rohoni, ambao Yesu alipokufa alishuka kuzimu nakumlaani shetani, kuzimu ni mji wa rohoni.

USHINDI DHIDI YA VIUMBE HEWA.

1. Tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na ng’e na nguvu zote za Yule muovu, wala hakuna kitu kitakacho kudhuru kwa namna yoyote ile.

2. Pia twaweza kuwashinda viumbe wa rohoni kwa kunena kwa lugha mara kwa mara, ambapo unamruhusu Roho mtakatifu akupiganie, hivyo viumbe vya ajabu vitajikuta vinajitenga na wewe.

3. Maombi pia ni silaha Kubwa dhidi ya viumbe vya hewa. Maombi yanalazimisha viumbe hivi kuondoka mahali ambapo walianza kujijenga kwa muda mrefu. Maombi yanauwezo wa kuangamiza ngome.

4. Sisi ni rungu la Bwana ambaolo kwa sisi, Mungu hufyeka farasi na mpanda farasi(viumbe hewa) kumbe hakuna wakufyeka ila sisi tuliookoka.


kunauwezekano wa kuwepo mji kabisa katika ulimwengu war oho kwaajili ya uhalibifu. Kuleta uhalibifu.. katika ulimwengu waroho kuna miji lakini ya rohoni.

Mungu wetu ni Mungu Mtakatifu, wa upendo, hakuna kama yeye.. ni Mungu mkuu mno.. atufunuliaye mambo ya rohohoni maagumu tusiyo yajua.. na wala kuyawazia. MUNGU ANATUPENDA SANA.

Ufufuo na Uzima (The Glory Of Christ (T) Church)
Tanganyika Packers,
Kawe, Dar es Salaam.

Sunday, September 23, 2012

UJUMBE: NYOTA KIBIBLIA


Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima 23.9.2012



UTANGULIZI:

Huu ni mwendelezo wa somo la Nyota na Maisha mtu aliyonayo. Mathayo 2:1; Kama tulivyoona tangu mwanzo kuwa nyota ni kipawa, uweza, hatma au hali ya mtu ya baadaye. Tukaona nyota ya Yesu ilionekana kabla Yesu hajazaliwa na mamajusi wa mashariki walimwona kama Mfalme.



MAANANYOTA:

Kama tulivyooa sehemu ya kwanza kuwa nyota ni kiashiria cha rohoni, kinachoonesha mtu atakuwa nani baadaye, mafanikio ya mtu au hatma ya mtu. Viashiria hivi ndivyo vinavyoitwa nyota.



NYOTA KATIKA BIBLIA:

Hesabu 24:14-17 Baraki alikuwa mfalme, na alipoona kuwa wanaisrael wanakuja ili kushambulia ufalme wake, akamtafuta Balaam amtabirie. Hayo ni maneno ya Balaamu aliyoona, Hivyo Balaamu alipoangalia taifa la Israel akaona nyota, kimsingi nyota ya mtu inaonyesha jinsi mtu atakavyokuwa baadaye. Hivyo balaamu aliweza kumuona Yesu tangu mwanzo na ndio maana mamajusi wa mashariki nao pia walimwona Yesu kama nyota.



Nyota yaweza kuonyesha kusudi la maisha ya mtu, na ndio maana ingawa Suleimani alizaliwa na mke wa Huria ambaye Daudi alimuua mumewe ili ampate lakini kwasababu nyota ya kujenga hekalu ilikuwa juu yake (yaani Suleimani), Mungu alimchagua kujenga Hekalu. Daudi alikuwa na watoto wengine wengi, lakini aliyechaguliwa kujenga ni Suleimani kwasababu ndio mwenye nyota ya kujenga yaani tangu anazaliwa



Isaya 47:8-12; Hapa biblia inataja neno “wajuao Falaki”, hii ni elimu inayohusu mambo ya nyota ambayo wachawi husoma. Katika Mathayo 2:1- Biblia inataja mamajusi, wao ni wasomaji wa nyota ambao waliiona nyota ya Yesu kabla ya Yesu hajazaliwa. Nyota ya Yesu iliwafanya mamajusi kumfuata kutoka mbali, na wakati huohuo Herode alifadhaika. Kumbe nyota ya mtu ikionekana watu wanaweza kuifuata na kukuletea unalohitaji. Watu wengi wapo katika vifungo mbalimbali kwasababu nyota zao zimefunikwa.



