GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Sunday, October 21, 2012

UJUMBE: MAJESHI YA BWANA {MESSAGE: SOLDIERS OF THE LORD }

Sunday's Sermon with English Translations:
Na Mch. Mwangasa (RP)

With Ps. Mwangasa (RP)

Mchungaji Mwangasa akihubiri neno la Uzima Jumapili hii.

Pastor Mwangasa preaching the word of life this past Sunday

Mwanzo 14:1-16; Kedorlaoma na wafalme wenzake walifanya vita na kufanikiwa kumteka Lutu ambaye alikuwa nduguye Ibrahimu; Mungu akamwambia Ibrahimu kuwa nduguye (Lutu) alikuwa amekamatwa na kutekwa, Ndipo Ibrahimu akaamua kwenda vitani dhidi ya wafalme wale ili kumwokoa nduguye. Baada ya vita akafanikiwa kumkomboa Lutu na kurudisha mali zote zilizokuwa zimeibiwa. Kumbe pamoja na Ibrahimu kuahidiwa Baraka lakini ilimlazimu kupigana vita.



Wachungaji (RP's) wakisikiliza Ibada.

Pastors (RP’s) listening to the sermon

Genesis 14:1-16; During their warfare, King Chedorlaomer and his allied kings took Lot, relative of Abraham captive. God ensured to inform Abraham that his relative (Lot) was captured and carried away, and thus Abraham duly set out to save his relative by launching an offensive against the kings. After his successful warfare, not only was Lot delivered, but all that was plundered was also restored.  We see here that even though Abraham had a promise of blessing, it was still necessary for him to make war.




Vivyo hivyo katika kitabu cha Waefeso 6:10-12; tunagundua kuwa sisi tuliokoka tunatakiwa kupigana vita, ingawa vita vyetu si vya mwilini bali vya rohoni. Kuna wakati unaweza kuona mambo yanaendelea katika ulimwengu wa mwili, na ukafikiri kuwa yanatokea tu lakini kimsingi katika ulimwengu wa roho kuna vita inayoendelea. Shetani alinyang’anywa mamlaka na funguo ya mauti na Yesu alilikabidhi kanisa zile funguo za mauti.

That is why, in the book of Ephesians chapter six, verses ten to twelve (Ephesians 6:10-12) we discover that for those of us who are saved, there is a necessity for us to engage in combat, and yet this warfare of ours is not carnal, but spiritual. There are times when you may deem of things pertaining to the natural life as just mere events but fundamentally in the spiritual realm there is a battle raging. Jesus stripped Satan of authority and snatched from him the keys of death and He bestowed unto the church those keys of death.
Sehemu ya Maelfu ya watu wakiabudu na kusifu katika ibada ya leo Ufufuo na Uzima

Multitudes banding together in praise and worship during today’s service at Resurrection and the Life

Kwa kujua kuwa hana uwezo na amenyang’anywa mamlaka, shetani anatumia wanadamu ili kutimiza lengo lake la kuwadhuru wanadamu. Kimsingi mtu alipuliziwa pumzi na Mungu kwasababu hiyo roho yake ina nguvu (superior) katika ulimwengu wa roho. Hivyo shetani anawatumia hao kutimiza lengo lake la kuwadhuru wanadamu wengine. Kwa hiyo mtu kuwa mchawi maana yake ni kutumiwa na shetani katika kudhuru wanadamu.


Knowing that he has no power and that he has been stripped of authority, Satan uses people in order to fulfill his mission of destroying people. God breathed into man the breath of life and thus his spirit is the superior in the spiritual realm. That is why Satan uses people to destroy people, executing his mission. In effect, a person who practices witchcraft is one who is being used by Satan in order to destroy others.



Hatutakiwi kuwaogopa wachawi kwasababu kama wao wanavyotumiwa na shetani ndivyo sisi tunavyotumiwa na Mungu; na habari nzuri ni kwamba Mungu wetu ni mkuu kuliko shetani. Kumbe kama vile Ibrahimu alipowafuatia Mfalme Kedorlaoma na wenzake na kurudisha vyote, na ndio maana kwa msaada wa Mungu Joshua alisimamisha Jua wakati wakipigana vita.
Platform Choir wakiongoza sifa na Kuabudu Ufufuo na Uzima.

