GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Monday, November 5, 2012

UJUMBE: NEEMA YA MUNGU {MESSAGE: THE GRACE OF GOD}

Sunday Sermon's notes with English Translation!!!

   
Na. Mch. Mwangasa {Resident Pastor}      4.11.2012 


TAFSIRI YA NEEMA YA MUNGU KIBIBLIA:

THE BIBLICAL INTERPRETATION OF THE GRACE OF GOD:



Tito 2:11 “maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa…” Waefeso 2:1-10. Kuna tafsiri nyingi sana ya neema ya Mungu; lakini tafsiri ya karibu zaidi inasema neema ni upendeleo wa Mungu kwa mwanadamu ambao hatukuungaramia, tafsri nyingine inasema neema ni daraja kati ya Mungu na wanadamu. Tafsiri nyingine ya neema ya Mungu kwetu ni njia ya Mungu kumfikia mwanadamu kwa njia ya Kristo Yesu.



Titus 2:11 “For the grace of God that bringeth salvation hath appeared to all men…”

Ephesians 2: 1-10

There are many interpretations of the grace of God; but the most accurate states that grace is God’s unmerited favor toward man. Grace has also been interpreted as the bridge between God and man. Another interpretation of God’s grace for us is that it is the path that God takes to get to man, through Christ.



Hata kwenye agano la Kale kulikuwa na tafsiri ya neema mfano utakaposoma katika kitabu cha Mwanzo 6:8  “lakini Nuhu akapata neema machoni pa BWANA”. Kimsingi, ulimwengu wa kipindi kile uliokolewa kwasababu ya neema ambayo Nuhu aliipata kwa BWANA. Pia ukisoma katika kitabu cha Yona 4:2; Kwa Tafsiri ya Yona neema ilikuwa ni tabia ya Mungu KWAMBA Mungu ni mwenye rehema na huruma yaani ni kawaida ya Mungu.



Even in the Old Testament we can find a mention of grace, for example when you read Genesis chapter six verse eight (Genesis 6:8)But Noah found grace in the eyes of the LORD.” Principally, those who were saved at that time were saved on account of the grace that Noah had received from the LORD. Furthermore, if you read in the book of John chapter four verse two (John 4:2), John’s definition of grace is that it is the character of God; His compassion and mercy are part and parcel of His nature.



Ukiangalia katika agano jipya tunapata tafsiri nyingine ya neema; Yohana 1:7; kabla ya Kristo upendeleo wa mtu kwa Mungu ulikuwa unapatikana baada ya mtu kutenda matendo mema; lakini Yohana anataja neema kama upendeleo unaokuja bila kugharimia. Kimsingi; ingawa wanadamu walikuwa wametenda dhambi lakini pamoja na dhambi za wanadamu Mungu akaja kumwokoa Mungu, ndio maana katika  Warumi 3:24, Paulo anaeleza kuwa tumepokea ukombozi wa Mungu  bila kugharimia.



Further sifting through the New Testament uncovers another definition of grace, John 1:7. Prior to Christ appearing, an individual’s benevolence and outward righteousness was the only way in which one could obtain the favor of God. But John mentions grace as being unmerited favor. So in effect even though man has sinned, despite this sinful state God came to save man and that is why in Romans 3:24 Paul says that we have received salvation freely.



TUMEOKOLEWA NA NEEMA YA MUNGU:

WE ARE SAVED BY THE GRACE OF GOD:



Kama utapata nafasi ya Kufuatilia Maisha yako utagundua kuna wakati ulipita mahali kwasababu ya neema ya Mungu. Tumepata neema bure.  Unapokuwa umeokoka unakuwa umepokea neema ya Kristo iliyo ya bure; ndio maana hata kama unapitia katika hali ngumu lakini ni muhimu kujua kuna neema ya Mungu iliyo kuu ambayo ni zaidi ya matatizo au magonjwa unayopitia. Hii ndio maana ya lile andiko katika Tito 2:11 “maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa…” Neema ya Mungu yatutosha.



In taking time to reminisce upon your life, you will discover that there were times that it was only by the grace of God that you managed to make it through. Grace has freely been bestowed upon us. In that you are saved, it is that you have received this free grace of Christ; that is why even if you are enduring great hardship it is important to know that there exists the grand grace of God which is greater the problems or sickness that you are enduring. This is what is meant in Titus 2:11For the grace of God that bringeth salvation hath appeared to all men…” God’s grace is all sufficient.



Hakuna haja ya kuangalia watu wanakuita nani kwasababu hata kipindi cha Yusufu watu walimwona mfungwa mbakaji lakini Neema ya Mungu ilimwita kuwa ni waziri mkuu wa Misri. Ingawa alipitia kwenye wakati mgumu lakini bado neema ya Mungu ilimwita waziri Mkuu. Unapoona hayo ni muhimu kutenga muda wa kumshukuru Mungu kila siku, unapoliona jua linawaka yupo anayesababisha liwake mshukuru Mungu kwa neema yake.



There is no need for you to be concerned with the name-calling being people hurled at you because even in Joseph’s days, people labeled him prisoner and rapist but it was the grace of God that instead called him Prime Minister of Egypt. Despite the hardships he endured, the grace of God still called him Prime Minister. In beholding this it thus becomes important to put aside time to for thanksgiving every day; for us just to see the sun rise is enough reason to give thanks to God for His grace.



NEEMA YA WOKOVU:

GRACE OF SALVATION:



Hii ni neema iliyondani ya watu waliompokea Yesu Kristo. Wakati wengine wakipitia matatizo wanaenda kwa waganga wa dunia hii sisi tuliompokea Yesu Kristo tuna neno la ushindi (kwa kupigwa kwake sisi tumepona Isaya 53:5). Unapokuwa umeokoka yaani umempokea Yesu Mungu anakufanya uwe mtoto wake hivyo anakuwa anataka kila unachokitenda kiwe nembo ya utukufu wake.



This is the grace which is within those who have received Christ Jesus. While the people of this world consult with sorcerer’s and witches for their hardships, we who have received Jesus Christ have the words of victory: by His stripes, we are healed (Isaiah 53:5). When you are saved (when you have received Jesus) God makes you His child and as such he desires for His glory to be displayed in all that you do.



Kumbe ukiokoka unakuwa umepokea neema ya Mungu lakini hatuwezi kutenda dhambi kwasababu kuna neema. Neema inatuagiza kuishi maisha matakatifu. Mungu hachanganywi na dhambi. Inawezekana unapitia katika hali ngumu kimaisha lakini jambo la kujua ni kuwa neema ya Mungu yakutosha. Tuna neema ya Mungu sisi tuliompokea Yesu Kristo kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yetu.



In effect when you are saved you have received the grace of God, but because there is grace we must not use it as an excuse for committing sin. Grace commands us to live a holy life. God does not mix with sin. It could be that you are going through a hard time in life but it is imperative to know that God’s grace is sufficient. For those of us who have received Jesus as LORD and Savior of our lives, we have the grace of God.
THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH

KAWE, DAR ES SALAAM,
TANZANIA.

1 comment: