GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Sunday, November 11, 2012

UJUMBE: WAKATI WA BWANA


Na Mch. Mwangasa (Resident Pastor) 11/11/2012

Mch. Mwangasa (Resident Pastor)
Akifundisha Neno la Mungu
WAKATI KWA KILA JAMBO:


Mhubiri 3:1-8 “kila jambo kuna majira yake…” Mhubiri 9:11 “Nikarudi na kuona, chini ya jua, si wenye mbio washindao katika michezo… … lakini wakati na bahati huwapata wote”. Biblia inataja kwa kila jambo linalotokea lina majira yake; hakuna jambo linalotokea kama sio wakati wake kutokea. Kwa bahati mbaya sana, wanadamu tunaishi kwa kufuata majira na si majira kuwafuata watu, yaani hatuwezi hatuna jinsi ya kubadili majira, lakini kuna jinsi ya kuishi katika majira tofauti. Watu wengi wamekata tama kwasababu ya kutokujua majira na wakati katika maisha yao.


Platform Team wakimwabudu Mungu
leo wakati wa kusifu na kuabudu


Mhubiri 7:14 “siku ya kufanikiwa hufurahi, na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya hiyo moja kwenda sambasamba na hiyo ya pili, ili mwanadamu asiweze kufahamu jambo lolote litakalofuata baada yake.” Maana ya maneno haya ni kwamba duniani Mungu ameweka mambo mazuri na mabaya pamoja; yaani kuna wakati wa mambo mabaya na saa ya mambo mema. Kwasababu hiyo, watu wameshindwa kujua litakalo fuata mbeleni. Na Mungu amefanya hivi makusudi ili watu wamtafute na kumwomba yeye peke yake.



Tokea siku uliyookoka Mungu  ndiye anayeshughulikia maisha yeko. Na ndio maana unahitaji kujua baada ya kuokoka thamani yako ni kubwa sana; unatakiwa ujue kuwa Mungu anayekushughulikia ndiye muumbaji wa mbingu na nchi; naye ameweka majira na wakati kwa kila jambo.


Wakati wa Kusifu na Kuabudu: UFUFUO NA UZIMA
MAMBO YA KUFANYA KIPINDI UNASUBIRI WAKATI BWANA:


Ukisoma kwa habari ya Hana:

(Angalia.. 1Samweli 1:1-…)  Hana alikaa muda mrefu bila kupata mtoto lakini jambo la muhimu ambalo alifanya ni kwamba, akawa anaenda kuomba huko shilo kila mara. Kumbe pamoja kuwa tunapitia katika wakati mgumu ni muhimu kuomba, watu wengi wameshindwa kupokea na hata kutokujua wakati wao kwasababu wamekuwa hawaombi, wakati wapo katika magumu. Haijalishi, tatizo limechukua muda gani, kwasababu hata tatizo la Hana lilichukua muda mrefu lakini aliendelea kuomba. Ndipo biblia inasema katika mstari wa  20” “ikawa wakati ulipowadia,Hana akachukua mimba akamzaa mtoto mwanaume” kumbe mtoto wa Hana *Samweli, alikuwa anasubiri wakati wake ufike. Tatizo halikuwa kwa Hana, bali wakati ulikuwa bado haujafika. Jambo la kujifunza hapa ni kuwa, wakati Hana anasumbuka kwa kukosa mtoto, alitumia muda ule kuomba. Hili ni jambo la muhimu sana kipindi unasubiri ahadi yako.


Mungu alikuwa ameruhusu Hana apite katika shida ile ili aandike Historia. Wakati mwingine Mungu anaweza kuruhusu upitie wakati mgumu ili utengeneze historia nyingine kwenye maisha yako. Hivyo ni muhimu kujua muda ule unaosubiri muujiza wako unatakiwa ufanye nini. Kama Hana angekatatamaa, Samweli asingekuja leo na hata kama angekuja ingekuwa si kwa kusudi la mwanzo. Subiri wakati wa BWANA, hakuna haja ya kukata tamaa wala kuvunjika moyo.