MAMBO 15 AMBAYO UTAYAONA KAMA NYOTA YA MTU HAIPO:

·        Umahiri na utendaji kazi wa mtu hauonekani; kama mtu hana nyota ule umahiri wa wake na utendaji kazi hauwezi kuonekana. Hata ajitahidi kufanya kazi kwa bidii umahiri hawezi kuonekana.

·        Hawezi kuwa mbunifu katika maisha; nyota huleta ubunifu sasa kama haipo basi ubunifu wa mtu hautaonekana. Mtu huyo atakuwa anashindwa kubuni kitu cha kufanya ili kupata mafanikipo katika maisha.

·        Hawezi kufanya kazi zake kwa ufanisi; nyota huleta ufanisi katika kazi, mtu akikosa nyota basi ule ufanisi wake hauwezi kuonekana, mtu huyo atakosa ufanisi katika kazi zake.

·        Hukosa mvuto; nyota huleta mvuto hivyo mtu nyota yake haipo, anakuwa anakosa mvuto hata wa watu kuomuona tena.

·        Hukosa kibali; nyota humfanya mtu awe na kibali hivyo mtu anapochukua nyota, kimsingi anakuwa amechukua kibali chako.

·        Huwezi kusikilizwa katika jamii; kwasababu nyota huleta kusikilizwa, mtu akichukuliwa nyota hawezi kusikilizwa katika jamii.

·        Hawezi kuthubutu;

·        Anakosa uthubutu wa kutenda;

·        Anakosa ujasiri wa kusema; mtu akikosa nyota anakosa ujasiri wa kusema.

·        Anakosa uthubutu wa kutoa maamuzi magumu; mafanikio ya mtu ni matokeo ya maamuzi magumu aliyowahi kuyafanya.

·        Anakosa ujasiri wa kudai unachojua ni kweli;

·        Huwezi kutumia hata kile ulichonacho; ndio maana ya lile andiko utajenga nyumba na mtu mwingine atalala ndani yake”.

·        Anakuwa na matatizo;

·        Anakuwa na hofu ya kutenda mapenzi ya Mungu; nyota ikichukuliwa mtu aweza kuwa na hofu ya yajayo, yaliyopo au yaliyopita.

·        Kukosa uaminifu kwenye mambo ya Mungu.



Kwahiyo wachawi au waganga wanapochukua nyota yako kimsingi, mambo hayo yanakuwa hayapo kwenye maisha yako.



JINSI WACHAWI WANAVYOCHUKUA NYOTA NA MATUMIZI YAKE:

Utajiuliza ni wakina nani wenye uwezo wa kuiona nyota; biblia inathibitisha kuwa waganga na wachawi wana uwezo wa kuiona nyota na kuifuata. Na kama nyota haina ulinzi wa Mungu waganga wanaweza kuichukua nyota. Kuna watu wanadhania kuwa uchawi haupo na kutokujali uwepo wake, lakini uchawi upo kwasababu biblia imetaja kuwa uchawi upo.



Wanachuaje; kwasababu wachawi wanaweza kuiona nyota ya mtu na kuifuata, hivyo wakigundua kuwa nyota ni nzuri wanaweza kuichukua na kumuuzia mtu mwingine; na ndio maana mtu anaweza kuzaliwa nyota ya uongozi, ujasiri, upendeleo, ubunifu au kupata kibali mbele za watu, alafu ikachukuliwa na kupewa mtu mwingine. Na ndio maana kuna watu ni matajiri kwasababu ya nyota za watu; na wakati huohuo mtu Yule ambaye nyota yake oimechukuliwa anaanza kuwa na matatizo; kile kibali au upendeleo aliokuwa nao awali hawezi kuwa nao tena.



