GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Friday, November 2, 2012

Somo: Roho ya ufahamu na hekima.

Na Mchungaji: Adriano Makazi (RP)

Isaya 11:1~2
1 Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.
2 Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana;

Mambo mchache ya kufahamu.
-shetani huzifumba fahamu za watu waoumbwa kwa sura na mfano wa Mungu ili wasizijue haki zao.
-kwenye bustani ya edeni nyoka alimdanganya Hawa akamwambia ukila matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya utakuwa Kama Mungu
-lakini tayari waliumbwa kwa mfano na sura ya Mungu
Imeandikwa mtaifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru (Yohana 8:32)
1 Yohana
2. Cor 4:3-4....mungu wa dunia amepofusha fikila zao wasio amini ili isiwazukie nuru ya injili iliyo sura yake Mungu

Yohana 1:1~5
1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
5 Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.
Neno ni Mungu
Neno ni Yesu
Neno ni mkate
Neno ni njia
Neno linaweza kuvaa mwili

YOHANA 1:14
14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.

(..."kila aliye mkiri Yesu ni mwana wa Mungu ,,,,,Mungu yuko ndani yako....")
Ukizishika amiri zake watatu watakuja kukaa kwako.
i). Mungu baba.
ii). Mungu mwana.
iii). Mungu Roho Mtakatifu

YOHANA 14:21~23
21 Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.
22 Yuda (siye Iskariote), akamwambia, Bwana, imekuwaje ya kwamba wataka kujidhihirisha kwetu, wala si kwa ulimwengu?
23 Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.
(.....Tamani Mungu afanye MAKAO kwako.....")

 Mdhihilishe Yesu kwa watu waliokuzunguka usimfungie Yesu ndani ya box.

No comments:

Post a Comment