GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Sunday, November 25, 2012

UWEZA MUNGU WETU

Na Mchungaji: MWANGASA (RP)





Danieli 3:1-30; 6:10-;  tumesoma habari mbili ambazo zinawahusu kwa ukaribu watu wane yaani, Danieli, Meshaki, Shedraka na Abednego.  Kipindi kile Babeli walivamia Yerusalemu na kuwachukua waisraeli utumwani, na kati yao wakachukuliwa watu kadhaa kwenda kufanya kazi za mfalme, baadhi ya waliokuwepo ni hawa wane. Kupitia hao tunapata kujifunza:-





Habari ya Kwanza kuhusu Sanamu iliyowekwa na Mfalme Nebkadneza: (Danieli 3:1-30):

Mtoto akitoa ushuhuda baada ya Maombezi
Mfalme Nebkadneza baada ya kuvamia wayaudi na kuwachukua utumwani, akatenga siku na kuwalazimisha watu wote waiabudu sanamu aliyoitengeneza. Lakini Shedraka, Mashaki na Abednego hawakukubali kuinama kuiabudu sanamu. Ndipo baadhi ya Wakaldayo wakapeleka mashtaka, tunaona hili katika mstari wa 8* “Basi baadhi ya Wakaldayo wakakaribia, wakaleta mashitaka juu ya Wayahudi.” Hawa ndio waliopeleka mashtaka kwa Mfalme. Mfalme akakasirika akasema, moto na uongezwe mara saba. Kibiblia mara saba ni namba ya ukamilifu wa Mungu, ukianzia kwa habari ya ukuta wa Yeriko ulianguka siku ya saba hivyo, hawa wakina shedraki hawakushtuka kwasababu walijua ukamilifu wa utukufu wa Mungu umekaribia.

Jambo la ajabu likatokea pale mfalme alipowatupa kwenye moto, maana moto uliwalamba na kuwateketeza wale walioenda kuwatupa. Lakini wao hawakuungua, moto haukuwaweza kabisa.  Lakini jambo la muhimu kujifunza kupitia habari hii. Pata picha ya hali iliyokuwepo kwa hawa watu watatu, maana lilikuwa ni jambo gumu kwao. Wangetarajia Mungu awaokoe mapema yaani Mungu asingeruhusu watupwe kwenye moto.  

Kwanza; Mungu alitaka atimize neon lake alilonena kupitia nabii Isaya KWAMBA “Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.” Isaya 43:2, Mungu wetu ni moto ulao, na kwakulithibitisha hilo akaruhusu hadi wafikie dakika ya mwisho, ili ajichukulie utukufu wake.


Pili; Mungu huwa anaokoa dakika ya mwisho, pale unapohisi kuwa huna msaada mwingine ndipo Mungu anajichukulia utukufu; watu wengi wanakata tama mapema bila kujua kuwa Mungu huokoa katika saa ambayo hukuitarajia, Wakina Shedraka wangetarajia Mungu awaokoe katika hatua ya kwanza, lakini Mungu alikuja kwao dakika ya mwisho.

Tatu; tunaona watu walioenda kuwashtaki kwa Mfalme; hapa tunajifunza kuwa unapoishi kuna watu watasema, kuna watu watakupinga, kuna watu watakushtaki kwa waganga wa kienyeji wakitaka kukuangamiza. Lakini ni muhimu kujua kuwa Mungu wetu ni Mungu wa kuokoa. Unapookoka Mungu anakuwa pamoja na wewe.

Nne; ndani ya moto kulikuwa na mtu wane; Yesu Kristo yupo pamoja nasi, imeandikwa, “wa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu;” 1 Yohana 5:4, hakuna moto ambao umeanzishwa na wanadamu, utakaoweza kukushinda. Sisi tumezaliwa na Mungu, na lazima tuushinde ulimwengu. Ni kweli unaweza kuwa unapitia kunye tatizo ambalo limekuwa moto kwenye maisha yako, lakini jambo la muhimu kujua kwamba, Hakuna moto uliofanywa na wanadamu utakaoweza kukushinda, kwasababu maana baada ya kuokoka unakuwa umezaliwa na Mungu.


