GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Sunday, October 28, 2012

UJUMBE: MKARIBISHE YESU KWENYE CHOMBO CHAKO (MESSAGE: INVITE JESUS INTO YOUR VESSEL)

Sunday Sermon with English Translation


Na Mch.: Mwangasa (Resident Pastor)
Maelfu wakisifu na kuabudu katika ibada ya leo (28 0ct.)

Multitudes during today’s services’ praise and worship(28th Oct.)
Mathayo 14:22-33, Yesu alikuwa akiendelea kutenda kazi alizokuja kuzifanya duniani na ukisoma kuanzia Mathayo 14:1-… Utaona aliwalisha watu elfu tano (waume). Na wakati watu wakitaamaki akawalazimisha wanafunzi wake kupanda chomboni ili wavuke bahari. Wanafunzi wake walipokuwa katikati ya bahari ndipo ilipotokea upepo mkali na kuanza kusukasuka chombo. Tuna mmbo mengi ya kujifunza kupitia maandiko haya:-


In the passage of Matthew 14:22-33, we see that Jesus was one who busied Himself with the mission that was bestowed upon Him to accomplish here on earth. In reading from Matthew 14:1, you will see that He fed five thousand people (this figure accounting only for the men that were present). Thereafter, Jesus constrained His disciples to enter into a ship that they should cross over the sea. While His disciples were along this journey though, their ship was tossed about with the waves as a strong wind was upon the sea. There are many things that we can learn from this passage:

HALI YA WANAFUNZI KATIKA CHOMBO: 
(THE DISCIPLES STATE OF AFFAIRS IN THE SHIP):
Ukitafakari kwa makini utaweza kuona hali ya wanafunzi chomboni; inawezekana walishaanza kumlaumu Yesu, au kumlaumu kwa kuwalazimisha kupanda chomboni na yeye asiwemo.

If you were to contemplate, you would begin to come to terms with the disciple’s state of affairs in the ship; it is quite possible in fact that they had began to grumble against Jesus, or grumble against His order for them to enter into the ship without Him accompanying them.
Pia, wanafunzi wa Yesu walikuwa wamekata tama, kwasababu tukio hili lilipotokea mwanzo walikuwa na Yesu chomboni akaukemea upepo lakini mara hii Yesu hakuwepo chomboni. kwa maana hiyo wanafunzi walikuwa katika hofu kuu.


Furthermore, the disciples of Jesus had given up as in a previous sea storm, Jesus was onboard the ship with them. This time round, they were not with Him and as such they were even more petrified and in great distress.

Biblia inasema hata wanafunzi walipomuona Yesu akitembea juu ya maji, wakahisi ni kivuli chake. hapa tunajifunza kuwa kuna wakati kwenye maisha unaweza kuwa unapita kwenye hatua ngumu kimaisha, na kwasababu ya hofu ukajikuta unaiogopa njia ambayo ndio ufumbuzi wa tatizo lako.


The Bible says that when the disciples saw Jesus walking on the water they perceived that it was a spirit. Hear we learn that there are times in life that one may find him or herself enduring a tough season and on account of fear, one will be afraid of a particular appearance or occurrence that will in fact be for their breakthrough.

KWANINI YESU ALITEMBEA JUU YA MAJI:

(WHY DID JESUS WALK ON THE WATER?):

Yawezekana umejiuliza kwanini Yesu alikuja huku akiwa juu ya maji; Kimsingi bahari ndio ambayo ilikuwa tatizo kwa wanafunzi wake, kwahivyo Yesu alikanyaga bahari kuonyesha kuwa  lile tatizo lilikuwa chini ya miguu ya Yesu. Kumbe Yesu yupo juu ya tatizo linalokuzunguka maana lipo chini ya miguu yake.


It could be that you have asked yourself, why did Jesus walk on the water? Principally, the tumultuous sea was the disciple’s key problem, as such Jesus walked on the water to demonstrate that that problem was under His feet. Of a truth, Jesus is above the problem that surrounds you, in other words, your problems are under His feet.

Na ndio maana Petro naye alijaribu kupita juu ya tatizo yaani bahari lakini alipoiangalia bahari alipata hofu. HAPA tunajifunza jambo kwamba hatakiwi kuliangalia tatizo bali mwangalie Yesu ambaye yupo juu ya tatizo.


That is why; Peter attempted to walk on his problem (i.e. the sea) but unfortunately became fearful when he displaced his focus to looking upon the boisterous elements. Here we learn that our focus should not be on our problems but rather on Christ alone who is on top of the problem.

Ukimwamini Yesu unavuka kutoka mautini unaingia uzimani, na Yesu ana mamlaka na funguo za mauti na kuzimu. Hivyo ukiwa kwenye tatizo, usiangalie tatizo bali mwangalie Yesu. unapoelekea kwa Yesu usipepese macho, mtazame Yesu aliyekufa msalabani kwaajili yako.   


If you believe in Jesus you will cross over from death to life; moreover, Jesus has the authority and keys of hell and of death. Therefore when you are in a predicament, do not look upon it but rather fix your focus upon the LORD. In moving toward Him do not shift your gaze, only behold Jesus Christ who died on the cross for you.