Mtu aliyechukuliwa nyota; anakuwa na mafanikio mwanzoni lakini ghafla yanabadilika baada ya kuchukuliwa nyota. Kimsingi; Mungu akikupa kutu huwa kinadumu lakini kama maisha ya mtu yanaashiriwa na nyota pale nyota inapochukuliwa mtu huyo upendeleo wake unaanza kuondoka. Rudisha nyota yako kwa Jina la Yesu.



Maombi ya kuamuru aliyechukua Nyota yako arudishe:

Baba katika Jina la Yesu leo nimetambua kuwa nina nyota, nayo yaweza kuchuliwa na kunitia katika matatizo; hivyo ninaamuru ila aliyechukua nyota yangu arudishe katika Jina la Yesu. NInapokonya nyota yangu iliyochukuliwa katika Jina la Yesu, naamuru mahali popote ilipowekwa na kutumika ninaamuru irudi kuanzia sasa katika Jina la Yesu.



Ninaamuru umahiri wangu, ufanisi, uwezo wangu wa kutenda na uwezo wa kuthubutu ninaurudisha katika Jina la Yesu. Ninaamuru kibali, afya, ujasiri na mvuto wangu urudi katika Jina la Yesu; nataka nyota yangu katika Jina la Yesu.

UFUFUO NA UZIMA {THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH}
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM.