Habari ya pili kuhusu, Danieli na Mfalme Dario: (Danieli 6:10-28):

Katika kipindi cha Mfalme Dario, watu kadhaa wakaamua kwa hila kumuangamiza Danieli, na hawakuona jambo lolote la kumuangamiza isipokuwa kwa habari ya Mungu wake. Imeandikwa, “Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba.” Hivyo, Mfalme akaweka muhuri kwenye sharia, lakini Danieli bila kujua ile sharia yeye akaendelea na Ibada kama kawaida; wakati huohuo, liliandaliwa ntanuru la samba ambao nao hawakupewa chakula kwa muda wa siku saba. Lakini cha ajabu kuwa walipomtupa ndani ya shimo wale samba hawakuweza kumdhuru. Ndipo mfalme akaamuru wale waliopangia hila watupwe wao. Ambapo samba waliwadaka hewani kabla ya kufika chini. Katika habari hii kuna mambop kadhaa ya kujifunza:-

Kwanza; Simba wakagoma kumla Danieli; biblia inasema, “Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika wake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto.” Waebrania 1:7.  Mungu anasema hutufanya sisi watumishi wake kuwa miale ya moto, n wale samba walimuona danieli kama mwali wa moto hivyo hawakuweza kumrarua. Unapookoka unakuwa mwali wa moto katika ulimwengu wa roho na hakuna silaha inayoweza kukudhuru.

Pili; Danieli alikuwa mtu wa kabila la Yuda na kwaabari ya Yuda kuna Simba wa kabila la Yuda, samba wasingeweza kumdhuru, kwa kuwa Danieli alikuwa pamoja na Mungu aliye simba wa kabila la Yuda. Hakuna haja ya kuogopa yale magumu unayopitia,. Kwa kuwa ndani yako kuna simba wa kabila la Yuda yaani Yesu Kristo. Pamoja na kukosa chakula kwa muda wa siku saba, hawakuweza kumla Danieli mtu wa Mungu.

Tatu; baada ya Mfalme kugundua kuwa samba wameshindwa kumuua Danieli, ndipo akaamuru wale waliotaka kumuua Danieli kwa hila waingize wao shimoni. Likatimia andiko kuwa, “Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake;  Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.” Mhubiri 10:8, wale waliokuandalia kifo au aibu kwa hila, itamrudia mwenyewe. Mungu huwaondoa wenye haki kwenye ajali na kuwaweka waovu badala yake.  Wanakupiga vita kwa hila usiangaike we mwangalie Mungu, yeye atakupigania.

Unapokuwa unaomba, inabidi ujue kuwa upo na Mungu awezaye kutenda kwa namna ya ajabu sana; Yoshua 10:9 “Bwana naye akawatapanya mbele ya Israeli, naye Israeli akawaua uuaji ulio mkuu hapo Gibeoni, akawafukuza waikimbilie hiyo njia ya kukwelea kwenda Bethhoroni, na kuwapiga hata kufikilia Azeka, tena hata kufikilia Makeda. Kisha ikawa, hapo walipokuwa wakimbia mbele ya Israeli, hapo walipokuwa katika kutelemkia Bethhoroni, ndipo Bwana alipowatupia mawe makubwa kutoka mbinguni juu yao hata kufikilia Azeka, nao wakafa; hao waliokufa kwa kuuawa na hayo mawe ya barafu walikuwa ni wengi kuliko hao waliouawa na wana wa Israeli kwa upanga.” Mungu aliwahi kuwaangushia mawe, maadui wa Israeli, Unatakiwa ujue BWANA amewatia adui zako mikononi mwako uwatende unavyotaka. Unatakiwa ujue hauko peke yako Mungu yupo kwaajili yako, kukuokoa. Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa na njia za kutoka mautini zina yeye!!!



Glory Of Christ (T) Church
Ufufuo na Uzima
Dar es Salaam, Tanzania.

1 comment:

  1. very blessing mass,nimemiss kweli kanisa la Ufufuo na uzima Mbarikiwe sana

    ReplyDelete