GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Wednesday, August 8, 2012

UJUMBE: MAUTI NA KUZIMU

Na Mch. Kiongozi : Josephat  Gwajima. 15/4/2012

UTANGULIZI:
Kila jambo lina nguzo linazozitegemea, na kila utawala una nguzo unaotegemea.. vilevile utawala washetani umejengwa juu ya nguzo ziitwazo MAUTI na KUZIMU.. Ayubu 38:18 na nguzo hizi mbili ndizo ambazo zinashikilia utawala wa shetani na ndio maana maeneo mengi ambayo kuzimu inatajwa basin a mauti ipo pia.. mfano katika kitabu cha zaburi 116 :3 .. HAPA UTAONA kila mahali ambapo mauti imetajwa basi kuna mahusiano na kuzimu .

MAANA YA MAUTI NA KUZIMU:
Mauti  ni roho ambayo kazi yake ni kuuondoa uhai ulio ndani ya mtu. Na KUZIMU ni roho ambayo kazi yake ni kuwahifazi wale waliokufa.. ufunuo 6: 9, Isaya 28 :15 ..

 Mauti ni roho yenye akili na yenye kupanga.. ndio maana wanafunzi wa Yesu , walipomuona Yesu yuko juu ya maji, biblia inasema wanafunzi wa Yesu wakadhani wameona roho.. kumbe roho ina personality ina akili kili, inaweza kupanga na kutekeleza na pia yaweza kumpagaa mtu. Kwahiyo mauti ni roho yenye personslity hapo tunaweza sema mauti ni mtu.. Tunaweza sema mauti ni mtu ina “personality”  ufunuo 20 : 13.. mauti inaweza kumeza watu..

ufunuo 20 : 14 kila mahali inapotajwa mauti kuzimu inafuata pale, hii inaonyesha kuwa mauti inaanza alafu kuzimu inafuata..  katika hiki kitabu cha ufunuo 20 : 14 tunaona kuwa “ mauti na kuzimu vikatupwa kwenye jehanamu” kumbe mauti unaweza uka ikamata kabisa na kuitupa mahali.. kama mauti na kuzimu vingekuwa ni matukio basi visingeweza kushikwa na kutupwa kwenye moto. Ndio maana Yesu alipokufa alishinda mauti na kuzimu. ( yohana 20 :3)

tuangalie hili andiko mwanzo 37:25   katika agano la kale kuzimu lilikuwa linatumika kama mahali wafu walipokuwa wanakwenda, na palikuwa panaitwa “sheol” kwa lugha ya kingereza na huko wako wafu wote waliotenda haki na walitenda maovu walikuwa wanakwenda kule.. lakini palikuwa wamepagawa mahali pa watenda haki na mahali pa watenda maovu.. na mahali walipokuwa wanaenda watenda palikuwa panaitwa Kifuani pa Ibrahimu, ( yaani wale walioamua kuungana na imani ya Ibrahim) na sasa kunaitwa paradiso..

TOFAUTI YA JEHANAMU NA KUZIMU:
Jehanamu ni shimo la rohoni la moto watakapo angamizwa watu watendao dhambi, kwasasa jehanamu hakuna mtu ndani maana hukumu bado haijatolewa lakini watu wanaokufa kwa sasa wanaenda kuzimu (bottomless pit) hii ni roho iliyojifunua kama shimo.  Isaya 14:11,15 . tunaona shetani alipoasi akatupwa kwenye hilo shimo ndio maana ya maneno yaliyo katika kitabu cha ufunuo 12:7-9 kumbe kuzimu ipo hapa katika nchi, hapaonekani kwa kuwa lipo katika ulimwengu wa roho. Ufunuo 9:15 , KUZIMU ndio kwenye makao makuu ya shetani , wanakofanyia kazi zao.. (operation centre) ufunuo 17:8 .. kwa hiyo ni muhimu kujua kuzimo ipo angani, baharini na hata kwenye nchi.. ndio maana biblia inataja mara nyingu neon hili wakuu wa anga’

KAZI ZA MAUTI NA KUZIMU:
 Kuzimu ndio inayo achilia uovu duniani, inaachilia magonjwa, tabu, dhambi, mateso, balaa,mikosi, ukimwi, kuchanganyikiwa, kuchukiwa na watu, inadhoofisha, inatesa na inaleta uhalibifu.. kwahiyo kuzimu inaleta roho ya uzinzi na uasherati, uovu na dhambi na hizi zote zinamfanya mtu kudhoofika na kuishiwa nguvu. Hapo sasa mauti ndo inakuja pale mtu anapokuwa kwenye comma. KWAHIYO kuzimu kazi yake ni kudhoofisha kwanza.. na ndio maana unaweza muona mtu anaumwa hadi kudhoofika sana lakini huyo mtu hafi.. hii ni kwasababu mashetani ya mauti hayajaanza kufanya kazi..

Hapo mgonjwa anapokuwa dhaifu ndipo sasa mauti inakuja na kufanya kazi yake, ya kumuua . na mauti ikifanikiwa kuutoa uhai basi sasa mauti inatuma mapepo wa kuja kumchukua Yule mtu kama alikuwa mtenda dhambi.. na ndio maana utaona kuwa mtu anapotaka kufa waliowengi utawasikia wanasema maneno kama ‘naona giza’ au msinichukue’ basi ujue wakati huo.

Kuzimu inaleta duniani hata mitindo ya kuvaa..   ili kuingiza tamaa za uzinzi na uasherati.. na unapoona tamaa ya dhambi inaongezeka basi jua unakaribia kufa.. kama ulipangiwa kuishi miaka 80 utajikuta unaishi miaka 40.. kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti.

Tumepewa mamlaka dhidi ya mauti na kuzimu, tukiomba kwa Jina la Yesu tunaweza kusambaratisha mauti na kuzimu. LUKA 10:19

UFUFUO NA UZIMA(THE GLORY OF CHRIST (T) CHURCH)
TANGANYIKA PACKERS,
KAWE, DAR ES SALAAM.

2 comments:

  1. thanks, May God bless you for visiting... if you have something encouraging dont hesitate to send it through my email.. :dmgongolwa@gmail.com and i will post..

    ReplyDelete