The platform choir leading praise and worship at
The House of Resurrection and the Life


We are not supposed to fear witches because just as they are used by Satan, so we are used by God; and the good news is that our God is sovereign, even over Satan.
In the same way in which Abraham pursued King Cherdolaomer and his allied kings and restored all, Joshua also by the help of God subdued and stopped the sun whilst his battle was raging.



Huwezi kumiliki na kurudisha afya, biashara, kazi au mafanikio uliyonyang’anywa na shetani bila kupigana vita. Kimsingi huwezi kumiliki bila kupigana, shetani ni kama mfalme Kedorlaoma anaweza kuteka na kujimilikisha vile ambavyo Mungu ametuahidia kwa hivyo ili kumiliki ni lazima kufanya vita naye. Kama Mungu alivyomwagiza Ibrahimu kwenda vitani kupambana na waliomteka nduguye ndivyo Yesu ametupa mamlaka ya kupambana na shetani na kumshinda hatimaye kurudisha mali zote.


You cannot take dominion and restore your health, business, career or prosperity which has been plundered from you by Satan without making war. This is a principle, you cannot dominate without battling it out, Satan is like King Chedorlaomer and he can capture and dominate that which God has promised us. Therefore in order to dominate we must make war against him. Just as God commanded Abraham to go to war and contend against those who had taken his relative captive, Jesus has given us authority to contend against Satan and to eventually defeat him, restoring all that had been plundered.

Watu waliokubali kumpa Yesu maisha yao (kuokoka) katika ibada ya Leo
Ufufuo na Uzima

People who made a decision to give their lives to Jesus (get saved) during today’s service at Resurrection and the Life.

Maombi ya Vita:
Baba Katika Jina la Yesu Kristo, umesema lolote tutakalo muomba Mungu kwa Jina la Yesu tutapokea, leo ninasimama kupigana vita katika ulimwengu wa roho. Imeandikwa na alaaniwe azuiaye upanga wake usimwage damu leo ninatumia upanga ambao ni neon la Mungu kuwasambaratisha mapepo wachafu wote, jeshi la giza la wachawi na waganga wanaharibu maisha yangu nina wasambaratisha katika Jina la Yesu.


Father in the Name of Jesus Christ, you said that whatsoever we ask of you oh God in the Name of Jesus, we will receive, today I stand to make war in the spiritual realm. It is written, cursed be he that refrain’s his sword from shedding blood, today I exert the sword, which is the word of God to scatter every unclean spirit, dark forces of sorcerers and witches that are ruining my life, I scatter them in the Name of Jesus.

 

Imaandikwa kwasababu hii mwana wa Adamu alidhihirishwa ili azivunje kazi za ibilisi, leo ninavunja kazi za ibilisi kwenye maisha yangu katika Jina la Yesu. Leo ninawafuata na ninarudisha vyote walivyochukua kwangu Kwa damu ya Yesu Kristo. Afya yangu, mali zangu, nyota yangu na kila jambo walilolichukua kwangu ninarudisha katika Jina la Yesu Kristo.


It is written, for this reason did the son of man appear so that he should destroy the works of the devil, today I destroy the works of the devil over my life in the Name of Jesus. Today I pursue and recover all that was plundered from me by the blood of Jesus Christ. My health, my prosperity, my star and all else that was plunder from me I restore them all in the Name of Jesus.




Ninatangaza ushindi kwenye maisha yangu katika Jina la Yesu, ninatangaza kuwa mali zangu na Baraka zangu zimerudi na ninazifunika katika Jina la Yesu, leo nimeokoka kutoka kwenye mtego wa mwindaji katika Jina la Yesu.


I declare victory over my life in the Name of Jesus, I declare that my prosperity and blessings have been restored and I seal them in the Name of Jesus, today I am delivered from the hunter’s trap in the Name of Jesus.

IBADA KATIKA PICHA (Sunday's Surmon in Pictures):














(we are sorry for the wrong date on pictures;  They were all taken on 21st Oct. 2012)
UFUFUO NA UZIMA (THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH)
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM.

No comments:

Post a Comment