GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Thursday, August 16, 2012

IMANI DHIDI YA SHETANI


Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana (Waebrania 11:1). Kuna tafsiri nyingi za imani lakini tafsiri hii ni sahihi zaidi. Kwasababu imegusa maeneo yote, kiufupi ni tafsiri ambayo unapoisoma inakupa mwanga halisi wa imani!

Biblia inasema si kwa mafumbo bali waziwazi kuwa imani chanzo chake ni kusikia, kama hukusikia huwezi kuipokea imani, tena haiishii hapo, inaenda mbali na kusema kusikia huku kunatokana na neno la Kristo (Warumi 10:17). Kumbe IMANI dhidi ya shetani haiji kwa kusikiliza neno la mganga bali ni kwa kusikiliza neno la Kristo!

Jambo lingine, imani pasipo matendo, biblia inafananisha na roho bila mwili (Yakobo 2:26). Kimsingi kabla ya roho kuingia kwenye mwili, mwili ulikuwa kama sanamu kiufupi (functionless), kama roho ilipoleta uhai kwenye mwili, ndivyo matendo yanavyoleta uhai kwenye imani. Waweza kuwa na imani lakini kama haiambatani na matendo ile imani imekufa.

Ili kupambana dhidi ya huyu mzee kibogoyo au shetani kwa jina maarufu, unatakiwa uchague uwanja wa kupambania. Na ukishindwa kujua uwanja wa kupigania, kimsingi unakuwa umeshindwa kabla ya kuanza. Kuna viwanja aina mbili, kwanza cha mawazo na pili cha imani. Ukipambana na shetani kwenye uwanja wa mawazo, lazima akushindi kwasababu yuko fiti katika eneo hilo kiufupi ni uwanja wake wa nyumbani.

Ila uwanja wa imani + matendo yaani unamfanya shetani awe ugenini, alafu hana washabiki kwa maana hata mapepo wanaelewa ni saa ya kushindwa. Kivipi? Mawazo yako ndani ya nafsi, na nafsi imejaa yale mambo uliyopitia ambayo ni ya hapa duniani. Na kama unavyojua shetani kaisuka hii dunia anavyopenda yeye kwahiyo kukubali kuwa uwanja huo maana yake rahiso ni kuwa uwanja wa ugenini. Lakini uwanja wa imani ni wa nyumbani, kwanza kwakuwa wenyeji wetu uko mbinguni(Wafilipi 3:20), pili imani yatokana na neno la Kristo, ambalo limemwagiwa sifa kemukemu (Waebrania 4:12)

Tena Mtaifahamu Kweli, Nayo  Hiyo Kweli Itawaweka Huru (Yohana 8:32)
Hii ni imetolewa kwenye masomo mbalimbali ya baba yanayohusu IMANI…. Barikiwa!!!

No comments:

Post a Comment