Sunday, September 16, 2012

NYOTA YA MTU NA MAISHA ALIYONAYO

 
Na Mchungaji Josephat Gwajima  16.9.2012

Utangulizi:
Biblia imeeleza kuhusu nyota ya Yesu ilivyoonekana  kutoka mashariki,(Mathayo2:1); Hii inadhihirisha wazi kuwa kila mtu ana nyota yake. Hivyo katika mfulilizo wa somo hili tutaona maana ya nyota, kazi ya nyota, nyota yaweza kufunikwa kichawi, madhara ya kuishi bila nyota, dalili za kuchukuliwa nyota, nyota yaweza kurudishwa na namna ya kutambua nyota yako. Hapa hatuzungumzii kuhusu kusoma nyota au utabiri wa nyota bali tunaangalia nyota kama ilivyo katika Biblia.
MAANA YA NYOTA:
Nyota katika Biblia inawakilisha kipawa, hatma ya mtu, lengo lililomfanya Mungu akulete  hapa duniani na kusudi lako la maisha. Hivyo tunaposema nyota yako ipo au imechukuliwa maana yake hayo mambo yamechukuliwa au yapo. Kimsingi hakuna mtu asiye na maana tangu kuzaliwa kwake, kwasababu kila mtu aliye duniani amekuja kwa kusudi lake.
Kuna tofauti kati ya elimu na nyota; elimu sio nyota lakini elimu yaweza kunoa nyota. Na si kwamba kujifunza kunaleta nyota bali nyota ipo kwa wote lakini elimu inainoa nyota; na ndio maana ni rahisi kumwona mtu hana elimu lakini anamafanikio mahali fulani. Ukisoma Mhubiri 9:11 Biblia inasema wakati na bahati huwapata wote na sio swala la elimu au ujuzi tu.
KAZI YA NYOTA:
1.       Nyota humfanya mtu kuwa mahiri katika utendaji kazi wake. (Effectiveness)
2.       Nyota huleta ubunifu katika maisha ya kila siku (Creativity)
3.       Nyota inamfanya mtu anatenda kwa ufanisi (Efficiency)
4.       Nyota huleta mvuto kwa watu kutoka mbali ili kuleta vitu kwa ajili yako. (Attraction)
5.       Nyota humfanya mtu awe na maisha yenye mwelekeo na kibali mbele za watu. (Acceptance  and Favor)
6.       Nyota humfanya mtu kusikilizwa katika jamii.
Kuna vitu ambavyo mtu anaweza kuvipata kwasababu nyota yake imeonekana. Nyota yaweza kuvuta zawadi yaani vile vitu ambavyo hujavitaabikia, na ndio maana Yesu alipokuwa mdogo aliletewa zawadi na mamajusi wa mashariki. (Mathayo 2:11) kwahiyo nyota ikichukuliwa maana sahihi ni kwamba hayo mambo hapo juu yote hayapo.
Mathayo 2:1-2; Wakati Yesu anazaliwa kulikuwa na watu wanaitwa mamajusi, ambao walikuwa na uwezo wa kusoma nyota. Hivyo katika ulimwengu wa roho waweza kuona watawala wajao, maisha yajayo au yale yatarajiwayo.  Na ndio maana Mamajusi wa mashariki ya mbali waliweza kuifuata nyota ya Yesu.
Nyota inapoonekana inaweza kufuatwa, yaani watu waona zile kazi zake na kumfuata mtu. Kimsingi tunaposema mtu hana nyota maana yake umahiri, ufanisi na kibali vimechukuliwa. Lakini nyota ikionekana  maana yake haya mambo yote yamerudishwa na hapo utamwona mtu anafanikiwa hata kama elimu yake sio kubwa.
NYOTA ILIYOCHUKULIWA/ ILIYOFUNIKWA KICHAWI:
Nyota ikifunikwa au kuchukuliwa kichawi maana yake mvuto, umahiri, ufanisi na uwezo unakuwa umechukuliwa au umefunikwa. Na ndio maana kuna watu wanahangaika kuanzisha kampuni, kujenga nyumba, kulima, au kufanya biashara kama nyota imefunikwa au kuchukuliwa kichawi huwezi kupokea mafanikio ya sahihi kwenye maisha. Watu wengi wanahangaika kuonekana au kukubalika lakini kumbe tatizo lipo kwenye nyota yaani imefunikwa au imechukuliwa kichawi.
Wachawi wanaweza kuona nyota ya mtu na kuifunika ili isionekane; na kwa namna hii watu wengi wanaonekana hawana mafanikio katika maisha kumbe nyota zao zimefunikwa. Hivyo ni muhimu kupambana Kwa Jina la Yesu ili nyota yako ionekane.
MADHARA YA KUISHI BILA NYOTA YAKO:
  •   Kwa kuwa nyota ndiyo inamwezesha mtu kuwa na kila kitu, ndio kusudi la mtu, upendeleo wa mtu; hivyo madhara ya kutokuwa na nyota ni kutokuwa navyo vyote vile.
  •  Siku zote unakuwa unatenda chini ya kiwango (Under performance). Na kwa namna hiyo hakuna mtu anakubali kile unachotenda; yaani elimu na maarifa yote yakuwa chini ya kiwango.
  •  Utapata na kuibiwa; unapata kazi baadaye unaibiwa au unapata mchumba baadaye anaibiwa. Kimsingi huwezi kudumu na haya mambo.
  • Unapata lakini anatumia mtu mwingine.