Kwenye Biblia tunaweza kuona maisha ya Yusufu:

Tunajifunza maisha ya Yusufu ambaye aliota ndoto (angalia Mwanzo 37:5), kuwa mkuu kuliko ndugu zake; ingawa alipitia kipindi kigumu sana, ambacho kama asingesimama na BWANA angekuwa ameshakata tamaa. Yusufu alijua kuwa Mungu ni Mungu wa wakati na majira katika kila jambo. Jambo la kujifunza kwa Yusufu ni kuwa hakutenda dhambi, hata ilipobidi kwenda gerezani kwaajili ya kukwepa dhambi. Kumbe ni muhimu kujilinda na dhambi wakati unamngojea BWANA. (angalia Mwanzo 37-48). Siku zote mawazo ya Mungu sio ya wanadamu, na ndio maana Yusufu aliwaambia ndugu zake kuwa ninyi mliniwazia mabaya lakini Mungu aliniwazia mema.kumbe jambo linguine la kufanya wakati unasubiri ahadi yako kwa Mungu ni kutokutenda dhambi.



Pia tunaweza kujifunza kuhusu jambo hili kupitia Nabii Danieli:

Danieli 9:1-3; Danieli baada ya kusoma kitabu cha tarehe, akafahamu kuwa ulikuwa wakati wa wana wa Israeli kutoka utumwani. Kumbe kuna umuhimu wa kusoma wakati na majira, hata mkulima mzuri ni yule anayejua kusoma majira na wakati. Ndipo Danieli akachukua hatua ya kufunga na kuomba ili kumwomba Mungu watoke utumwani. Jambo la ajabu analokutana nalo ambalo ni kikwazo kingine ni Mkuu wa anga la Uajemi, (angalia Danieli 10:1- … ). Kumbe inawezekana wakati wako ukafika lakini kuna mkuu wa anga (shetani) ambaye amekaa kuzuia. Kuna watu wanapitia wakati mgumu na wa kukatisha tamaa na kumbe kuna mkuu wa anga anayezuiua. Jambo la kufanya ni kupambana na mkuu wa anga hapo lazima wakati wako udhihirike.



Inawezekana umedumu kwenye tatizo kwa muda mrefu sana, umefika hata hali ya kukata tamaa lakini ni muhimu kujua kuwa kila jambo lina wakati wake. BWANA akiamua kutenda kwako, hakuna wa kuzuia kusudi la BWANA.  Unapookoka unatangaza wakati wa BWANA kwenye maisha yako, huu ndio wakati wa BWANA. Hata Yusufu alipita kwenye nyakati tofauti na ngumu lakini wakati wa BWANA ulipotimu aliyaona aliyoahidiwa. Huu ndio wakati wa BWANA kwako na unatakiwa uutangaze katika ulimwengu wa roho. Huwezi kumiliki bila kupigana na mkuu wa anga azuiaye, na kutangaza wakati wa BWANA. Hata Yesu wakati ulipofika alitangaza wakati wa BWANA duniani, tangaza wakati wako katika Jina la YESU. Huu ni wakati wako katika Jina la Yesu.



Translation:


MESSAGE: THE TIMING OF THE LORD

With Ps. Mwangasa (Resident Pastor) 11/11/2012

THERE IS A TIME FOR EVERYTHING:

Ecclesiastes 3:1 To everything there is a season…” [Read Ecclesiastes 3:1-8].
Ecclesiastes 9:11I returned, and saw under the sun, that the race is not to the swift…but time and chance happeneth to them all.”
The Bible tells us that to everything there is a season and that nothing comes to pass outside of its appointed time. Unfortunately though for mankind, we live in step with the seasons, and not the seasons occurring in step with us. There is no means available to mankind to alter the seasons but what there is, is a way in which man can live to cope through the different seasons. Many people have given up because they are unaware of the times and seasons of their lives.

