GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Wednesday, August 15, 2012

JINSI SHETANI ANAVYOFUNGA MWILI:


Na Mchungaji: Josephat Gwajima.

Shetani ana mbinu nyingi za kumfunga mtu, na ndio maana Biblia inasema 2Wakorintho 2:11 Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.  Kwa maana hiyo imetupasa kujua mbinu anazotumia shetani, ili kuufunga mwili wa mwanadamu. Watu wengi wanasumbuliwa na vifungo vya mwilini, ikiwemo magonjwa mbalimbali hii ni kwasababu ya kutokujua siri hii, kuwa mwili ni udongo. Sasa tuone njia ambazo shetani hutumia kuufunga mwili, ambao kwa asili ni udongo, tofauti yake na udongo wa kawaida ni kwamba mwili uliwahi kushikwa na Mungu, pili mwili wa binadamu unauhai unao upata kutoka kwenye roho: njia kadhaa anazotumia shetani...

i)                   Kupanda na Kung’oa:
Mhubiri 12:7Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.Kama tulivyoona toka mwanzo kuwa mwili ni udongo, na kwamaana hiyo, unavyoweza kuutendea udongo wa kawaida ndivyo hata mwili nao waweza kuutendewa vivyo hivyo katika ulimwengu wa roho. Kwenye udongo wa kawaida watu hupanda na kung’oa, kwahiyo na kwenye mwili ambao ni udongo kunaweza kupanda vitu mbalimbali. 

Biblia inasema Mungu ni roho (Yohana 4:24), lakini pamoja na hilo kwamba ni roho aliweza kupanda bustani katika kitabu cha Mwanzo 2:8 Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya.Ingawa Mungu alikuwa roho lakini aliweza kupanda bustani, na maandiko mengine kuonyesha BWANA aweza kupanda (Zaburi 104:16; Hesabu 24:6). Kumbe roho zaweza kupanda na ndio maana katika Mathayo 15:13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa.Kumbe kuna mapando ambayo hayajapandwa na Mungu, na yanatakiwa yang’olewe. Hapa tunafundishwa kuwa kuna uwezekano wa mwili wa binadamu ambao ni udongo, kupandiwa vitu kama udongo wa kawaida.

Ayubu 4:8, Shetani ni mkulima analima maovu, na kupanda madhara. Mwili wa binadamu unaweza kupandiwa mmea au mti. Na ndio maana mtu anaweza kuwa safi rohoni na nafsini, lakini kumbe kwenye mwili wake amepandiwa vitu. Kwa namna hii shetani amefunga miili ya watu wengi sana bila ya wao kujua, ukifunguliwa macho ya rohoni ukaona utagundua kuwa watu wengi wamefungwa kwa jinsi hii. Na biblia inasema kwa muda nchi idumupo majira ya kupanda na kuvuna hayatakoma (Mwanzo 8:22), hivyo dunia imekaa katika kupanda na kuvuna.

Tunaweza kujifunza zaidi katika hili, kwenye Mambo ya walawi 19:19 “…usipande shamba lako mbegu za namna mbili pamoja;…” utajiuliza kwanini Mungu aliyasema haya kwenye torati, kimsingi torati asili yake ni ya rohoni Warumi 7:14 “…torati asili yake ni ya rohoni;…” sasa basi hayo Mungu aliagiza kuonyesha kuwa kuna uwezekana kwenye udongo kukapandwa pando la kiMungu au la shetani.  Maana ya maneno haya ni kwamba pale ambapo Mungu amepanda shetani hatakiwi kupanda, Mfano, Ukiokoka Mungu anakupandia mbegu ya amani, upendo, furaha na afya. Hapo shetani hatakiwi kupanda mbegu yake, na hapo andiko la kila pando asilolipanda Mungu, litangolewa linapoleta maana.

Asili mia kubwa ya magonjwa yanayowapata watu, ni matokeo ya mapando ya rohoni. Mtu anaweza akawa anaonekana kwa nje amepooza kumbe kwenye mwili wake amepandiwa mti. Na pepo wamekaa kwenye mwili wake kama mti.

ii)                Pepo anaweza kugeuka na kuwa:
Shetani na mapepo wachafu wote ni roho, na wanafanya kazi katika ulimwengu waroho. Na kwa hivyo kuna sifa ambazo wanazo zinazowatofautisha na wanadamu ojawapo ni uwezo wa kujibadilisha kwenye maumbo mbalimbali. Ukisoma kitabu cha 1wafalme 22:19-23 “…Akatokapepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, Mimi nitamdanganya. Bwana akamwambia, Jinsi gani? Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo kinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka ukafanye hivyo...Tunaona huyu pepo, hakuwa pepo wa uongo lakini aliweza alijibadili na kuwa pepo wa uongo. Kumbe kimsingi shetani na mapepo yanaweza kujibadili na kuwa umbo wanalotaka.

Kama tulivyoona kuwa mwili wa binadamu ni udongo, na kwenye udongo waweza kuchoma vitu kama kisu, kunawanyama wanatambaa, mimea inaota na hatakuchimba shimo. Hivyo mapepo wao wapo katika ulimwengu wa roho kwahivyo wakiuangalia mwili wanaona ni udongo kabisa, sasa wanapotumwa na mchawi au mganga wa kienyeji, wanakuja na kujiuza na kuwa kitu kile walichotumwa kufanya. Mfano, waweza kumkuta mtu analalamika kuwa kuna vitu vinatembea kwenye mwili, kumbe ni pepo kajigeuza akawa mnyama atambaaye, mtu anawashwa mwili kumbe mmea wa upupu au mwili unachoma kumbe pepo kajigeuza na kuwa kisu.  Shetani yupo na anatenda kazi ya kufunga miili kwa namna hiyo.

Pepo anaweza kujibadili na kisu cha kuchoma moyo, na matokeo yake utamwona mtu huyu anakuwa na uchungu au anakosa amani kila wakati. Jambo linaweza kuwa dogo tu lakini likamuumiza sana moyo, kumbe kuna pepo aliyejibadili na kuwa kisu. Kinachofanyika ni kwamba pepo ametumwa na kunuiziwa awe kisu, hivyo anabadilika na kuwa kisu kwenye moyo ili usione amani kwenye maisha. Na watu namna hii wasipopata msaada wa haraka hufikia kujiua.

iii)              Kufunikwa uso:
Kama tulivyoona kuwa pepo aweza kujigeuza na kuwa. Njia hiyo shetani huitumia kufunika uso. Na ndio maana mtu anawezasema ana roho ya kukataliwa kumbe pepo amekuja usoni na kujigeuza kuwa sura nyingine kabisa. Na mpo mtu mwingine anapoongea naye yaani hisia tu zinakuja,  kuwa anaongea na kitu kingine, kwa njia hiyo watu wanaanza kujitenga naye. Kumbe ni pepo aliyejigeuza na kuwa uso bandia.

Tabia ndiyo ambayo Yule pepo kwenye kitabu cha (1wafalme 22:19-23). Alivyofanya. Kumbe unaweza kumuona mtu anatukana matusi ya ajabu kumbe pepo kajigeuza kuwa kinywa chake usoni. Mapepo waweza kujigeuza maumbo mbalimbali, kama nyani, samba, paka hata bundi ilimradi kuharibu hatma ya mtu. Mnamkuta dada aolewi kumbe uso wake umefunikwa kwa sura ya simba, kila mwanaume anayetaka kumchumbia haoni sura nzuri bali anaona simba. Na ndio maana kuna baadhi ya wadada watumia muda mwingi kufanya kujipodoa lakini bado, kumbe wamefunikwa.

"KWA KUSUDI HILI MWANA WA ADAMU ALIDHIHILISHWA, ILI AZIVUNJE KAZI ZOTE ZA IBILISI"

barikiwa.....



No comments:

Post a Comment