DALILI ZA NYOTA ILIYOFUNIKWA:.
Ø  Maisha kukosa mwelekeo; mtu akikosa nyota hata kama akiwa na elimu kama nyota haipo lazima mtu huyo atakosa mwelekeo.
Ø  Kukwama kibiashara na kuishi maisha kwenye madeni.
Ø  Unafanya kazi lakini hupati maendeleo. Yaani mtu anapata mshahara mzuri lakini anakosa mafanikio halisi kwasababu ya nyota iliyofunikwa au kuibiwa.
Ø  Wewe ni kiongozi lakini jamii haikutambui.
Ø  Ukichangia hoja za mijadala mbalimbali hakuna anayekusikiliza.
Ø  Umesoma lakini hupati kazi, na ukipata kazi haiendani na elimu yako
Ø  Maisha ya upweke na hakuna anayekujali katika familia.
Ø  Unatenda kazi kwa bidii lakini hupandi cheo.
Ø  Kama ni binti  sifa zote lakini hakuna anayekuchumbia maana huonekani.
Ø  Kuandamwa na mabalaa na mikosi.
Ø  Kupotelewa na watu wa muhimu
NYOTA YAWEZA KURUDISHWA:
Hatua ya kwanza kama hujaokoka unatakiwa kuokoka; kuokoka ni kumpokea Yesu awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako ili upate uwezo wa kushindana, hivyo ukigundua nyota imechukiliwa unatakiwa umpokee Yesu ndani ya moyo wako. Ni kitu cha kushangaza kuhitaji msaada wa Yesu halafu yeye humtaki kimsingi kuokoka ni hatua ya kwanza ya kurudisha nyota.
Hatua ya pili ni kushindana kwa maombi; kama mtu anayetaka kurudisha nyota yake ni lazima achukue hatua  ya kushindana katika maombi. Hivyo baada ya kuokoka hatua inayofuata ni kushindana ili nyota irudi. Nyota yaweza kurudishwa kwa kuomba katika Jina la Yesu Kristo.

UTAJUAJE NYOTA YAKO NI IPI:
Usithubutu kwenda kwa mganga wa kienyeji au kusoma kwenye magazeti ili kujua nyota yako.  Ni muhimu kujua kilichoibiwa ni kipi katika maisha yako. Isaya 47:13Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na wasimame hao wajuao falaki, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata.FALAKI ni elimu juu ya mambo ya nyota; biblia inataja kuwa kuna watu wanaojishughulisha na usomaji wa nyota. Lakini kuna mambo kadhaa yanayoweza kukuonyesha nyota yako ni ipi:-
Moyo wako, akili zako na mawazo yako yanakuwa katika hilo jambo AMBALO NI NYOTA YAKO. Mfano kama nyota yako ni biashara basi utakuta moyo wako upo kwenye biashara, basi lazima nyota yako ni k biashara. Kama nyota ni kuimba au siasa lazima moyo utakupeleka kwenye kuimba na siasa. Hivyo tambua kuwa kwenye nyota yako ndipo kuna Baraka zako.
Jambo ambalo ni nyota yako utalitenda bila kupambana; Yaani hutatumia nguvu kwenye kulitekeleza jambo hilo.

MAOMBI YA KURUDISHA NYOTA:
Kurudisha nyota Iliyoibiwa:
Baba katika Jina la Yesu, nimetambua kuwa nyota yangu yaweza kufunikwa na kuibiwa; na leo ninaamua kuirudisha kwa Jina la Yesu kila nyota yangu iliyoibiwa, nyota ya kukubaliwa, ufanisi, umahiri, biashara, kazi au nyota ya hatma njema naamuru irudi kwa Jina la Yesu Kristo. Ninaamuru nyota yangu ikombolewe kwa damu ya Yesu, ninaamuru iachiliwe katika Jina la Yesu.



Kufunua nyota iliyofunikwa:
Katika Jina kuu la Yesu ninasafisha nyota yangu iliyofunikwa; nyota ya mafanikio ninaisafisha kwa Jina la Yesu. Katika torati kila kitu husafishwa kwa Damu nami natumia Damu ya Yesu kusafisha nyota yangu katika Jina la Yesu. Ninatakasa nyota yangu iliyochafuliwa katika Jina la Yesu.  Ninang’arisha nyota yangu katika Jina la Yesu.