Ecclesiastes 7:14In the day of prosperity be joyful, but in the day of adversity consider: God also hath set the one over against the other, to the end that man should find nothing after him.”
These words demonstrate that in the world God has put both prosperity and adversity, indicating that there is a time for adversity and a time for prosperity. God has allowed this on purpose so that man, in not knowing which lies ahead will entreat Him only.


From the day of your salvation God began to concern Himself with your life. Therefore it is imperative for you to know that from salvation you are of great value and that the God who concerns Himself over you is the creator of the heavens and the earth and He has appointed times and seasons for everything.

WHAT TO DO WHILE WAITING FOR THE TIME OF THE LORD:

In reading up on Hannah:

 (Refer to 1 Samuel 1, from verse one onwards)
Hannah was barren and without child for many years but the notable thing she did was that she ensured to go for prayer at Shiloh at its every appointed time. Despite the hardship that we go through we see here the importance of consistent prayer, many people have not been able to receive and be made aware of what kind of season they are in because they do not pray, her time came about in the midst of her hardship. The duration of the problem does not matter because even Hannah was barren for a long time but she continued in prayer. That is why the Bible says in verse twenty “Wherefore it came to pass, when the time was come about after Hannah had conceived, that she bare a son…” Hannah’s son, Samuel was awaiting his right time to come.
As such the problem was not with Hannah, but rather that her time had not yet come. What we can learn from Hannah is that despite her grief over her barrenness she utilised her time well in prayer. This is a very important thing to do while awaiting your promise.

God allowed Hanna to pass through that problem so that she would make history. Sometimes God can allow for you to endure hardship so that you can attribute a different history to your life. Therefore it is important to know what to do while you are waiting for your miracle from the LORD. If Hannah had given up, Samuel would not have been born and even if he was later born it would have been out of line with God’s original purpose. Wait for the time appointed by the LORD, there is no need to give up or have a broken heart.

From the Bible we can also get an analysis of Joseph’s life:

We can learn from the life of Joseph who dreamt that he was head over his brothers (refer to Genesis 37:5) that despite the hard times that he endured; if he had not held fast unto the LORD he would have given up. Joseph knew that God is a God of times and seasons and that there is a time for everything. What we can learn from Joseph is that he did not sin, and for his refusal to sin he even ended up being imprisoned.  Hear we learn the importance of keeping yourself from sin while awaiting the LORD (refer to Genesis 37 – 48). The thoughts of God are never as those of man, and that is why Joseph told his brothers that even though they had purposed evil toward him God purposed good. So in effect you must ensure not to commit sin while awaiting your promise from the LORD.


Furthermore, we can instruct ourselves about this matter via the Prophet Daniel:

Daniel 9: 1-3
After reading from prophetic records Daniel became aware that it was time for the restoration of Jerusalem. So here we see the great importance in investigating on times and seasons, a good farmer is he who knows how to understand the seasons. It was then that Daniel went forward with fasting and prayer that God should restore Jerusalem. An amazing thing to note of here is the contending of the Prince of Persia (read Daniel chapter ten from verse one). We see that it could be that your time has come but the Prince of the Air (Satan) has positioned himself in opposition. There are people who go through hard and discouraging times but behind it all is the Prince of the Air who is opposing. What needs to be done is warfare against the Prince of the Air and surely then, your time will manifest.


It could be that you have enduring the same problem for a very long time, and you are even at the point of giving up but assuredly that there is a time for everything. When the LORD has purposed to perform something toward you, no amount of opposition can prevent the fulfilment of the purpose of the LORD. When you got saved it was your declaration that it from then it is the LORD’s time in your life, this is the LORD’s time. Even Joseph went through different seasons and hard times but when the time of the LORD came about he saw all that he had been promised. This is the time that the LORD has purposed for you therefore ensure to declare so in the spiritual realm. You cannot dominate without battling against the Prince of the Air who opposes, and to declaring that it is the time of the LORD. Even Jesus when He arrived He declared that it was the time of the LORD on the earth, declare your time in the Name of Jesus. This is your time in the Name of Jesus!



GLORY OF CHRIST (T) CHURCH

UFUFUO NA UZIMA

DAR ES SALAAM

TANZANIA.

2 comments: