GOD LOVES YOU/MUNGU ANAKUPENDA

Yohana 3:16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

John 3:16 "For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life.

Saturday, August 25, 2012

KUNENA KWA LUGHA:


Ukiona nzi ameweza kutua katika jiko la mkaa, basi kwa urahisi tu utajua kuwa hakuna moto juu ya jiko hilo. Vivyo hivyo kama ndani ya roho yako hamna moto wa Roho Mtakatifu lazima mapepo watafanya makazi. Ili uweze kupata moto wa Roho mtakatifu ndani yako ni lazima ujazwe Roho Mtakatifu na upate muda wa kutosha wa kuomba kwa kunena kwa lugha.

Unapojazwa Roho Mtakatitifu, huwa haingii kwenye akili, mawazo wala kwenye mwilini mwako bali huingia kwenye roho. Roho Mtakatifu anapoingia ndani huwa anafanya mawasiliano na roho yako. Wakati roho ya mwanadamu inapokuwa inafanya mawasiliano na roho mtakatifu hapo ndipo mtu huyo anajikuta ananena kwa lugha; kwahiyo kunena kwa lugha ni udhirisho kuwa roho ya mwanadamu ina fanya mawasiliano na Mungu. Na ndio maana moja ya udhihirisho kuwa umeokolewa ni kunena kwa lugha (Marko 16:17), kwasababu ukiokoka Roho Mtakatifu anaingia ndani yako.

Katika Biblia; kuna namna tatu ambazo watu walijazwa Roho Mtakatifu; kama ifuatavyo:
i)                   Kuomba mwenyewe:
Siku ya pentekoste, wanafunzi wa Yesu walikuwa wamekusanyika wakiwa wanaomba; (Matendo ya Mitume 2:1-7), kumbe namna ya kwanza ni kwa kuomba mwenyewe, yaani unakuwa unaomba alafu katikati ya maombi Roho Mtakatifu anakuja ndani mwako na hapo unaanza kunena kwa lugha.

ii)                Kuwekewa mikono:
Namna ya pili ya mtu kupokea Roho Mtakatifu kwenye Biblia ni kwa kuwekewa mikono, tunaona katika (Matendo ya Mitume 19:6), Paulo aliwawekea mikono, na alipowawekea wote wakanena kwa lugha, kumbe mtu anaweza kujazwa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono na mtumishi wa Mungu.

iii)              Kulisikia neno la Mungu linapohubiriwa:
Namna nyingine ni kwa kusikiliza neno la BWANA; (Matendo ya Mitume 10:44), hapa tunaona Roho Mtakatifu amewashukia watu wakati Petro alipokuwa akiongea, kumbe unaweza kupokea Roho Mtakatifu kwa kusikiliza neno la Mungu, (Ezekieli 2:2); Mungu aliposema naye Roho ikamwingia, ni kwa kusikiliza neno la Mungu.

Kuna vizuizi vinavyoweza kumzuia mtu asinene kwa lugha; Adui wakuu watatu wanaomfanya mtu asinene kwa Lugha:
i)                   Ujasiri:
Roho mtakatifu ni Roho wa ujasiri, kwa hiyo unapoomba unatakiwa uombe kwa ujasiri. Unapokosa ujasiri wakati kuomba, Roho mtakatifu hawezi kuingia (1Timotheo 1:7), Roho mtakatifu si roho wa kusitasita wala woga bali ujasiri. Mtu aweza kushindwa kunena kwa lugha kwasababu ya kukosa ujasiri.

ii)                Mapokeo:
Maarifa uliyoyapokea zamani yanaweza kukuzuia kunena kwa lugha kwasababu inawezekana kabla ya kuokoka mtu alikuwa ametokea katika dhehebu ambalo halineni kwa lugha, nalo linaweza kuwa kikwazo, (Marko 7:8), maarifa ni jambo muhimu sana kwenye maendeleo ya mtu, unapokosa maarifa sahihi ya neno la Mungu Roho Mtakatifu hawezi kuingia ndani yako.

iii)              Hofu:
hofu inaweza kukufanya ushindwe kupokea Roho Mtakatifu kwasababu ya kuogopa watu watakuonaje, unawaza ukianza kuongea maneno yale watahisije, (Waebrania 10:38) hofu ni adui mkubwa wa kunena kwa lugha kwasababu inakuzuia kujiachia mbele za Mungu.

Kunena kwa lugha ni njia mojawapo ya kufunguliwa kutoka katika vifungo vya rohoni kwasababu unaponena kwa lugha, kimsingi; roho yako inakuwa inawasiliana na Roho Mtakatifu. Na ndio maana nguvu za mtu za rohoni zinategemeana sana na muda anaotumia kunena kwa lugha; kama ukinena kwa lugha kwa saa moja basi utakuwa na upako wa saa moja. Nena kwa lugha muda wa kutosha.

Limetolewa kwenye moja ya masomo ya Mch. Josephat Gwajima:

No comments:

Post a Comment