Kuangamiza wasimamizi wa nyota:
Ninasimama kinyume na kila mashetani, wachawi na waganga wa kienyeji wanaoshikilia nyota yangu katika Jina la Yesu. Waliofunika nyota ninawaangamiza katika ulimwengu wa roho, ninateketeza wote walioiba nyota yangu kwa Jina la Yesu. Katika Jina la Yesu niharibu kazi na utawala wa mashetani wanaoiba nyota yangu katika Jina La Yesu.

Kukiri ushindi:                           
Ninatangaza kurudishwa kwa nyota yangu katika Jina la Yesu; ninatangaza maisha yangu kung’arishwa katika Jina la Yesu. Mafanikio yangu yamerudi katika Jina la Yesu. Nimeshinda  kwa damu ya Yesu.

UFUFUO NA UZIMA (THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH)
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DARES SALAAM.

Friday, September 14, 2012

UTOTO (KIFUNGO CHA UTOTO)

Na Pastor Adriano Makazi:

Unapo kuwa mtoto mdogo unakuwa huwezi kujitegemea kwa jambo lolote lile hadi usaidiwe na mzazi au mkubwa wako aliye kuzidi umri.

Utoto si udhaifu au ugonjwa bali ni hatua ambayo kila mtu ameipitia au anaipitia.

Mfano mzuri tunaona hata YESU mwenyewe alipo vaa mwili alivaa umbo la utoto hii ni kuonyesha kuwa ni lazima hatua hii kila mmoja wetu aipitie.


KUNA AINA TATU ZA UTOTO
1: Utoto wa kimwili. (mwilini)
2: Utoto wa kiroho. (rohoni)
3: Utoto wa akili. (nafsini)

Mtoto wa kimwili anakuwa hajui na hafahamu na hawezi mambo mengi yahusuyo mwili

Mtoto wa kiroho anakuwa hajui na hafahamu na hawezi mambo mengi yahusuyo roho

Mtoto wa akili anakuwa hajui na hafahamu na hawezi mambo mengi yahusuyo kutumia akili(mfano kufikiri, kuwaza, kutafakari, kuamua kwa usahihi n.k)

Kwa kuwa kila kitu kinaanzia kwenye hali ya utoto na kinakuwa taratibu hadi kufikia hali ya utu uzima ndio maana Mungu alituonyesha hili kupitia mwanawe Yesu,jinsi alivyo zaliwa na hadi akakuwa na hatimaye akaanza kazi katika utu uzima.

Watoto huwa wanapatikana kwa uchungu mwingi na maumivu makali,

Angalia jinsi mwanamke azaapo mtoto wake jinsi anavyo zaa kwa uchungu na maumivu makali.

Angalia jinsi Mungu alivyo tuzaa sisi kwa uchungu mwingi kwa kumtoa mwanawe wa pekee Yesu akafa kwa ajili yetu sisi.

Angalia jinsi Yesu alivyo tuzaa sisi kwa njia ya mateso mengi (kupigwa mijeredi,kutemewa mate,kipigiliwa misumari,kuvalishwa taji ya miiba,kufa msalabani,kuchomwa mkuki ubavuni.

Mtoto yeyote azaliwapo anazaliwa akiwa amebeba kusudi la Mungu ndani yake tangu tumboni mwa mamaye.

Mfano=Yesu,Yohana mbatizaji,Yeremiha,Samsoni,Gidioni,Yoshua,Musa n.k


KWA NINI MUNGU ANARUHUSU TUPITIE UTOTO?

  • Kwa sababu ni hatua ambayo kila mtu lazima aipitie ndipo awe mtu mzima baadaye.
  • Kwenye utoto ndio sehemu ya kujifunza mambo mengi na vitu vingi vya aina mbalimbali.
  • Kwenye utoto ndipo tuna jifunza unyenyekevu.
  • Kwenye utoto ndipo tunajifunza utii
Mungu anapo kuweka kwenye utoto anatazamia ujifunze mambo mengi ili uwe mtu ajuae vitu vingi baadaye na uweze kutumika vizuri na yeye.