 
JAMBO LA KUFANYA UKIWA NDANI YA TATIZO:

(WHAT TO DO WHEN YOU ARE IN A PREDICAMENT):

Katikati ya bahari wanafunzi wakamuona Yesu kama tumaini lao, na ndipo Petro alipoamua kumfuata. kimsingi uamuzi wa Petro kumfuata Yesu kwa kutembea juu ya maji ni sahihi kabisa, ila tatizo ni kwamba petro alitumia uzoefu wake wa bahari ambao ukamfanya asiwaze sauti ya Yesu aliyemuita. watu wengi wameshindwa kutoka ndani ya tatizo kwasababu ya taarifa walizozisikia kutoka kwa watu.


In the midst of the raging seas the disciples saw Jesus as their defense and put their trust in Him, as such Peter was determined to go after Him. Peter’s decision to get to Jesus by walking on the water was a sound one indeed; but the problem was that he relied upon his familiarity of the seas which caused him to disregard the voice of the LORD who had called him. Many people have been unable to break out from their predicament because of what they have been told by others.

Mfano; Mtu ana tatizo la ndoa na ndio limeanza, lakini baada ya kuongea na mtu mwengine mwenye tatizo kama hilo, anamwambia kuwa amedumu kwenye tatizo hilo kwa miaka mingi. Taarifa hiyo moja tu inamfanya huyu ambaye tatizo la ndoa ndio limeanza, akate tamaa na kuingiwa na hofu  kabisa kwa kuhisi naye atadumu kwa miaka hiyo yote.


For example:  a certain newlywed has a marital problem, but after sharing this issue with another person who has a similar problem, the newlywed is told that he or she is rooted therein for the next good couple of years. This single opinion alone is highly likely to cause the newlywed to lose heart and be filled with fear, believing that he or she is stuck for good.

Ni muhimu kujua hakuna haja ya kuangalia tatizo wala watu wengine waliopo kwenye tatizo. tunatakiwa tumuangalie Yesu Kristo ambaye aweza kukutoa kwenye tatizo ulilonalo. unapomwita Yesu kwenye mwili wako uliojaa magonjwa atakapofika yeye yote yatakoma, ukimwita Yesu kwenye ndoa yako yenye matatizo atakapofika tatizo litakama.


It is important to know that there is no need to behold the predicament at hand, neither to look upon others who are also in the same boat. What is needful is for us to look upon Jesus Christ who is able to save from the predicament that one may be facing. When you call the LORD to your sickly body that is filled with disease, when He arrives all issues will cease. When you call the LORD to attend your marital problems, when He arrives the issue will cease.

Isaya 41:9-10 “wewe niikushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa; usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwamaana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.”  Kama ukijua jambo ambalo Mungu anataka utend kwenye tatizo utalibadili tatizo hilo na kuwa daraja la kukuvusha na kukupeleka kwenye hatma njema ya maisha yako.


Isaiah 41:9-10:
“Thou whom I have taken from the ends of the earth, and called thee from the chief men thereof, and said unto thee, Thou art my servant; I have chosen thee, and not cast thee away. Fear thou not; for I am with thee: be not dismayed; for I am thy God: I will strengthen thee; yea, I will help thee; yea, I will uphold thee with the right hand of my righteousness.”
If you knew what it was that God has intended to perform toward you in the midst of your predicament, you would give it a substitute title of bridge instead of problem; and it will be the kind of bridge that would take you up and over and toward your life’s pleasant destiny.

Maombi :

Prayer:

Baba Mungu katika Jina la Yesu Kristo leo nimetambua kuwa ninatakiwa nitakiwa nikutazame wewe ninapokuwa kwenye tatizo. ninaomba msamaha kwasababu ya kutazama mambo mengine badala kukutazama wewe Mungu, Mungu naomba unisamehe katika Jina la Yesu.


Father God in the Name of Jesus Christ, today I have discovered that I am to behold you whenever I find myself in any kind of situation. I ask you to forgive me because I have fixed my focus on many other things instead of you oh God, I ask you to forgive me in the Name of Jesus.


 
Katika Jina la Yesu nimeamua kukuita wewe leo, imeandikwa katika Yeremia 3:33 “niite, nami nitakuitikia, name nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.” Leo ninakuita katika Jina la Yesu. Mungu kutoka katika kiti chako cha enzi ninakuita katika Jina la Yesu. Ninakutumaini wewe Mungu katika Jina la Yesu. Natakanivuke na wewe Mungu hadi ng’ambo ya maisha yangu katika Jina la Yesu.


In the Name of Jesus, I have decided to call upon you today, it is written in Jeremiah 33:3, “call unto me, and I will answer thee, and shew thee great and mighty things, which thou knowest not.” Today I call upon you in the Name of Jesus. Oh God, before your throne I call upon the Name of Jesus. I trust in you oh God in the Name of Jesus. I want to cross over with you unto the other side of my life in the name of Jesus.


*picha zote zimechukuliwa katika ibada ya leo*

*All the pictures were taken during today’s service*



MWITE YESU KWENYE TATIZO ULILONALO!!!

INVITE JESUS INTO YOUR SITUATION!!

UFUFUO NA UZIMA {THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH}
TANGANYIKA PACKERS,
Dar es Salaam, TANZANIA

No comments:

Post a Comment